Kwa speed hii ya ukopaji likitokea janga lingine mfano wa corona hali itakuwaje?

The Phylosopher

JF-Expert Member
Mar 11, 2015
1,495
2,041
Nimekaa tu na kujiuliza kama raia wa kawaida kwamba serikali yetu inakopa na inaendelea kukopa, na inaonekana kila inapotokea uhitaji au upungufu wa aina yoyote, ufumbuzi unaowajia viongozi wetu vichwani ni kutafuta mahali pa kwenda kukopa.

Huenda wako sahihi kwa sababu wao Wana wataalam na wana washauri wa mambo ya kiuchumi ila wasiwasi wangu kama raia wa kawaida ni kwamba dunia imekuwa ikikumbwa na dharula mbalimbali zinazopelekea kubadilika kwa matarajio ya mapato.

Kwa mfano rahisi ni hili janga la corona ukame mafuriko vita na majanga mengine ya asili. Je ikitokea majanga ya namna hii halafu tumejaa madeni Hali itakuwaje? Je serikali yetu ina mpango wowote wa kujinusuru!?
 
Nimekaa tu na kujiuliza kama raia wa kawaida kwamba serikali yetu inakopa na inaendelea kukopa, na inaonekana kila inapotokea uhitaji au upungufu wa aina yoyote, ufumbuzi unaowajia viongozi wetu vichwani ni kutafuta mahali pa kwenda kukopa...
Tunaelekea kwenye Great Economic Depression nyingine.

Hali itakuwa mbaya sana. Ni suala la muda tu.
 
Nimekaa tu na kujiuliza kama raia wa kawaida kwamba serikali yetu inakopa na inaendelea kukopa, na inaonekana kila inapotokea uhitaji au upungufu wa aina yoyote, ufumbuzi unaowajia viongozi wetu vichwani ni kutafuta mahali pa kwenda kukopa...
Tuna uono kimo cha mbilikimo na hatuna plan B.. Ni kudra za Mwenyezi Mungu tu ndio zinatubeba
 
Mkuu, bila shaka unakumbuka jinsi Spika wa Bunge alivyoshinikizwa ajiuzulu baada ya kuhoji masuala ya mikopo, na wewe unataka kujiuzulu katika majukumu na nyadhifa uliyonayo kwa sasa ?
Ningependa waje wajibu hoja badala ya kunishinikiza kujiuzulu. Ndugai aliuliza swali ambalo alipaswa kuliuliza tena na tena!?
 
Nilale tuu maana sijui itkuwaje keaho na sina mpango wowote wa kujua


Nje ya mada
Mshana jr nina shida na wewe mkuu
 
Hivi kwani corona ipo jamani? Mimi nashangaa hata rais wetu na jopo lake wakisafiri nje ya nchi wanavaa barakoa wenyejiwao hawavai!! Kuna viongozi wetu wamekuja juzi toka Spain tulikuwa nao kikundi cha watu 200 hakuna aliyevaa barakoa sasa hii corona ya viongozi wetu hata sielewi pia nina wasi wasi dawa za chanjo zimesha eksipaya hakuna anayejipeleka kuchanja llabda wale anaotoka nje ya nchi
 
Nimekaa tu na kujiuliza kama raia wa kawaida kwamba serikali yetu inakopa na inaendelea kukopa, na inaonekana kila inapotokea uhitaji au upungufu wa aina yoyote, ufumbuzi unaowajia viongozi wetu vichwani ni kutafuta mahali pa kwenda kukopa.

Huenda wako sahihi kwa sababu wao Wana wataalam na wana washauri wa mambo ya kiuchumi ila wasiwasi wangu kama raia wa kawaida ni kwamba dunia imekuwa ikikumbwa na dharula mbalimbali zinazopelekea kubadilika kwa matarajio ya mapato.

Kwa mfano rahisi ni hili janga la corona ukame mafuriko vita na majanga mengine ya asili. Je ikitokea majanga ya namna hii halafu tumejaa madeni Hali itakuwaje? Je serikali yetu ina mpango wowote wa kujinusuru!?
Kuna mtikisiko mkubwa wa kiuchumi unatunyemelea, ni issue ya muda tu...
 
Back
Top Bottom