Kwa teuzi hizi; Rais Magufuli ni mwanademokrasia kuliko Kikwete?

kirerenya

JF-Expert Member
Aug 27, 2013
1,696
2,251
Habari wakuu,
Tumeshuhudia teuzi katika serikali ya awamu ya tano inayoongozwa na Dr John Pombe Magufuli. Tofauti kabisa na matarajio yetu na wengi ameweza kuteua wapinzani kuingia katika serikali yake tena, tena amethubutu kabisa kuweka mpinzani kuwa kiongozi mkubwa wa mkoa.

Tunaona kwenye uteuzi wa huyu mama Anna Elisha Mghwira, mkuu mpya wa mkoa wa Kilimanjaro. Pia tumeweza kuona katibu mkuu wizara ya maji na umwagiliaji Prof Kitila Mkumbo.

Mheshimiwa Magufuli pia siku za nyuma mtakumbuka alimteua mwenyekiti wa TLP Mh Agustino Lyatonga Mrema kuwa mwenyekiti wa bodi ya taifa ya Parole. Zaidi ya hayo Rais Magufuli alidiriki kuruhusu wimbo wa wimbo wa Ney wa Mitego ambao ulikuwa na baadhi ya maneno yaliyoonekana kuwa na ukakasi kwa serikali yake.

Mambo kama haya hayakuonekana kwa sana kipindi cha Mh Kikwete japo uteuzi wa mpinzani ninaokumbuka ni wa mwenyekiti wa NCCR-Mageuzi Mh James Mbatia kuwa mbunge wa kupitia zile nafasi kumi za rais.

Pamoja na ukweli kuwa Mh Magufuli ameonekana kuwa mwiba mchungu kwa demokrasia kupitia matamshi yake, lakini matendo yake yanaonesha dhahiri kuwa yeye ni mwanademokrasia mzuri sana.

Je, haitoshi kusema Mh Magufuli ni mwanademokrasia kuliko mtangulizi wake Dr Jakaya Kikwete?
Nawasilisha..
 
Huu uteuzi umefanywa ili kutusahaulisha na swala la mchanga wa madini maana inaonyesha kuna jambo limefanywa kwakukurupuka,hatupendi kuibiwa mali zetu lakini kuna kitu tumedanganywa so huu uteuzi ni funika kombe mwanaharamu apite
 
Swala la uteuzi tu ndo limekufanya uone ni mwanademokrasia bora,habari gani juu ya manyanyaso kwa wapinzani au ile ni democracy?
 
Swala la uteuzi tu ndo limekufanya uone ni mwanademokrasia bora,habari gani juu ya manyanyaso kwa wapinzani au ile ni democracy?

Lakini Magufuli ana mikwara tuu kwa wapinzani, kimatendo anaonekana mwanademokrasia
 
Hivi nani aliapa kule Zanzibar kuwa hawezi kumchagua mpinzani kwenye serikali yake?

Ni kweli ni yeye JPM aliyeapa kwamba hatochagua wapinzani, na mpaka sasa hajafanya hivyo. Hao aliochagua wanaitwa "wapinzani" na sio wapinzani, kama unaelewa kinachoendelea.
 
Ni kweli ni yeye JPM aliyeapa kwamba hatochagua wapinzani, na mpaka sasa hajafanya hivyo. Hao aliochagua wanaitwa "wapinzani" na sio wapinzani, kama unaelewa kinachoendelea.
Ukimaanisha nini mkuu?
 
Demokrasia maana yake ni nini? Kuna aina ngapi kuu za demokrasia? Tanzania inafuata demokrasia ya aina gani kwa mujibu wa katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania?
 
Ukimaanisha nini mkuu?

Ni wewe tu ndio umeshindwa kuelewa, mpaka sasa rais bado hajachagua wapinzani. Mrema (TLP), kitila na Mghwira (ACT) sio wapinzani, kwa maana ya kwamba hawamchallenge wala kumpinga kwa lolote, na hao ndio aina ya "wapinzani" utakao waona kwenye serikali yake.
 
Alama tatu za Mnafiki:

(1) Akizungumza husema uongo
ref: Alisema hatochagua upinzani sasa amechagua... Huu ni Uongo.

(2) Akiahidi hatimizi
ref; Aliahidi milioni 50 kila kijiji, kusitisha ajira kwa mwezi mmoja n k Yote hakutekeleza.

(3) Akiaminiwa hufanya khiyana.
ref. Kauli yake kuhusu michango ya maafa kule Kagera.
 
2 Reactions
Reply
Back
Top Bottom