Guselya Ngwandu
Member
- Sep 17, 2021
- 39
- 84
Jamhuri ya Muungano wa Tanzania...
Kwanza pongezi sana kwa kila anayetamani Katiba Mpya kwa sababu nia ya Rais Samia Suluhu kutekeleza nia yake inaonekana wazi. Kwenye Bunge lijalo la Bajeti, Wizara ya Katiba na Sheria inaenda kuomba pesa kwa ajili ya mchakato wa Katiba Mpya. Ni wazi 'Mama' anakwenda kufufua mchakato huo kabla ya 2025.
Hata hivyo kwa sasa, tunamhitaji zaidi MAMA kuliko Katiba Mpya yenyewe. Naomba nieleweke.
Tunachohitaji kwa sasa ni utashi wa kisiasa na utayari kiongozi. Katiba Mpya haijitengenezi, ndio maana kabla ya Rais Samia hata kutaja Katiba mpya ilikuwa inatisha, ila yeye karuhusu. Tunamuhitaji yeye kwa sasa kuliko hata hiyo katiba Mpya, bila yeye hakuna Katiba Mpya.
Pia tunamhitaji Rais Samia kwa sababu yeye anatoa suluhu kwa matatizo ya msingi ya nchi. Anaboresha elimu, maji, afya na mengi ya msingi. Katika miaka yake miwili tumeona mambo yote haya yakifanikiwa.
Unaweza kuwa na Katiba mpya ila kama Rais sio mtu wa kuendana na upya huo itakuwa kazi bure. Kenya wana katiba mpya ila hawaachi kulia kila siku.
Tumuunge mkono Mama, tumuunge mkono kama wanavyofanya CHADEMA, ACT na wengine.
#MamaAnafanikisha
Kwanza pongezi sana kwa kila anayetamani Katiba Mpya kwa sababu nia ya Rais Samia Suluhu kutekeleza nia yake inaonekana wazi. Kwenye Bunge lijalo la Bajeti, Wizara ya Katiba na Sheria inaenda kuomba pesa kwa ajili ya mchakato wa Katiba Mpya. Ni wazi 'Mama' anakwenda kufufua mchakato huo kabla ya 2025.
Hata hivyo kwa sasa, tunamhitaji zaidi MAMA kuliko Katiba Mpya yenyewe. Naomba nieleweke.
Tunachohitaji kwa sasa ni utashi wa kisiasa na utayari kiongozi. Katiba Mpya haijitengenezi, ndio maana kabla ya Rais Samia hata kutaja Katiba mpya ilikuwa inatisha, ila yeye karuhusu. Tunamuhitaji yeye kwa sasa kuliko hata hiyo katiba Mpya, bila yeye hakuna Katiba Mpya.
Pia tunamhitaji Rais Samia kwa sababu yeye anatoa suluhu kwa matatizo ya msingi ya nchi. Anaboresha elimu, maji, afya na mengi ya msingi. Katika miaka yake miwili tumeona mambo yote haya yakifanikiwa.
Unaweza kuwa na Katiba mpya ila kama Rais sio mtu wa kuendana na upya huo itakuwa kazi bure. Kenya wana katiba mpya ila hawaachi kulia kila siku.
Tumuunge mkono Mama, tumuunge mkono kama wanavyofanya CHADEMA, ACT na wengine.
#MamaAnafanikisha