Kwa speed hii ya Rais Magufuli ni bora kingerudishwa cheo cha RDD maana Wakuu wa mikoa wanachemka!

johnthebaptist

JF-Expert Member
May 27, 2014
83,914
141,866
Awali pale mkoani palikuwa na mtu anaitwa RDD akisimamia shughuli zote za maendeleo. Cheo hiki kilifutwa baadaye lakini kule wilayani akina DED wakaachwa.

Nimefuatilia agizo la Waziri mkuu Majaliwa kwamba wakuu wa mikoa wakasimamie shughuli za biashara ya madini kule mikoani. Kisha nikamsikia Waziri Jaffo akisema RCs wote wanaitwa na Rais Magufuli jijini Dsm ili kupewa maelekezo ya utoaji wa vitambulisho vya ujasiriamali kwani wengi wao wamevurunda.

Ndiposa nimejiuliza hawa walioshindwa kugawa vitambulisho watawezaje kusimamia biashara nyeti na yenye changamoto ya madini. Ghafla nikaikumbuka nafasi ile ya RDD enzi za Mwalimu Nyerere.

Si vibaya Rais Magufuli akawarejesha Wakurugenzi wa Maendeleo wa Mikoa na huko awajaze wataalamu siye makada tutabaki kwenye uRC na uDC.

Mungu wa mbinguni ambariki Rais Magufuli
Maendeleo hayana vyama!
 
Awali pale mkoani palikuwa na mtu anaitwa RDD akisimamia shughuli zote za maendeleo. Cheo hiki kilifutwa baadaye lakini kule wilayani akina DED wakaachwa.

Nimefuatilia agizo la Waziri mkuu Majaliwa kwamba wakuu wa mikoa wakasimamie shughuli za biashara ya madini kule mikoani. Kisha nikamsikia Waziri Jaffo akisema RCs wote wanaitwa na Rais Magufuli jijini Dsm ili kupewa maelekezo ya utoaji wa vitambulisho vya ujasiriamali kwani wengi wao wamevurunda.

Ndiposa nimejiuliza hawa walioshindwa kugawa vitambulisho watawezaje kusimamia biashara nyeti na yenye changamoto ya madini. Ghafla nikaikumbuka nafasi ile ya RDD enzi za Mwalimu Nyerere.

Si vibaya Rais Magufuli akawarejesha Wakurugenzi wa Maendeleo wa Mikoa na huko awajaze wataalamu siye makada tutabaki kwenye uRC na uDC.

Mungu wa mbinguni ambariki Rais Magufuli
Maendeleo hayana vyama!

Ujue kazi za RDD zilihamishiwa kwa RAS ambaye kimsingi inapaswa kuwa ni MTAALAMU mwenye uzoefu serikalini si chini ya miaka 7 nadhani. Vitu vingi vinakwama kwa sababu RAS na DED walioteuliwa wengi sio wataalamu kama tulivyotegemea.
Ishu kama ya kugawa vitambulisho sio kazi ya maRC. Ile kazi wangepewa maRAS na maDED wangefanya kiuweledi zaidi. Ile ni technical work sio Political work
 
Ujue kazi za RDD zilihamishiwa kwa RAS ambaye kimsingi inapaswa kuwa ni MTAALAMU mwenye uzoefu serikalini si chini ya miaka 7 nadhani. Vitu vingi vinakwama kwa sababu RAS na DED walioteuliwa wengi sio wataalamu kama tulivyotegemea.
Hapana RDD ( Regional Development Director) alishughulikia maendeleo mkoani hawa akina RAS na DAS wao ni ma adminstrator wanashughulika na utawala!
 
Hapana RDD ( Regional Development Director) alishughulikia maendeleo mkoani hawa akina RAS na DAS wao ni ma adminstrator wanashughulika na utawala!
Nakumbuka kuleta cheo cha RDD na DDD enzi za Mwl.Nyerere iliitwa kupeleka madaraka ya maendeleo katika mikoa na wilaya yawe karibu na wananchi wao.
Lakini kadiri miaka ilivyosonga hiyo kazi ikaingiliwa na watoto wa mjini wakaongeza idadi kubwa ya wilaya na mikoa ili watengeneze vyeo.Hata idadi ya majimbo ya wabunge yaliongezwa na pia viti maalumu yote hayo ni kuongeza matumizi na si maendeleo kama alivyokuwa amekusudia raisi Nyerere.
 
Back
Top Bottom