Kwa ufupi: Bilal alikuwa aondoke CCM...

Mzee Mwanakijiji

Platinum Member
Mar 10, 2006
33,476
39,995
Amekuwa ni chaguo lisilo chaguo; chaguo lililojichagua na kuchaguliwa. Ilikuwa ni "Urais au nothing". Bilali hakuwa na uamuzi wa kurudi bila ya kitu kinachokaribiana na urais. Uamuzi wa Shein kugombea Zanzibar umekuja baadaye sana baada ya kuona kuwa mtu pekee mwenye nguvu Zanzibar kuweza kumrithi Karume ni Bilal hao kina Nahodha na wenzake walikuwa ni wasindikizaji tu.

Hata hivyo Bilal kwa sababu wanazozijua wao alikuwa tayari anaigawa Zanzibar na kugombea kwake Zanzibar kungempa ushindi mwepesi tu Seif. Lakini hakuwa tayari kujitoa safari hii na alijua kabisa nguvu pekee anayoshindana nayo ni ya Rais wa Jamhuri ya Muungano.

Lakini alikuwa anajua vile vile kuwa JK ni dhaifu kwenye masuala magumu. Alijua JK hawezi kufanya kazi kukiwepo na dissent ya kweli ndani ya CCM, dissent ambayo kwa mara ya kwanza ingewapa ushindi rahisi zaidi Zanzibar. Lakini kilichoharibu ni wajumbe wa kutoka Zanzibar walioamua kuondoka juzi kwa hasira kurudi Zanzibar wakiwa na dhamira moja tu nayo ni kuhakikisha Shein hashindi visiwani.

Lakini JK ni mwanasiasa ambaye anatumia nafasi zinazojileta kuzuia migogoro, yuko tayari kumuachilia mtu wake wa karibu aanguke (kama linamletea yeye sifa) na kama kumleta karibu mtu ambaye ni tatizo kwake.

Sasa, Bilal ni chaguo lililojichagua; hawakumpa nafasi JK kumchagua mtu mwingine, asingeweza kumchagua mtu mwingine; hakukuwa na uwezekano wa kumchagua mtu mwingine.

Ni jinsi gani hawa wawili watafanya kazi? Ni jinsi gani wataweza kupatana?

Well.... Wamarekani wanasema... "Politics make strange bedfellows"..

Historia itaamua.

MM
 
Yet another weakness by Mr President. But again, these are party politics and nothing to do with effective service delivery to the people of Tanzania.
 
hadi jana mchana seif khatib aikuwa atangazwe kuwa mgombea mwenza , hali ya zanzibar ikazidi kuchafuka JK yakamfika shingoni wazee wakamwita out akapewa jina la billal kwa nguvu na amemtangaza kama mgombea mwenza kwa shingo upande tu :pound:
 
MM, mimi nadhani hawa jamaa wa CCM walitaka kucheza karata za kisiasa, karata za kutuliza mambo visiwani. Kwa jinsi ilivyo walitaka kutuliza kiu ya wapemba ambao wamekuwa wakilalamika kuwa hawapati nafasi za uongozi a.k.a urais. Tatizo ni kuwa CCM hawapo tayari kumpa mgombea wa CUF nafasi kama hiyo, kwahiyo Shein akatumwa kwa vile anaonekana kuwa na sifa hata kama si lazima ziwe za kweli. Kwa bahati mbaya Seif anatoka pemba kwa hiyo njia nyepesi ya kupunguza au kugawa kura za pemba ni kupitia Shein. Hapa ndipo karata mbovu ilipochezwa kwasababu unguja kwa mazoea wanadhani ndio wazanzibar na rais lazima atoke hapo. Kitakachofuata ni CCM kupoteza majimbo ya unguja kwa kura za hasira.
Kama upinzani ungekuwa unajua kusoma alama za nyakati hili la dodoma ni ''gross mistake'' na wange tumia fursa hii kuingia ikulu kiulaini. Bahati mbaya hakuna mkakati wa hilo. Nasema hakuna mkakati kwasababu hata huku bara upinzani umedoorora. Kama ingelikuwa nchi za wenzetu wanaojua kucheza na politics JK asingerudi magogoni. JK amezungukwa na ushahidi wa kutosha kabisa kuwashawishi wananchi kuwa ameshindwa kazi lakini wapinzani wamelala hadi october 22 ndipo waanze kampeni.
Mfano mzuri kama JK antumia data za kupika kuwa uchumi umekuwa kwa asilimia 6.4 kwanini wapinzani wasiwaambie wananchi kuhusu inflation toka 7 hadi 11.
Kwanini wapinzani wasitumie data kuonyesha mamilioni yanavyotafunwa!
Kwanini wapinzani wasieleze uzembe wa serikali kama kupoteza bilioni 200 kwa fuel adulteration
Kwanini wapinzani wasieleze wananchi kuwa fenicha :sick: za ofisi moja zinajenga zahanati.
Kwani wapinzani wasieleze wananchi kuwa hela za vitafunio vya chai ni kubwa kuliko thamani ya vijiji vyao.
etc etc etc....

Wapinzani kama mtaenda na sera za kinadharia asilimia 70 wanafuata mkumbo na hawatawaelewa, waambieni wananchi uhalisia wa maisha yao na umasikini wao na si wa taifa. Nina uhakika ukimweleza mwananchi kuwa thamani ya VX moja ni sawa kujenga madarasa 50 au zahanati 10 watawaelewa. Lakini si Singara wala zinduka hatuzisikii tena.
This year was an opportunity to reclaim our country from fisadi but it seems as if we have long way to go.
 
Duh what a calculated move! Sasa 2015 imekuwa ni kama kitendawili. Nahisi 'Pweza' ataonyesha Shein kuwa rais wa URT 2015!
 
MM, mimi nadhani hawa jamaa wa CCM walitaka kucheza karata za kisiasa, karata za kutuliza mambo visiwani. Kwa jinsi ilivyo walitaka kutuliza kiu ya wapemba ambao wamekuwa wakilalamika kuwa hawapati nafasi za uongozi a.k.a urais. Tatizo ni kuwa CCM hawapo tayari kumpa mgombea wa CUF nafasi kama hiyo, kwahiyo Shein akatumwa kwa vile anaonekana kuwa na sifa hata kama si lazima ziwe za kweli. Kwa bahati mbaya Seif anatoka pemba kwa hiyo njia nyepesi ya kupunguza au kugawa kura za pemba ni kupitia Shein. Hapa ndipo karata mbovu ilipochezwa kwasababu unguja kwa mazoea wanadhani ndio wazanzibar na rais lazima atoke hapo. Kitakachofuata ni CCM kupoteza majimbo ya unguja kwa kura za hasira.
Kama upinzani ungekuwa unajua kusoma alama za nyakati hili la dodoma ni ''gross mistake'' na wange tumia fursa hii kuingia ikulu kiulaini. Bahati mbaya hakuna mkakati wa hilo. Nasema hakuna mkakati kwasababu hata huku bara upinzani umedoorora. Kama ingelikuwa nchi za wenzetu wanaojua kucheza na politics JK asingerudi magogoni. JK amezungukwa na ushahidi wa kutosha kabisa kuwashawishi wananchi kuwa ameshindwa kazi lakini wapinzani wamelala hadi october 22 ndipo waanze kampeni.
Mfano mzuri kama JK antumia data za kupika kuwa uchumi umekuwa kwa asilimia 6.4 kwanini wapinzani wasiwaambie wananchi kuhusu inflation toka 7 hadi 11.
Kwanini wapinzani wasitumie data kuonyesha mamilioni yanavyotafunwa!
Kwanini wapinzani wasieleze uzembe wa serikali kama kupoteza bilioni 200 kwa fuel adulteration
Kwanini wapinzani wasieleze wananchi kuwa fenicha :sick: za ofisi moja zinajenga zahanati.
Kwani wapinzani wasieleze wananchi kuwa hela za vitafunio vya chai ni kubwa kuliko thamani ya vijiji vyao.
etc etc etc....

Wapinzani kama mtaenda na sera za kinadharia asilimia 70 wanafuata mkumbo na hawatawaelewa, waambieni wananchi uhalisia wa maisha yao na umasikini wao na si wa taifa. Nina uhakika ukimweleza mwananchi kuwa thamani ya VX moja ni sawa kujenga madarasa 50 au zahanati 10 watawaelewa. Lakini si Singara wala zinduka hatuzisikii tena.
This year was an opportunity to reclaim our country from fisadi but it seems as if we have long way to go.

Duh, umeshachangia CHADEMA?
 
Bilal angeweza ingia kwenye kundi la wenye uchu wa madaraka kama angetoka CCM kisa tu hajachaguliwa kuwa mgombea urais. Kwa hivyo basi, sidhani kama sifa ya Bilal ni uchu wa madaraka hivyo hata kama angekosa kuteuliwa kugombea nafasi ya urais Zanzibar, au hiyo aliyopata ya ugombea mwenza wa Rais wa JMT (makamu wa rais) asingejitoa CCM.
 
Nakubaliana na wewe MKJJ kuwa Bilal hakuwa chaguo la Kikwete na hii imedhihirisha wazi kumbe kuna vyeo vya kusafisha roho staili ya kina Mwilima na hilo ndilo kosa analolifanya Kikwete.

Kwa kumchagua Bilal Kikwete kameza mfupa na si mbali utamkwaa kooni.
 
Bilal angeweza ingia kwenye kundi la wenye uchu wa madaraka kama angetoka CCM kisa tu hajachaguliwa kuwa mgombea urais. Kwa hivyo basi, sidhani kama sifa ya Bilal ni uchu wa madaraka hivyo hata kama angekosa kuteuliwa kugombea nafasi ya urais Zanzibar, au hiyo aliyopata ya ugombea mwenza wa Rais wa JMT (makamu wa rais) asingejitoa CCM.

basi neno "uchu wa madaraka" limepoteza maana.
 
hadi jana mchana seif khatib aikuwa atangazwe kuwa mgombea mwenza , hali ya zanzibar ikazidi kuchafuka JK yakamfika shingoni wazee wakamwita out akapewa jina la billal kwa nguvu na amemtangaza kama mgombea mwenza kwa shingo upande tu :pound:

Kila siku yeye ndio anaonewa, sio makosa yake ni washauri...haya!
 
Ndio maana kwenye magenge wanasema yuko kama picha tu, wanaoendesha nchi ni wengine. What does this guy stand for ?? I wonder!? Bora siku imepita, mbeleni mtajua baadaye na shilingi inazidi kuanguka, maisha yanazidi kuwa magumu.... Lakini atashinda kwa kishindo tu, Tanzania nchi yangu, hili balaa gani
 
Watajijua huko huko magogoni :sick:

Hili ndilo neno. Hawana hata chembe ya kufikiria maisha ya Watanzania kwa hiyo waache tu waendelee na upuuzi wao ingawa unasababisha madhara makubwa kw anchi yetu na wananchi walio wengi.

Hivi gharama za mkutano mkuu wa porojo kama huo ni shs ngapi?
 
Back
Top Bottom