Petro E. Mselewa
JF-Expert Member
- Dec 27, 2012
- 10,174
- 25,446
Natazama kwa hicho la tatu kitendo cha wanasiasa mbalimbali wa upinzani kuhamia CCM. Naona ni kama bahati iliyomfikia Mhe Rais na hata CCM anayoiongoza katika kuwapata wateule wake.
Tangu mwaka 2015, Mhe Rais na CCM kwa ujumla wake umepata wateule kwenye nafasi mbalimbali za kiuongozi na katika kutimiza matakwa na dhima ya kuunda Serikali. Hadi sasa waliokuwa Wapinzani wameteuliwa kwenye nafasi mbalimbali.
Kuna Manaibu Mawaziri (Waitara na Shonza); Katibu Mkuu wa Wizara (Profesa Mshiriki Kitila Mkumbo); Balozi(Dr. Slaa); Mkuu wa Mkoa(Mama Mghwira); Katibu Tawala wa Mkoa(Kafulila); Wakuu wa Wilaya(Katambi na Mtatiro); MaDAS (mfano Mtela Mwampamba) na kadhalika.
Kwangu mimi huo ni ushahidi kuwa Upinzani uliwaandaa, kuwalea na kuwapika wahusika hao na kuwapa sifa za kiuongozi. Ndiyo maana Mhe Rais na CCM kwa ujumla wameridhika nao na kuwakabidhi nafasi hizo za kiuongozi. Mimi siwaiti Wasaliti wa upinzani ni fursa iliyopatikana kwa CCM ambayo 'haikuwa na watu kama hao'.
CCM wamekwama wapi katika kupika vijana na kuwakomaza kuwa na sina za kiuongozi kama hao waliotoka Upinzani? CCM ilikwama wapi kuwa na watu wazima kwenye sifa na kaliba hizo ili kuonwa na kuaminiwa na Mhe Rais? Kimsingi, sifa ziende kwa Upinzani, jiko lenye kuivisha wengi!
Tangu mwaka 2015, Mhe Rais na CCM kwa ujumla wake umepata wateule kwenye nafasi mbalimbali za kiuongozi na katika kutimiza matakwa na dhima ya kuunda Serikali. Hadi sasa waliokuwa Wapinzani wameteuliwa kwenye nafasi mbalimbali.
Kuna Manaibu Mawaziri (Waitara na Shonza); Katibu Mkuu wa Wizara (Profesa Mshiriki Kitila Mkumbo); Balozi(Dr. Slaa); Mkuu wa Mkoa(Mama Mghwira); Katibu Tawala wa Mkoa(Kafulila); Wakuu wa Wilaya(Katambi na Mtatiro); MaDAS (mfano Mtela Mwampamba) na kadhalika.
Kwangu mimi huo ni ushahidi kuwa Upinzani uliwaandaa, kuwalea na kuwapika wahusika hao na kuwapa sifa za kiuongozi. Ndiyo maana Mhe Rais na CCM kwa ujumla wameridhika nao na kuwakabidhi nafasi hizo za kiuongozi. Mimi siwaiti Wasaliti wa upinzani ni fursa iliyopatikana kwa CCM ambayo 'haikuwa na watu kama hao'.
CCM wamekwama wapi katika kupika vijana na kuwakomaza kuwa na sina za kiuongozi kama hao waliotoka Upinzani? CCM ilikwama wapi kuwa na watu wazima kwenye sifa na kaliba hizo ili kuonwa na kuaminiwa na Mhe Rais? Kimsingi, sifa ziende kwa Upinzani, jiko lenye kuivisha wengi!