Kwa staili hii maazimio ya mkutano mkuu wa CCM utekelezaji wake utakuwa kizungumkuti

sammosses

JF-Expert Member
Jan 24, 2011
1,682
1,110
Tumeona tumeshuhudia yanayojiri kutokana na maazimio ya mkutano mkuu na nimegundua kuwa utekelezaji wake utakuwa ni kizungumkuti.Nasema hivi baada ya kuhudhuria moja ya mikutano ya hadhara ambayo ndiyo effectively impact ya maazimio yaliyo kusudiwa.Kinacho jiri baada ya mkutano mkuu ni tofauti na kazi waliyotumwa wajumbe wa NEC katika kukiimarisha chama. Mwenyekiti wa taifa CCM alisema chama kimepoteza taswira yake,kiasi kimekimbiwa na wanachama wake.

Ina hitaji nguvu ya ziada ya kimkakati kurudisha imani ya wananchi ili waweze kuiamini serikali yao waliyoichagua wakiamini serikali hiyo itatekeleza yale wananchi waliyoyakusudia.Alifika mbali kwa kuwataka wajumbe wa NEC na viongozi mbalimbali wa CCM kujibu tuhuma zinazoelekezwa kwa CCM kutoka kwa wapinzani wao. Kinyume na jitihada za kukiokoa chama wajumbe waliochaguliwa na kupewa majukumu wameshindwa kuendeleza yale ambayo waliyoyaagizwa na M/kiti na mkutano mkuu.Chama kinatuhumiwa kuwakumbatia wahalifu wenye mikono michafu na kuwapa nafasi za uongozi ilihali hawana status quo katika jamii walizotoka,matokeo yake ni chama kuzidi kujichimbia kaburi lake.

Kushindwa huku mapema kabla hata mwezi haujapita tangu kumalizika mkutano mkuu ni dalili mbaya kwa CCM kuelekea 2015.Jana nili hudhuria mkutano wa hadhara ambao agenda kuu ya mkutano mkuu huo haikujulikana pamoja na kuwa walipokea wanachama ambao wanaosema walikuwa vyama vya upinzani wakitokea CCM lakini hatimaye wamerudi tena. Mbali na hayo protocol haikuzingatiwa na kila mtu alivamia jukwaa kutaka kuongea bila utaratibu kama vile chama hakijui taratibu za vikao.Ni hivi punde mmoja wa wajumbe wa NEC kutoka wilaya ya Shinyanga mjini alituhumiwa kuwa ana mikono michafu,lakini akiwa ndiye mgeni rasmi alishindwa kujibu tuhuma hizo zaidi ya kuitaka chombo cha dola kuwachukulia hatua za kisheria wale wote waliyojitangazia Ngokolo ni jamhuri.Ikiwa wajumbe wote wa NEC toka wilaya ya Shinyanga wana tuhuma za mikono michafu hivi kweli chama hiki kitabaki salama.

Wameagizwa kushughulikia matatizo ya wananchi na kuyapeleka serikalini kwa kutumia vikao vyao,lakini ajabu majukwaa haya ya mikutano ya hadhara nayo yameingia mkenge kumtuhumu mtu binafsi kama Dr. Slaa kuwa ni mwanachama wa CCM bila kutatua matatizo ya watu wa Shinyanga,ili yaweze kutatuliwa na serikali kama walivyoagizwa.Dr. Slaa kuwa na kadi au kutokuwa na kadi ya CCM kunatatua vipi tatizo la maji mkoani hapa ilhali kuna mradi wa maji mkubwa toka ziwa Victoria uliogharimu mabilioni ya pesa ambao hauna tija kwa watu wa mkoa huu. Pesa kiasi gani za miradi ya maendeleo ambazo zinahujumiwa na miradi mingi kukwama.

Kiko wapi chuo chenu cha viongozi ambacho mwalimu alikitumia kupika viongozi waadilifu na wazalendo. Hivi kama Mwalimu angejaza mafisadi ndani ya CCM kwa miaka ile nchi kweli ingefika hapa tulipo? CCM kwa kuwatumia wajumbe wenu wapya ambao mnaamini pesa zao chafu ndizo zitakazo weza kuwavusha 2015 basi mna kazi ya ziada,kwani hata kitendo cha kuwarubuni wananchi warudi ndani ya CCM kwa staili ya kupewa mapesa si suluhisho la matatizo ndani yenu.Watarudisha kadi lakini mapenzi na imani kwa vyama vingine vitabaki pale pale.
 
Jina la Dr Slaa kwa sasa limekuwa ni tishio kwa matapeli wa nchi hii!!! Wakilala, wakiamka hawana raha na Dr Slaa!!! Utadhani jina hili "Dr Slaa" lilikuwa ni mojawapo ya ilani ya uchaguzi ya CCM. Ilani zao zote walizoahidi kuzitekeleza hazijulikani zimeyeyukia wapi. Sasa wamebaki na ilani moja tu, "Dr Slaa". Hawana amani mioyoni mwao kwa vile wanajua huyu ndiye kiongozi thabiti atakayerudisha maadili ya kitaifa!
 
Waacha waendelee kumtangaza Dr Slaa, Kurudisha Imani kwa wananchi wanatakiwa waitekeleze Ilani yao ya uchaguzi, ili waweze kufanya maisha bora kwa watanzania lakini wakiendelea na hii tabia kiama kinakaribia, Ndani ya chama cha mapinduzi kuna wasanii wengi sana yaani wanaishi kimjini mjini na kuna watu wazuri ambao wanaweza kuokoa jahazi hili lakini hawapewi nafasi.
 
Jina la Dr Slaa kwa sasa limekuwa ni tishio kwa matapeli wa nchi hii!!! Wakilala, wakiamka hawana raha na Dr Slaa!!! Utadhani jina hili "Dr Slaa" lilikuwa ni mojawapo ya ilani ya uchaguzi ya CCM. Ilani zao zote walizoahidi kuzitekeleza hazijulikani zimeyeyukia wapi. Sasa wamebaki na ilani moja tu, "Dr Slaa". Hawana amani mioyoni mwao kwa vile wanajua huyu ndiye kiongozi thabiti atakayerudisha maadili ya kitaifa!

Ila kwa upande mwingine ni vizuri maana wanamfanyia kampeni ili afahamike vizuri..CDM wasifanye kosa kwakweli maana ameshakuwa advertized vyakutosha....
 
Hata zile methali za wahenga zilizosema samaki hujikaangaa kwa mafuta yake mwenyewe sasa zina thibitisha uhalisia wa misemo hii ya hekima iliyotumiwa na wazee wetu toka enzi hizo.Wamesahau kutekeleza yale waliyoyaahidi na kumfanya Dr. Slaa kuwa agenda kuu ndani ya CCM.Mbaya zaidi hata viongozi wa juu wa CCM wameshindwa kuuepuka mtego huu wa kumanadi Dr. Slaa.Lakini wakumbuke kuwa siku zote chema cha jiuza kibaya cha jitembeza.
 
Dr Slaa hana uwezo wa kuibeba CDM 2015; lakini kwa kuwa watu kwa maksudi hawapendi kuzisoma nyakati wanamg'ngania watashangaa.
 
Dr Slaa hana uwezo wa kuibeba CDM 2015; lakini kwa kuwa watu kwa maksudi hawapendi kuzisoma nyakati wanamg'ngania watashangaa.

sisi tunamuona Dr slaa ni jembe la kweli na anatufaa, je wewe unadhani nani anakufaa tupia jina mkuu
 
Sijawahi kuwa na imani na CCM tangu 2005 hivyo,hata wakifanya maazimio gani hawana ubavu wa kuyasimamia na kuyatekeleza
 
Dr Slaa hana uwezo wa kuibeba CDM 2015; lakini kwa kuwa watu kwa maksudi hawapendi kuzisoma nyakati wanamg'ngania watashangaa.

tupe vigezo man,humu tuna kwenda kwa vigezo positive and negative comments why he does not hold his party
 
Tunapo sema CCM wameishiwa sera hatubabaishi,tunamaanisha hasa.Tumeona kauli mbiu zao ambazo zimekuwa zikishindwa kutekelezeka kabla hata ya kipindi walichoahidi hakijaisha.Nchi haipelekwi kwa kauli mbiu tunataka kujua nini hasa sababu za uamsikini huu uliowagubika wananchi ilihali nchi ni tajiri wa rasilimali.

Kauli mbiu ya maisha bora kwa kila Mtanzania yanawezekana imefia wapi,Watanzania hawataki kusikia wapinzani wamefanya nini wanataka kusikia ilani yenu ya CCM mliyoinadi kwa nguvu zaidi ari zaidi na kasi zaidi mbona imeshindwa kwa nguvu kubwa zaidi,kasi kubwa zaidi na ari kubwa zaidi kiasi sasa kauli mbiu hiyo umehamishia kwenye malaria.Eti utasikia Tanzania bila malaria yawewzekana.

Tuliaminishwa enzi ya TANU kuwa maadui wakubwa katika nchi hii ni ujinga,maradhi na njaa nk,lakini pia tuliambiwa kuwa ili tuendelee tunahitaji watu,ardhi,siasa safi na uongozi bora.Lakini ajabu na kweli haya serikali yetu imeshindwa kuyatafutia mbinu mbadala hasa ukizingatia wakati ule teknolojia ili kuwa chini tofauti na hivi sasa.

Leo nchi hii inaongoza kwa njaa ilihali rais ana jinasibu mtandao wa barabara ni mkubwa,sawa ni mkubwa unasaidiaaje katika kukiinua kilimo chetu kiwe ni chenye tija.Ardhi ilikuwa kigezo kikubwa kama chachu ya maendeleo lakini ardhi hii Watanzania sana sana tunaitumia kwaajili ya kuzikana na sehemu kubwa tumemilikisha wakoloni wa kileo(wawekezaji).Uongozi bora hapa ndiyo tume prove zero kabisa,maana hawa tulionao tusipokuwa makini ipo siku tutaamkaa asubuhi nasi tumeuzwa.

Nchi imekuwa ya udalali kila kona,nchi inaongoza kwa deal zisizo na tija kwa wanachi wake.Vikao vimekuwa badala ya kujadili matatizo yanayo ikumba nchi hii,vimekuwa ni vikao vya posho na kutajirishana.Viongozi hawa hawa wanaanzisha vitengo magumashi ili kuweza kulinda maslahi yao wanapokuwa na wanapotoka madarakani,mfano TAKUKURU.
 
Kilicho cha msingi lazima Watanzania tuwe priceless,lakini kama tutaendelea kuivalia njaa kibwaya hakika wataendelea kula mpaka wavimbiwe maana hivi sasa tu hawajali hata kunawa,wanacho jali ni tonge kwenda mdomoni.
 
Back
Top Bottom