Makinikia Original
Member
- Aug 29, 2017
- 90
- 154
Nimebaki mtazamaji wa suala hili kwa muda mrefu nikijaribu kupata mdhahania wa hoja za pande zote mbili, Lissu upande mmoja na serikali upande mwingine.
Tutakubaliana kwamba Lissu ni kati ya watanzania wachache waliobaki wenye uwezo wa kujenga hoja na kueleweka. Lissu ana kipaji cha kutumia ubongo wake kuchekecha na kufikia hitimisho juu ya hoja aina aina na mara zote hufanikiwa kuzitetea, awe sahihi au amekosea.
Kaliba ya aina hii imepatwa kumilikiwa na watanzania wachache tu, mmoja ambaye atakumbukwa kwa wepesi ni baba wa taifa ingawa kiukweli Lissu bado anasafari ndefu kufikia kiwango hiki.
Ziara anayoendelea nayo huko ughaibuni kuelezea mkasa mbaya uliompata Septemba 7 mwaka juzi imeibua watu wengi upande wa serikali wanaojitosa kujibu kufukia ombwe linalokuwa limeachwa na mjibuji aliyetangulia.
Kwa uchache watu hawa ni Sirro, Kangi Lugola, Dr. Bashiru Ally, Humphrey Polepole, Balozi Abdallah Possi, Balozi Wilson Masilingi, Kibajaji, Msukuma, Makonda na hivi karibuni DC wa Kigamboni Lucy Msafiri.
Majibu ya timu hii yamekuwa yanaacha maswali mengi kuliko majibu ndani yake. Katika namna yoyote ile hakuna hata mmoja aliyeweza kujibu aghalabu moja ya kumi ya hoja za Lissu lakini wamebaki kuivua nguo serikali kwa majibu yao yasiyo ya kidiplomadia wala kisheria.
Kuna baadhi ya sehemu ukivulia nguo inabidi uchutame hasa kama sehemu hii ni mbeke ya hadhara, kwa hili serikali ya awamu ya tano imechemka, ikubali kushindwa.
Cha kufanya ni kukaa kimya au kuagiza upelelezi makini utakaoisafisha serikali mbele ya wananchi wake na hata jumuia ya kimataifa.
Serikali inayonuka damu haipaswi kuwepo karne hii ya ishirini na moja.
Tutakubaliana kwamba Lissu ni kati ya watanzania wachache waliobaki wenye uwezo wa kujenga hoja na kueleweka. Lissu ana kipaji cha kutumia ubongo wake kuchekecha na kufikia hitimisho juu ya hoja aina aina na mara zote hufanikiwa kuzitetea, awe sahihi au amekosea.
Kaliba ya aina hii imepatwa kumilikiwa na watanzania wachache tu, mmoja ambaye atakumbukwa kwa wepesi ni baba wa taifa ingawa kiukweli Lissu bado anasafari ndefu kufikia kiwango hiki.
Ziara anayoendelea nayo huko ughaibuni kuelezea mkasa mbaya uliompata Septemba 7 mwaka juzi imeibua watu wengi upande wa serikali wanaojitosa kujibu kufukia ombwe linalokuwa limeachwa na mjibuji aliyetangulia.
Kwa uchache watu hawa ni Sirro, Kangi Lugola, Dr. Bashiru Ally, Humphrey Polepole, Balozi Abdallah Possi, Balozi Wilson Masilingi, Kibajaji, Msukuma, Makonda na hivi karibuni DC wa Kigamboni Lucy Msafiri.
Majibu ya timu hii yamekuwa yanaacha maswali mengi kuliko majibu ndani yake. Katika namna yoyote ile hakuna hata mmoja aliyeweza kujibu aghalabu moja ya kumi ya hoja za Lissu lakini wamebaki kuivua nguo serikali kwa majibu yao yasiyo ya kidiplomadia wala kisheria.
Kuna baadhi ya sehemu ukivulia nguo inabidi uchutame hasa kama sehemu hii ni mbeke ya hadhara, kwa hili serikali ya awamu ya tano imechemka, ikubali kushindwa.
Cha kufanya ni kukaa kimya au kuagiza upelelezi makini utakaoisafisha serikali mbele ya wananchi wake na hata jumuia ya kimataifa.
Serikali inayonuka damu haipaswi kuwepo karne hii ya ishirini na moja.