Kwa spidi hii Rwanda watatuacha

Game Theory

JF-Expert Member
Sep 5, 2006
8,545
833
Naam baada ya baadhi ya watu humu kuacha vivywa wazi kwenye ile thread ya Viwanda vya Sudan sasa someni VISHINDO vya wanyaRWANDA hii nimeiata toka kwa mwenzetu YAKUBU ambaye alikwepo na mhishimiwa KAGAME alipokwenda London

Msafara mzito wa Rais Paul Kagame na viongozi wa serikali ya Rwanda leo hii umefanya mkutano mkubwa hapa London na wawekezaji/wanaotaka kuwekeza Rwanda ambapo serikali imeainisha maeneo makuu yanayoweza kuvutia wawekezaji. Ikiwa ni mara ya kwanza kufanyika hapa UK na kwangu kuwa ni mara ya kwanza kumuona Rais Paul Kagame ''in action'' kuna mambo kadhaa yamenivutia:

1. Ukweli kwamba alikataa kuwa mzungumzaji mkuu katika mkutano huo kwa vile alitaka kusikiliza zaidi hasa fursa ya maswali na maoni kujua nini hasa wawekezaji wanataka na vipi Rwanda inaweza kusaidia. Alipotakiwa kusalimia alitaja mambo mawili ya msingi:
- Alisema Rwanda inakerwa na hali ya utegemezi na wanajitahidi kuondokana nao, mwaka 1994 walikuwa wakitegemea misaada toka nje kwa 99% hivi sasa 49%


- Alitoa hadithi ya wawekezaji waliotaka kununua kahawa kwa centi 90 za dola wakiahidi kujenga shule,hospitali nk akawaambia huo utakuwa bado ni utegemezi bado ''tulipeni dola mbili kwa kilo na tutajenga hospitali na shule wenyewe''!

2. Ukweli kwamba wafanyakazi wengi wa ngazi za juu wa Rwanda ni vijana wadogo tu, alikuwepo Mkurugenzi wa Kituo cha Uwekezaji, Naibu Gavana wa Benki Kuu wote wakiwa ni vijana wenye uchungu na maendeleo.

3. Rwanda ili kuondokana na ukabila ingependa kutoa uraia kwa watu wa mataifa mengi zaidi hivyo Rais kawaalika wengi wajitokeze hata kuomba uraia, ''watu wanaona hili ni tatizo mimi naona ni faida kwa nchi mradi wanaopewa uraia wanafuata sheria''

4. Rwanda imejipanga vizuri kutumia vyema Bandari yetu kwa kuuza kwa nguvu zote na kwa msisitizo mkubwa kuwa Reli ya kutoka Isaka-Kigali itawanufaisha wao zaidi kwa vile nchi yao haina bandari. Reli hiyo itagharimu Dola bilioni mbili lakini ina faida kubwa kwa Rwanda na wataigharimia hata kwa mikopo.

5. Ifikapo mwaka 2010 Rwanda itakuwa imeunganishwa na wireless internet nchi nzima!

Katika hali ya kawaida baadhi ya mambo ningeona kwenye mikutano mingine kama ni matamko ya kisiasa tu lakini pale palikuwa na mikakati ya uhakika...Kwa jinsi mambo yalivyokuwa yakienda katika mkutano huo, wazo la kuendesha serikali kama kampuni katika baadhi ya maeneo ilikuwa na maana kubwa!Mengi katika haya nadhani Tanzania tungeweza kujifunza...


SOURCE:

http://www.saidiyakubu.blogspot.com/
 
Wireless internet can be achieved very easily because you will be using the mobile phones communication masts. (i.e. wherever a mobile phone communication is available you can have internet access as well.

Even in developed countries like UK this technology is widely used to compete with landlines. I am wondering why do they take so many years when the technology is easily available.
 
''tulipeni dola mbili kwa kilo na tutajenga hospitali na shule wenyewe''!

Kwa sisi wabongo We should take royalty ya madini kama asilimia kumi tu, hizo shule na mifuko ya uwezeshaji tutachangia wenyewe....
 
GT,
Mie naona kama Tanzania is a sleeping giant! Huenda tukiungana na wenzetu ktk EAF tutapata changamoto na kuanza kushindana!
Good thing..we have more potential of resources than our neighbors!
Tunaanza kuamka..ila taratibu sana!
 
Naam baada ya baadhi ya watu humu kuacha vivywa wazi kwenye ile thread ya Viwanda vya Sudan sasa someni VISHINDO vya wanyaRWANDA hii nimeiata toka kwa mwenzetu YAKUBU ambaye alikwepo na mhishimiwa KAGAME alipokwenda London

Msafara mzito wa Rais Paul Kagame na viongozi wa serikali ya Rwanda leo hii umefanya mkutano mkubwa hapa London na wawekezaji/wanaotaka kuwekeza Rwanda ambapo serikali imeainisha maeneo makuu yanayoweza kuvutia wawekezaji. Ikiwa ni mara ya kwanza kufanyika hapa UK na kwangu kuwa ni mara ya kwanza kumuona Rais Paul Kagame ''in action'' kuna mambo kadhaa yamenivutia:

1. Ukweli kwamba alikataa kuwa mzungumzaji mkuu katika mkutano huo kwa vile alitaka kusikiliza zaidi hasa fursa ya maswali na maoni kujua nini hasa wawekezaji wanataka na vipi Rwanda inaweza kusaidia. Alipotakiwa kusalimia alitaja mambo mawili ya msingi:
- Alisema Rwanda inakerwa na hali ya utegemezi na wanajitahidi kuondokana nao, mwaka 1994 walikuwa wakitegemea misaada toka nje kwa 99% hivi sasa 49%


- Alitoa hadithi ya wawekezaji waliotaka kununua kahawa kwa centi 90 za dola wakiahidi kujenga shule,hospitali nk akawaambia huo utakuwa bado ni utegemezi bado ''tulipeni dola mbili kwa kilo na tutajenga hospitali na shule wenyewe''!

2. Ukweli kwamba wafanyakazi wengi wa ngazi za juu wa Rwanda ni vijana wadogo tu, alikuwepo Mkurugenzi wa Kituo cha Uwekezaji, Naibu Gavana wa Benki Kuu wote wakiwa ni vijana wenye uchungu na maendeleo.

3. Rwanda ili kuondokana na ukabila ingependa kutoa uraia kwa watu wa mataifa mengi zaidi hivyo Rais kawaalika wengi wajitokeze hata kuomba uraia, ''watu wanaona hili ni tatizo mimi naona ni faida kwa nchi mradi wanaopewa uraia wanafuata sheria''

4. Rwanda imejipanga vizuri kutumia vyema Bandari yetu kwa kuuza kwa nguvu zote na kwa msisitizo mkubwa kuwa Reli ya kutoka Isaka-Kigali itawanufaisha wao zaidi kwa vile nchi yao haina bandari. Reli hiyo itagharimu Dola bilioni mbili lakini ina faida kubwa kwa Rwanda na wataigharimia hata kwa mikopo.

5. Ifikapo mwaka 2010 Rwanda itakuwa imeunganishwa na wireless internet nchi nzima!

Katika hali ya kawaida baadhi ya mambo ningeona kwenye mikutano mingine kama ni matamko ya kisiasa tu lakini pale palikuwa na mikakati ya uhakika...Kwa jinsi mambo yalivyokuwa yakienda katika mkutano huo, wazo la kuendesha serikali kama kampuni katika baadhi ya maeneo ilikuwa na maana kubwa!Mengi katika haya nadhani Tanzania tungeweza kujifunza...



sasa hapo kuna nini cha kujifunza ktka kwa huyo kagame na ujumbe wake ndugu muheshimiwa??
 
jamaa wamezamilia kuiniua uchumi wao.la kwanza wametuma vijana wao kusoma nje ya nchi na ni wazalendo sijapata ona baada ya masomo ni nyumbani.kuna jamaa yao mmoja alikuwa engineer CNN ila amekubali kurudi na kulipwa mshahara pungufu nyumbani.Cha msingi ni uzalendo na bidii ya kazi na wamefanikiwa kuiba ujuzi nje maana wako tayari kujifanya raia ila baadae hao nyumbani.Bongo wako kila sehemu USALAMA WA TAIFA hadi IKULU.wenyewe wanajiita WAISRAELI WA AFRIKA.kazi kwenu Watanzania
 
sasa hapo kuna nini cha kujifunza ktka kwa huyo kagame na ujumbe wake ndugu muheshimiwa??

Mambo ya kujifunza ni haya:

[Source: Game theory]


Alipotakiwa kusalimia alitaja mambo mawili ya msingi:
- Alisema Rwanda inakerwa na hali ya utegemezi na wanajitahidi kuondokana nao, mwaka 1994 walikuwa wakitegemea misaada toka nje kwa 99% hivi sasa 49%

- Alitoa hadithi ya wawekezaji waliotaka kununua kahawa kwa centi 90 za dola wakiahidi kujenga shule,hospitali nk akawaambia huo utakuwa bado ni utegemezi bado ''tulipeni dola mbili kwa kilo na tutajenga hospitali na shule wenyewe''!

2. Ukweli kwamba wafanyakazi wengi wa ngazi za juu wa Rwanda ni vijana wadogo tu, alikuwepo Mkurugenzi wa Kituo cha Uwekezaji, Naibu Gavana wa Benki Kuu wote wakiwa ni vijana wenye uchungu na maendeleo.

3. Rwanda ili kuondokana na ukabila ingependa kutoa uraia kwa watu wa mataifa mengi zaidi hivyo Rais kawaalika wengi wajitokeze hata kuomba uraia, ''watu wanaona hili ni tatizo mimi naona ni faida kwa nchi mradi wanaopewa uraia wanafuata sheria''

Reli ya kutoka Isaka-Kigali itawanufaisha wao zaidi kwa vile nchi yao haina bandari. Reli hiyo itagharimu Dola bilioni mbili lakini ina faida kubwa kwa Rwanda na wataigharimia hata kwa mikopo.

5. Ifikapo mwaka 2010 Rwanda itakuwa imeunganishwa na wireless internet nchi nzima!
[/QUOTE]

kijakazi kama hizo pointi alizoandika game theory wewe kwako huoni zina mantiki, basi una matatizo ya kutotaka kujifunza.
 
kijakazi kama hizo pointi alizoandika game theory wewe kwako huoni zina mantiki, basi una matatizo ya kutotaka kujifunza.

..ni vijakazi wachache sana wanaojifunza!

..wengi huwa wanatumia muda wao mwingi kumtumikia bwana/bi mkubwa wao!

..si kosa lake!
 
Mbona hawakumuuliza ni kwa nini serikali na jeshi lake limejaa asilimia kubwa ya watusi kuliko makabila mengine? au hapo anatufundisha nini hasa?
 
jamaa wamezamilia kuiniua uchumi wao. la kwanza wametuma vijana wao kusoma nje ya nchi na ni wazalendo sijapata ona baada ya masomo ni nyumbani.kuna jamaa yao mmoja alikuwa engineer CNN ila amekubali kurudi na kulipwa mshahara pungufu nyumbani.Cha msingi ni uzalendo na bidii ya kazi na wamefanikiwa kuiba ujuzi nje maana wako tayari kujifanya raia ila baadae hao nyumbani.Bongo wako kila sehemu USALAMA WA TAIFA hadi IKULU.wenyewe wanajiita WAISRAELI WA AFRIKA.kazi kwenu Watanzania


Hao waliokwenda nje wengi wao walikuwa wakimbizi wa genocide ya 1959 na 1994. I wonder kama hicho ndicho kilichochochea zaidi uzalendo walio nao??
 
Mbona hawakumuuliza ni kwa nini serikali na jeshi lake limejaa asilimia kubwa ya watusi kuliko makabila mengine? au hapo anatufundisha nini hasa?

Watusi ndio waliouwawa na wahutu kwenye mauwaji ya halaiki ya 1994...Jeshi la Kagame la Watusi ndio waliomaliza vita, kweli unategemea jeshi liwe na Wahutu tena?
 
Wireless internet can be achieved very easily because you will be using the mobile phones communication masts. (i.e. wherever a mobile phone communication is available you can have internet access as well.

Even in developed countries like UK this technology is widely used to compete with landlines. I am wondering why do they take so many years when the technology is easily available.


Dua

Uzuri wa Warwanda hawajaishia kwenye kutegemea wireless internet. Hilo ni lengo ambalo kwa sasa ni kama wameshafanikiwa kwa urahisi wa technology yenyewe. Zaidi ya wireless, rwanda wanatandaza fiber-optic rings 2 kuzunguka Kigali; hili linakaribia kumalizika. Baada ya fiber ring kuwa sawia itawagharimu hela ndogo sana kusambaza realible network nchi nzima. Lengo lao la kuwa Internet & Information Gateway kwa nchi za maziwa makuu liko karibu sana kufanikiwa.

Rwanda wana-advantage moja kulinganisha na Tanzania kwenye haya mambo ya Internet infrastructure...nchi yao ni ndogo. That is not an excuse thou...!!
 
Rwanda wana-advantage moja kulinganisha na Tanzania kwenye haya mambo ya Internet infrastructure

..advantage yao kubwa zaidi ni nia ya kweli ya kuendelea!

..matumizi ya ict in bongo yanatia aibu!kwani serikali ndio inayotakiwa ku-spearhead hii kitu!lakini ni kinyume chake hapa!lots of talkshops and nothing on the ground!
 
..Rwanda hata barabara zake sasa ni za maana sana,karibu barabara zote kutoka one district to another ni lami tupu,na shirika lao la ndege sasa ni one of the most efficient & profitable in africa na kwa uwingi wa ndege &routes limezidi Tanzania by far na halitegemei ruzuku ya serikali na sasa wanapanua Airport yao
 
Dua

Uzuri wa Warwanda hawajaishia kwenye kutegemea wireless internet. Hilo ni lengo ambalo kwa sasa ni kama wameshafanikiwa kwa urahisi wa technology yenyewe. Zaidi ya wireless, rwanda wanatandaza fiber-optic rings 2 kuzunguka Kigali; hili linakaribia kumalizika. Baada ya fiber ring kuwa sawia itawagharimu hela ndogo sana kusambaza realible network nchi nzima. Lengo lao la kuwa Internet & Information Gateway kwa nchi za maziwa makuu liko karibu sana kufanikiwa.

Rwanda wana-advantage moja kulinganisha na Tanzania kwenye haya mambo ya Internet infrastructure...nchi yao ni ndogo. That is not an excuse thou...!!

Nafikiri cha msingi ni kuwawezesha WTZ kuwa na kipato cha uhakika na katika hilo kuwawezesha kumudu gharama za kutumia technology katika kuboresha maisha yao. Leo hii hata tukiwa na mawasiliano bure ya internet hadi vijijini itawasaidia wengi kupata mawasiliano lakini kuitumia kwa faida itakuwa ni ngumu kidogo, tuweze kufika mahali na kuwa na njia muhimu za kuwawezesha wengi wafaidi matunda ya nchi yetu na sio walafi wachache ambao wanakwamisha miradi ya kuwakomboa walalahoi.

Angalia jinsi tunavyoshindwa kutatua swala la usafiri wa uhakika wa mazao n.k. Inabidi tuanze sasa kuwa na njia za usafiri wa uhakika, kwa mfano kwa nini usafiri kwa zaidi ya masaa 12 kutoka Dar - Mwanza au kigoma? Mbeya - Mtwara n.k. Iko wapi mipango ya kujenga fast trains kwa nchi nzima? Hili ndilo tunatakiwa kulikodolea macho zaidi maana litawawezesha wengi kuuza mazao yao kwa bei nzuri na kuwakata madalali uchwara. Tukifanikiwa hilo mengine yatajipa tu jinsi tunavyokwenda.
 
Kikwete aende Rwanda ajifunze kwa Kagame

Johnson Mbwambo Juni 10, 2009

Raia Mwema~Muungwana ni Vitendo

MJADALA kuhusu ziara nyingi za nje za Rais Kikwete; hususan za Marekani na Ulaya, umekataa kufa. Mjadala huu unasinzia tu kwa muda; lakini huibuka upya pindi anapofanya safari nyingine ya nje. Na ndivyo ilivyokuwa hivi karibuni alipokwenda tena Marekani (mara ya sita au saba?).

Wananchi wamekuwa wakizijadili safari hizo majumbani, maofisini, vijiweni, kwenye baa, na hata kwenye intaneti. Wako wanaoziunga mkono na wako wanaoziona kuwa ni matumizi mabaya ya pesa za walipakodi.

Katika moja ya hotuba zake Rais Kikwete alipata kujitetea kuhusu safari hizo kwa kutoa mfano wa Soko la Mitaji la Nasdaq alilolitembelea New york, Marekani.

Rais alisema hivi: “Nilipotembelea Soko la Hisa la New York, ambalo biashara yake inazidi dola 22.8 trilioni za Marekani, tulipewa heshima ya kuzindua biashara ya siku ile. Ni kwa sababu nilikuwepo ndiyo maana tulipewa heshima hiyo. Hivi unadhani Jonathan Njau (Mkuu wa Soko la Hisa la Dar es Salaam –DSE), angeweza kukutana na jamaa wale angekuwa peke yake?”

Kauli hiyo ya Rais wala haielezi Tanzania ilinufaika vipi kwa yeye kutembelea soko hilo la mitaji la Nasdaq; ukiachilia mbali kwamba alipewa heshima hiyo ya kufungua rasmi biashara ya siku hiyo.

Kwa hakika, mtu unashindwa kujizuia kujiuliza: Hivi Rais wetu alikatisha bahari ya Atlantic hadi Marekani kwa ajili ya kulitembelea soko la hisa la Nasdaq? Hivi alitaka kujifunza kitu gani hasa kutoka katika soko hilo la hisa linaloongoza duniani ambacho asingeweza kujifunza kutoka katika masoko yaliyoendelea ya mitaji ya baadhi ya nchi za Afrika.

Ni nani asiyejua kwamba tofauti kati ya soko letu changa la hisa la Dar es Salaam (DSE) na lile la Nasdaq la New York, ni tofauti kati ya Mlima na kichuguu?

Kama Rais na ujumbe wake walitaka kujifunza masuala ya masoko ya hisa ili labda waje waisaidie DSE, basi hawakuwa na sababu ya kuvuka bahari ya Atlantic kwa hilo! Kenya tu hapo kuna Soko la Mitaji la Nairobi ambalo ni bora mara 20 kuliko DSE yetu! Na kama hilo la Nairobi haliwavutii, basi kuna jingine la Johannesburg, Afrika Kusini ambalo nalo ni bora mara 30 kuliko la kwetu!

Ninachojaribu kueleza hapa (kwa mfano huo) ni kwamba wakati mwingine watawala wetu hawana sababu yoyote ya kukatisha bahari ya Atlantic kwenda kujifunza Marekani; kwani, kwa baadhi ya mambo, mafunzo yako hapa hapa Afrika; tena wakati mwingine katika nchi jirani tu!

Ndiyo maana siziungi mkono baadhi ya ziara anazozifanya rais wetu. Ningeziunga mkono safari hizo kama zingekuwa ni za kutafuta kweli kweli ‘mwarobaini’ wa kutukwamua ki-maendeleo, na si za kufungua biashara ya siku ya Nasdaq au za kutembeza kwingineko bakuli la ombaomba!

Ningeziunga mkono kama zingekuwa ni za kututafutia teknolojia ya kutengeneza boti na nyavu za uvuvi, na si za kutuombea samaki! Ningeziunga mkono kama zingekuwa za kuwaombea Watanzania wafundishwe namna ya kutengeneza vyandarua (kama hawajui), na si za kuomba msaada wa vyandarua!

Kwa maneno mengine; ningeziunga mkono kama zingelenga kutuletea maendeleo endelevu, na si za kuomba kusaidiwa kutatuliwa shida za muda mfupi za hapa na pale.

Kwa mantiki hiyo hiyo, ningekuwa naziunga mkono kama zingekuwa ni za kwenda katika nchi kama za India, Brazil, Singapore, Malaysia, Korea Kusini, na hata nchi chache za Afrika, kudadisi na kujua ni kwa nini wenzetu walifanikiwa kupata maendeleo katika kipindi kifupi wakati sisi tumekwama.

Miaka si mingi sana iliyopita, nchi hizo zilikuwa hazitofautiani sana nasi ki-maendeleo; lakini zilipozinduka, zilipiga kasi ya maendeleo haraka na kutuacha mno nyuma. Zilikuwa dunia ya tatu kama sisi, lakini sasa zinabisha hodi dunia ya kwanza; huku zikituacha sisi pale pale!

Nchi kama Malaysia na Korea Kusini tulikuwa kiwango kimoja cha maendeleo mwaka 1961, lakini sasa ni tajiri kutuzidi mara 20 (msome Robert Guest katika kitabu chake The Shackled Continent).

Lakini hata Afrika, kuna baadhi ya nchi ambazo tunaweza kabisa kujifunza kitu. Moja ya hizo ni Rwanda. Miaka 13 iliyopita Rwanda ilianza upya (majivuni) baada ya kuharibiwa vibaya na vita na mauaji yale ya kimbari ya mwaka 1994 yaliyosababisha vifo vya Watusi na Wahutu wenye msimamo wa kati, zaidi ya 800,000.

Lakini leo hii, Rwanda iko mbali mno kimaendeleo (hasa vijijini) kutuzidi. Alichoweza Rais Kagame kukifanya Rwanda katika miaka 13, ni kile ambacho sisi, kama Taifa, tumeshindwa kukifanya kwa miaka 20 iliyopita. Na wala hatujasikia Rais Kagame akienda, mara kwa mara, Marekani au Ulaya!


Mwaka 2004 nilikuwa mmoja wa wahariri wachache wa Tanzania tulioalikwa na Serikali ya Rwanda kwenda huko kujionea maendeleo yaliyofikiwa baada ya miaka 10 ya yale mauaji ya kimbari ya mwaka 1994.

Tukiwa huko, tulipata fursa ya kuzungumza na wananchi wa kawaida mijini na vijijnini. Tulizungumza pia na viongozi mbalimbali wakiwemo mawaziri, mameneja, wahandisi, wahadhiri nk. Na si mazungumzo tu; bali tulitembelea miji na vijiji kadhaa na kushuhudia, kwa macho yetu, jinsi nchi hiyo inavyosonga mbele kwa kasi kimaendeleo.

Nikiri kwamba, kwa nilichokiona Rwanda (mijini na vijijini), ilikuwa vigumu kwangu kuamini kwamba miaka 10 iliyopita nchi hiyo iligubikwa na vita na umwagaji damu mkubwa!

Ni vipi Rwanda katika kipindi cha miaka 13 tu iliyopita imeweza kunyanyuka toka majivuni na kujipatia maendeleo hayo ya kasi? Siri yao ya maendeleo ya haraka ni nini?

Nadhani hicho ndicho kitu ambacho Rais Kikwete na wenzake wanapaswa kwenda Rwanda kujifunza, na si kukimbilia tu Marekani; ingawa naambiwa kwamba maofisa wake hawazipapatikii safari kama hizo za Rwanda; kwa vile hazina malipo makubwa ya posho kama za Marekani!

Kwa ufupi, Rwanda ni somo kubwa kwetu. Miaka michache tu iliyopita iliharibiwa vibaya na vita na mauaji yale ya kimbari ya mwaka 1994, lakini sasa inachanja mbuga kimaendeleo kutuzidi sisi ambao miaka yote tumekuwa “kisiwa cha amani”.


Nilijifunza katika ziara hiyo kwamba kuna tofauti kubwa kati ya watawala wetu na viongozi wa Rwanda. Wa kwao ni wazalendo kweli kweli kushinda wa kwetu. Akili na mioyo yao vyote huzama kwenye kuijenga nchi yao ya Rwanda.

Katika Rwanda kiwango cha rushwa (ufisadi) ni kidogo mno. Kiongozi fisadi anachukuliwa kama ni msaliti wa umma na hivyo adui wa umma; wakati hapa kwetu kiongozi fisadi akirejea jimboni hupokewa kwa maandamano ya magari na pikipiki!

Baraza la mawaziri la Rwanda limejaa vijana wasomi na wachapakazi kweli kweli wanaoipenda nchi yao. Kagame aliwafuata vijana hao sehemu mbalimbali duniani na kuwashawishi waache, ama biashara zao au ajira nono walizokuwanazo, na kurejea nyumbani kuijenga upya nchi yao.

Uchapakazi wa baraza la mawaziri la Rwanda unaanzia kwa Rais Kagame mwenyewe. Huyu ni rais ambaye huchapa kazi hadi usiku. Nakumbuka tulipokuwa Kigali mwaka 2004 tulifanikiwa kukutana naye kwa mahojiano saa 6 usiku! Na bado baada ya sisi alikuwa na mkutano na wasaidizi wake wengine!


Tulipoonyesha kushangaa kukutana na Rais Kagame saa 6 usiku, wenyeji wetu walitushangaa kwa kulishangaa hilo. Wakatwambia kwamba Kagame aliwahi kuamka saa 9 usiku na kwenda uwanja wa ndege kuipokea timu ya soka ya taifa ambayo ilikuwa inarejea nyumbani na ushindi mkubwa!

Hapa kwetu Tanzania sijapata kusikia habari za waziri yeyote, au kiongozi yeyote mwenye kawaida ya kuchapa kazi hadi saa 6 usiku. Kama yupo nitajieni. Kiongozi wa mwisho tuliyekuwanaye, aliyekuwa na tabia hiyo, ni Edward Sokoine. Huyo alikuwa na kawaida ya kusoma mafaili usiku na kuwapigia simu (hata saa 8 usiku) mawaziri, ma-RC au hata ma-DC; kuwauliza hili na lile!

Kwa hiyo, kwa uchapaji kazi wa Kagame haishangazi kuona kuwa kwa muda mfupi tu amefanikiwa kuugeuza mji wa Kigali kuwa kitovu kikubwa cha biashara; achilia mbali kufufua kwa kasi ya ajabu kilimo cha biashara cha mazao ya kahawa na chai ambacho kilikuwa kimekufa kabisa wakati wa vita na mauaji yale ya kimbari.

Hata mkakati wake wa kupambana na umasikini vijijini ni wa matendo zaidi kuliko blah blah. Mpango kama ule wa kutoa ng’ombe wanne kwa kila mwanakijiji, umewanyanyua wengi nchini Rwanda.

Rwanda wana visheni wanayoifukuzia kimatendo na si ya kwenye makaratasi tu kama visioni 2025 yetu. Kwa mfano, wameshaanza kutekeleza kidogo kidogo Mpango Mkuu wa Ujenzi wa Kigali Mpya ambayo ni visheni ya miaka 50. Hapa kwetu sidhani kama tuna hata mpango mkuu (master plan) wa Dar es salaam itakavyokuwa miaka 20 ijayo; achilia mbali miaka 50!

Kilichoniuma moyo wakati wa ziara hiyo, hata hivyo, ni kwamba baadhi ya walioiwezesha Rwanda kupata maendeleo hayo ya haraka ni Watanzania. Kwa mfano, Chuo Kikuu cha Kigali cha Sayansi na Teknolojia (KIST) ambacho kimechangia sana kusukuma maendeleo katika vijiji vya Rwanda, nguvu yake kubwa ya mwanzo ilikuwa ni Watanzania.

Si tu kwamba mkuu wa chuo mwanzilishi, Profesa Silas Rwekabamba ni Mtanzania aliyechukuliwa na Kagame kutoka Chuo Kikuu cha Dar es salaam, lakini pia idara kadhaa za KIST zilikuwa zinaongozwa na Watanzania wakati nilipokitembelea mwaka 2004.

KIST ndiyo chachu ya maendeleo ya Rwanda; hususan vijijini. Kama utakwenda vijijini na kukuta wananchi wanatumia nishati ya jua, ni kwa sababu ya KIST, kama utakuta madaraja mapya yamejengwa vijijini, ni kwa sababu ya KIST; vivyo hivyo kwa zana za kilimo na viwanda vidogo vidogo.

Natujiulize: Kwa nini Watanzania hao (kina Rwekabamba) walipokuwa kitivo cha uhandisi cha Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (UDSM), hawakukifanya kitivo hicho kuwa chachu ya maendeleo ya vijiji vyetu kama walivyoifanya KIST kwa Rwanda?

Jibu lake ni rahisi; nalo ni kwamba mazingira ya Tanzania si mazingira ya Rwanda. Nchini Rwanda si tu walilipwa vyema, lakini vipaji vyao vilithaminiwa na kutumiwa vyema. Aidha, viongozi wa Rwanda wako nao bega kwa bega katika jukumu kubwa la kuhakikisha sayansi na teknolojia inasambaa hadi vijijini, tofauti na hapa nyumbani.


Ukiachilia mbali kina Profesa Rwekabamba, hata baadhi ya mawaziri wa Rwanda wamepata elimu yao ya msingi na sekondari hapa Tanzania. Nazungumzia watu kama Donald Kaberuka ambaye alikuwa Waziri wa Fedha wa Kagame kabla ya kuwa Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya Maendeleo ya Afrika (ADB).

Hata sasa ambapo ni bosi mkuu wa ADB, bado mapenzi, akili na mawazo ya Kaberuka yameelekezwa kwa nchi yake ya Rwanda; na hiyo inaeleza ni kwa nini Rwanda inafaidika sana na misaada ya benki hiyo.

Natujiulize: ni Watanzania wangapi wenye nyadhifa kubwa nje (kina Migiro na kina Profesa Tibaijuka) ambao wameikumbuka nchi yao na kuisaidia kuipa miradi mikubwa; kwa namna ambayo kina Kaberuka wanaisaidia Rwanda? Mimi siwajui, kama wapo naomba nitajiwe.

Nihitimishe hoja yangu kwa kusisitiza tena kwamba si mara zote ziara za watawala wetu nchini Marekani na Ulaya zina kitu kipya cha kujifunza kinachoweza kutuletea maendeleo endelevu. Sana sana nyingi zinakuwa tu za kutembeza bakuli la omba omba; yaani kutafuta msaada wa pesa wa kutatua matatizo yetu ya muda mfupi ya hapa na pale.

Nionavyo, badala ya kukimbilia tu Marekani na Ulaya, ni vyema watawala wetu waende kujifunza katika zile nchi ambazo miaka michache tu iliyopita tulikuwanazo dunia ya tatu, na sasa zinabisha hodi dunia ya kwanza!

Lakini pia kuna nchi jirani kama Rwanda ambazo katika muda mfupi tu zimejipatia maendeleo makubwa kutuzidi. Kwa nini Rais wetu Kikwete asiende huko kuijua siri yao?

Simaanishi ziara ya siku moja kwenda mkutanoni au kuzungumza tu na Kagame. Naamanisha ziara ya karibu wiki nzima ya kutembelea vijiji na miji mbalimbali ya nchi hiyo na kujionea mwenyewe kasi yao ya maendeleo, na kisha kurejea Kigali kumsihi Kagame na wenzake wammegee ‘siri’ ya mafanikio yao ya haraka!

Najua kuna watakaosema kwamba Kagame ni dikteta. Ni kweli, lakini ni ‘dikteta karimu’ (benevolent dictator). Hata Nyerere walimwita dikteta, lakini ni nani aliyewafanyia Watanzania mema mengi kati ya Nyerere na marais waliomfuatia?

Tafakari.
 
Kikwete aende Rwanda ajifunze kwa Kagame

Johnson Mbwambo Juni 10, 2009

Raia Mwema~Muungwana ni Vitendo

MJADALA kuhusu ziara nyingi za nje za Rais Kikwete; hususan za Marekani na Ulaya, umekataa kufa. Mjadala huu unasinzia tu kwa muda; lakini huibuka upya pindi anapofanya safari nyingine ya nje. Na ndivyo ilivyokuwa hivi karibuni alipokwenda tena Marekani (mara ya sita au saba?).

Wananchi wamekuwa wakizijadili safari hizo majumbani, maofisini, vijiweni, kwenye baa, na hata kwenye intaneti. Wako wanaoziunga mkono na wako wanaoziona kuwa ni matumizi mabaya ya pesa za walipakodi.

Katika moja ya hotuba zake Rais Kikwete alipata kujitetea kuhusu safari hizo kwa kutoa mfano wa Soko la Mitaji la Nasdaq alilolitembelea New york, Marekani.

Rais alisema hivi: “Nilipotembelea Soko la Hisa la New York, ambalo biashara yake inazidi dola 22.8 trilioni za Marekani, tulipewa heshima ya kuzindua biashara ya siku ile. Ni kwa sababu nilikuwepo ndiyo maana tulipewa heshima hiyo. Hivi unadhani Jonathan Njau (Mkuu wa Soko la Hisa la Dar es Salaam –DSE), angeweza kukutana na jamaa wale angekuwa peke yake?”

Kauli hiyo ya Rais wala haielezi Tanzania ilinufaika vipi kwa yeye kutembelea soko hilo la mitaji la Nasdaq; ukiachilia mbali kwamba alipewa heshima hiyo ya kufungua rasmi biashara ya siku hiyo.

Kwa hakika, mtu unashindwa kujizuia kujiuliza: Hivi Rais wetu alikatisha bahari ya Atlantic hadi Marekani kwa ajili ya kulitembelea soko la hisa la Nasdaq? Hivi alitaka kujifunza kitu gani hasa kutoka katika soko hilo la hisa linaloongoza duniani ambacho asingeweza kujifunza kutoka katika masoko yaliyoendelea ya mitaji ya baadhi ya nchi za Afrika.

Ni nani asiyejua kwamba tofauti kati ya soko letu changa la hisa la Dar es Salaam (DSE) na lile la Nasdaq la New York, ni tofauti kati ya Mlima na kichuguu?

Kama Rais na ujumbe wake walitaka kujifunza masuala ya masoko ya hisa ili labda waje waisaidie DSE, basi hawakuwa na sababu ya kuvuka bahari ya Atlantic kwa hilo! Kenya tu hapo kuna Soko la Mitaji la Nairobi ambalo ni bora mara 20 kuliko DSE yetu! Na kama hilo la Nairobi haliwavutii, basi kuna jingine la Johannesburg, Afrika Kusini ambalo nalo ni bora mara 30 kuliko la kwetu!

Ninachojaribu kueleza hapa (kwa mfano huo) ni kwamba wakati mwingine watawala wetu hawana sababu yoyote ya kukatisha bahari ya Atlantic kwenda kujifunza Marekani; kwani, kwa baadhi ya mambo, mafunzo yako hapa hapa Afrika; tena wakati mwingine katika nchi jirani tu!

Ndiyo maana siziungi mkono baadhi ya ziara anazozifanya rais wetu. Ningeziunga mkono safari hizo kama zingekuwa ni za kutafuta kweli kweli ‘mwarobaini’ wa kutukwamua ki-maendeleo, na si za kufungua biashara ya siku ya Nasdaq au za kutembeza kwingineko bakuli la ombaomba!

Ningeziunga mkono kama zingekuwa ni za kututafutia teknolojia ya kutengeneza boti na nyavu za uvuvi, na si za kutuombea samaki! Ningeziunga mkono kama zingekuwa za kuwaombea Watanzania wafundishwe namna ya kutengeneza vyandarua (kama hawajui), na si za kuomba msaada wa vyandarua!

Kwa maneno mengine; ningeziunga mkono kama zingelenga kutuletea maendeleo endelevu, na si za kuomba kusaidiwa kutatuliwa shida za muda mfupi za hapa na pale.

Kwa mantiki hiyo hiyo, ningekuwa naziunga mkono kama zingekuwa ni za kwenda katika nchi kama za India, Brazil, Singapore, Malaysia, Korea Kusini, na hata nchi chache za Afrika, kudadisi na kujua ni kwa nini wenzetu walifanikiwa kupata maendeleo katika kipindi kifupi wakati sisi tumekwama.

Miaka si mingi sana iliyopita, nchi hizo zilikuwa hazitofautiani sana nasi ki-maendeleo; lakini zilipozinduka, zilipiga kasi ya maendeleo haraka na kutuacha mno nyuma. Zilikuwa dunia ya tatu kama sisi, lakini sasa zinabisha hodi dunia ya kwanza; huku zikituacha sisi pale pale!

Nchi kama Malaysia na Korea Kusini tulikuwa kiwango kimoja cha maendeleo mwaka 1961, lakini sasa ni tajiri kutuzidi mara 20 (msome Robert Guest katika kitabu chake The Shackled Continent).

Lakini hata Afrika, kuna baadhi ya nchi ambazo tunaweza kabisa kujifunza kitu. Moja ya hizo ni Rwanda. Miaka 13 iliyopita Rwanda ilianza upya (majivuni) baada ya kuharibiwa vibaya na vita na mauaji yale ya kimbari ya mwaka 1994 yaliyosababisha vifo vya Watusi na Wahutu wenye msimamo wa kati, zaidi ya 800,000.

Lakini leo hii, Rwanda iko mbali mno kimaendeleo (hasa vijijini) kutuzidi. Alichoweza Rais Kagame kukifanya Rwanda katika miaka 13, ni kile ambacho sisi, kama Taifa, tumeshindwa kukifanya kwa miaka 20 iliyopita. Na wala hatujasikia Rais Kagame akienda, mara kwa mara, Marekani au Ulaya!

Mwaka 2004 nilikuwa mmoja wa wahariri wachache wa Tanzania tulioalikwa na Serikali ya Rwanda kwenda huko kujionea maendeleo yaliyofikiwa baada ya miaka 10 ya yale mauaji ya kimbari ya mwaka 1994.

Tukiwa huko, tulipata fursa ya kuzungumza na wananchi wa kawaida mijini na vijijnini. Tulizungumza pia na viongozi mbalimbali wakiwemo mawaziri, mameneja, wahandisi, wahadhiri nk. Na si mazungumzo tu; bali tulitembelea miji na vijiji kadhaa na kushuhudia, kwa macho yetu, jinsi nchi hiyo inavyosonga mbele kwa kasi kimaendeleo.

Nikiri kwamba, kwa nilichokiona Rwanda (mijini na vijijini), ilikuwa vigumu kwangu kuamini kwamba miaka 10 iliyopita nchi hiyo iligubikwa na vita na umwagaji damu mkubwa!

Ni vipi Rwanda katika kipindi cha miaka 13 tu iliyopita imeweza kunyanyuka toka majivuni na kujipatia maendeleo hayo ya kasi? Siri yao ya maendeleo ya haraka ni nini?

Nadhani hicho ndicho kitu ambacho Rais Kikwete na wenzake wanapaswa kwenda Rwanda kujifunza, na si kukimbilia tu Marekani; ingawa naambiwa kwamba maofisa wake hawazipapatikii safari kama hizo za Rwanda; kwa vile hazina malipo makubwa ya posho kama za Marekani!

Kwa ufupi, Rwanda ni somo kubwa kwetu. Miaka michache tu iliyopita iliharibiwa vibaya na vita na mauaji yale ya kimbari ya mwaka 1994, lakini sasa inachanja mbuga kimaendeleo kutuzidi sisi ambao miaka yote tumekuwa “kisiwa cha amani”.

Nilijifunza katika ziara hiyo kwamba kuna tofauti kubwa kati ya watawala wetu na viongozi wa Rwanda. Wa kwao ni wazalendo kweli kweli kushinda wa kwetu. Akili na mioyo yao vyote huzama kwenye kuijenga nchi yao ya Rwanda.

Katika Rwanda kiwango cha rushwa (ufisadi) ni kidogo mno. Kiongozi fisadi anachukuliwa kama ni msaliti wa umma na hivyo adui wa umma; wakati hapa kwetu kiongozi fisadi akirejea jimboni hupokewa kwa maandamano ya magari na pikipiki!

Baraza la mawaziri la Rwanda limejaa vijana wasomi na wachapakazi kweli kweli wanaoipenda nchi yao. Kagame aliwafuata vijana hao sehemu mbalimbali duniani na kuwashawishi waache, ama biashara zao au ajira nono walizokuwanazo, na kurejea nyumbani kuijenga upya nchi yao.

Uchapakazi wa baraza la mawaziri la Rwanda unaanzia kwa Rais Kagame mwenyewe. Huyu ni rais ambaye huchapa kazi hadi usiku. Nakumbuka tulipokuwa Kigali mwaka 2004 tulifanikiwa kukutana naye kwa mahojiano saa 6 usiku! Na bado baada ya sisi alikuwa na mkutano na wasaidizi wake wengine!

Tulipoonyesha kushangaa kukutana na Rais Kagame saa 6 usiku, wenyeji wetu walitushangaa kwa kulishangaa hilo. Wakatwambia kwamba Kagame aliwahi kuamka saa 9 usiku na kwenda uwanja wa ndege kuipokea timu ya soka ya taifa ambayo ilikuwa inarejea nyumbani na ushindi mkubwa!

Hapa kwetu Tanzania sijapata kusikia habari za waziri yeyote, au kiongozi yeyote mwenye kawaida ya kuchapa kazi hadi saa 6 usiku. Kama yupo nitajieni. Kiongozi wa mwisho tuliyekuwanaye, aliyekuwa na tabia hiyo, ni Edward Sokoine. Huyo alikuwa na kawaida ya kusoma mafaili usiku na kuwapigia simu (hata saa 8 usiku) mawaziri, ma-RC au hata ma-DC; kuwauliza hili na lile!

Kwa hiyo, kwa uchapaji kazi wa Kagame haishangazi kuona kuwa kwa muda mfupi tu amefanikiwa kuugeuza mji wa Kigali kuwa kitovu kikubwa cha biashara; achilia mbali kufufua kwa kasi ya ajabu kilimo cha biashara cha mazao ya kahawa na chai ambacho kilikuwa kimekufa kabisa wakati wa vita na mauaji yale ya kimbari.

Hata mkakati wake wa kupambana na umasikini vijijini ni wa matendo zaidi kuliko blah blah. Mpango kama ule wa kutoa ng’ombe wanne kwa kila mwanakijiji, umewanyanyua wengi nchini Rwanda.

Rwanda wana visheni wanayoifukuzia kimatendo na si ya kwenye makaratasi tu kama visioni 2025 yetu. Kwa mfano, wameshaanza kutekeleza kidogo kidogo Mpango Mkuu wa Ujenzi wa Kigali Mpya ambayo ni visheni ya miaka 50. Hapa kwetu sidhani kama tuna hata mpango mkuu (master plan) wa Dar es salaam itakavyokuwa miaka 20 ijayo; achilia mbali miaka 50!

Kilichoniuma moyo wakati wa ziara hiyo, hata hivyo, ni kwamba baadhi ya walioiwezesha Rwanda kupata maendeleo hayo ya haraka ni Watanzania. Kwa mfano, Chuo Kikuu cha Kigali cha Sayansi na Teknolojia (KIST) ambacho kimechangia sana kusukuma maendeleo katika vijiji vya Rwanda, nguvu yake kubwa ya mwanzo ilikuwa ni Watanzania.

Si tu kwamba mkuu wa chuo mwanzilishi, Profesa Silas Rwekabamba ni Mtanzania aliyechukuliwa na Kagame kutoka Chuo Kikuu cha Dar es salaam, lakini pia idara kadhaa za KIST zilikuwa zinaongozwa na Watanzania wakati nilipokitembelea mwaka 2004.

KIST ndiyo chachu ya maendeleo ya Rwanda; hususan vijijini. Kama utakwenda vijijini na kukuta wananchi wanatumia nishati ya jua, ni kwa sababu ya KIST, kama utakuta madaraja mapya yamejengwa vijijini, ni kwa sababu ya KIST; vivyo hivyo kwa zana za kilimo na viwanda vidogo vidogo.

Natujiulize: Kwa nini Watanzania hao (kina Rwekabamba) walipokuwa kitivo cha uhandisi cha Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (UDSM), hawakukifanya kitivo hicho kuwa chachu ya maendeleo ya vijiji vyetu kama walivyoifanya KIST kwa Rwanda?

Jibu lake ni rahisi; nalo ni kwamba mazingira ya Tanzania si mazingira ya Rwanda. Nchini Rwanda si tu walilipwa vyema, lakini vipaji vyao vilithaminiwa na kutumiwa vyema. Aidha, viongozi wa Rwanda wako nao bega kwa bega katika jukumu kubwa la kuhakikisha sayansi na teknolojia inasambaa hadi vijijini, tofauti na hapa nyumbani.

Ukiachilia mbali kina Profesa Rwekabamba, hata baadhi ya mawaziri wa Rwanda wamepata elimu yao ya msingi na sekondari hapa Tanzania. Nazungumzia watu kama Donald Kaberuka ambaye alikuwa Waziri wa Fedha wa Kagame kabla ya kuwa Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya Maendeleo ya Afrika (ADB).

Hata sasa ambapo ni bosi mkuu wa ADB, bado mapenzi, akili na mawazo ya Kaberuka yameelekezwa kwa nchi yake ya Rwanda; na hiyo inaeleza ni kwa nini Rwanda inafaidika sana na misaada ya benki hiyo.

Natujiulize: ni Watanzania wangapi wenye nyadhifa kubwa nje (kina Migiro na kina Profesa Tibaijuka) ambao wameikumbuka nchi yao na kuisaidia kuipa miradi mikubwa; kwa namna ambayo kina Kaberuka wanaisaidia Rwanda? Mimi siwajui, kama wapo naomba nitajiwe.

Nihitimishe hoja yangu kwa kusisitiza tena kwamba si mara zote ziara za watawala wetu nchini Marekani na Ulaya zina kitu kipya cha kujifunza kinachoweza kutuletea maendeleo endelevu. Sana sana nyingi zinakuwa tu za kutembeza bakuli la omba omba; yaani kutafuta msaada wa pesa wa kutatua matatizo yetu ya muda mfupi ya hapa na pale.

Nionavyo, badala ya kukimbilia tu Marekani na Ulaya, ni vyema watawala wetu waende kujifunza katika zile nchi ambazo miaka michache tu iliyopita tulikuwanazo dunia ya tatu, na sasa zinabisha hodi dunia ya kwanza!

Lakini pia kuna nchi jirani kama Rwanda ambazo katika muda mfupi tu zimejipatia maendeleo makubwa kutuzidi. Kwa nini Rais wetu Kikwete asiende huko kuijua siri yao?

Simaanishi ziara ya siku moja kwenda mkutanoni au kuzungumza tu na Kagame. Naamanisha ziara ya karibu wiki nzima ya kutembelea vijiji na miji mbalimbali ya nchi hiyo na kujionea mwenyewe kasi yao ya maendeleo, na kisha kurejea Kigali kumsihi Kagame na wenzake wammegee ‘siri’ ya mafanikio yao ya haraka!

Najua kuna watakaosema kwamba Kagame ni dikteta. Ni kweli, lakini ni ‘dikteta karimu’ (benevolent dictator). Hata Nyerere walimwita dikteta, lakini ni nani aliyewafanyia Watanzania mema mengi kati ya Nyerere na marais waliomfuatia?

Tafakari.


Tusikate tamaa, tuendelee kupambana na ufisadi na wakati huo huo tuongeze nguvu katika uzalishaji. Serikali pia nadhani wapunguze matumizi ikiwa ni pamoja na kupunguza baraza la mawaziri, nikubwa mno na halina ufanisi.

Kuhusu rwanda hata hivyo naona kama bado hawana speed ya kutosha kwa sababu nadhani geographical area ya rwanda ni sawa na mikoa miwili ya TZ.

Kitu cha msingi kwa TZ ni kwamba sasa hivi tumisha elewa chanzo cha umasikini wetu kwamba ni:
1. mikataba ya kifisadi
2. utapeli wa akina Rosti-tamu na akina chenge na wenzao
3. kupeana uwaziri na kadhalika kwa ushemeji na mjomba
4. kuto kuwajibika ipasavyo ktk maeneo yetu ya kazi
5. kuto elewa ni nini priorities za maendeleo ya taifa
6. n.k.

Tukiyashughulikia haya basi TZ inaweza kuinuka ghafla.
 
Rwanda ni nchi ndogo sana kwa vyovyote vile haiwezi kutuacha, hata kama tunajichukia kwa kiasi gani binafsi nimepita huko miezi miwili iliyopita. Ni kweli wanapiga hatua lakini Tanzania ni nchi kubwa na inayokuwa kwa kasi kuliko Rwanda. Kujengeka kwa kasi kwa Dar ni kiashilio kwamba bongo inasongambele tukiacha politike.

Pia Rwanda sio salama sana kama Tanzania, na siasa yao ni tofauti na Tanzania. Kama ukifata utawala ule wa kiimla hapa bongo patakuwa hapakaliki manake hakuna compromise Kigali.
 
May be Kagame basi tumpigie debe awe raisi wa kwanza EAF!

Sasa kwa nini Tz tunasuasua..na hatusongi mbele kwa kazi??

As a society are we not ambitious enough?? Do we lack leadership??
 
1 Reactions
Reply
Back
Top Bottom