Kwa sasa Kenya ni nchi ya Kimaskini zaidi kuliko Tanzania, serikali ya Kenya yashindwa kulipa hata mishahara!

Zanzibar-ASP

JF-Expert Member
Nov 28, 2013
10,115
35,121
Mficha maradhi kifo kitamuumbua, yawahi hayawi sasa yamekuwa, ukweli halisi umeanza kujionyesha huko Kenya, hali ya maisha ni mbaya mnoo, vijijini ukame unawaua, mijijini maisha yanawanyonga na sasa Serikali imeshindwa kulipa hadi mishahara watumishi wake. Kenya kumechoka na kuchakaa balaa.

Rais wa Kenya (William Ruto) amekiri wazi wazi kuwa hali ya kiuchumi kwa wakenya na serikali yao ni tete mnoo, huku akisema serikali yake imezidiwa na madeni yaliyotokana na kukopa kiholela ili kugharamia miradi iliyojaa ufisadi mkubwa kiasi cha kushindwa kuwa na pesa za kulipa mishahara.

Sio hayo tu, zipo sehemu kadhaa (kaunti nyingi) katika Kenya ambapo mbali na kutokuweza kupokea pesa za kulipa mishahara kwa miezi kadhaa pia zimeshindwa kupokea pesa kwa ajili ya kugharamia utoaji wa huduma za Afya na elimu kutoka serikalini. Kwa lugha rahisi na fupi sana, Kenya kwa sasa ni taifa rasmi la kimaskini zaidi katika ukanda wa Afrika mashariki na kati.

Kwa hali ilivyo sasa ni dhihaka kubwa sana kutaka kuilinganisha Kenya na Tanzania, kwa kuwa Tanzania mbali na kuwa kihistoria ni nchi yenye mizizi ya kimaskini (ujamaa!) na tangu kumfukuza mkoloni imekuwa chini ya CCM (chama kinachoukumbatia umaskini) bado haijaweza kupitia vipindi vya umaskini na kufirisika kwa serikali kiasi cha kushindwa kulipa mishahara ya watumishi wake. Kwa sasa kimaskini Kenya imepitiliza.

Kama hali hii ikiendelea kwa muda mrefu kidogo kuna kila dalili kuwa huenda Kenya ikaweka rehani bandari ya Mombasa, viwanja vya ndege na mtandao wa reli ya SGR ili kulipa madeni au kuendelea kukopesheka.
 
Kasema anasimamia msimamo wake kuwa hatokopa kugharamia expenditures za serikali ikiwemo kulipa mishahara. Nafikiri ni ahadi zake wakati wa uchunguzi ila sidhani kama atamudu kuendelea na huo msimamo wake.
Kumbe siku zote tambo za wakenya kuhusu utajiri na ufahari zilikuwa ni michongo ya pesa za mikopo, sasa mikopo imeiva, madeni hayalipiki na njaa imewakamata balaa.
 
Jipeni moyo huku Madelu akikomba kibuyu cha taifa
Madelu hana tatizo, yupo pale kimkakati, waliomuweka ndio wana shida.

Tatizo kubwa ni yule kichaa aliyezikwa Chato, alituharibia mnoo taifa letu kwa kuharibu mifumo ya siasa, serikali na usimamizi katika taifa letu, kinachoendelea leo ni matunda maovu ya kazi zake.
 
Hivi unafuatilia revenue collection ya Kenya kwa mwezi au unatuletea hadithi hapa

Wale wanamapato karibia au niseme mara mbili ya Tanzania, japo wanamakosa kwenye usimamizi tu wa mapato ulio tokea hapo nyuma hasa kwenye kubadilishana madaraka/uchaguzi.

Unajua wana maviwanda mengi ya wazungu yanalipa kodi kubwa na yanauza bidhaa nje hivyo hupata fedha nyingi za kigeni na sio kutegemea utalii tu; Ni suala la muda; wala usijilinganishe nao.

Wanakusanya hela nyingi sana tena bila presha ya kukimbizana na walala hoi kwa kuwa wanategema zaidi kodi kubwa itoke kwenye maviwanda, mauzo ya nje na mashamba makubwa ya wazungu.
 
Back
Top Bottom