Kwanini mahusiano/ndoa nyingi hazidumu?

Galacha Maestro

JF-Expert Member
Sep 29, 2011
1,353
2,216
KWANINI MAHUSIANO / NDOA NYINGI HAZIDUMU?
Unapoingia katika ndoa au mahusiano huwezi kufikiria hata kidogo kwamba asilimia kubwa ya ndoa au mahusiano hayo kufeli.Ndoa au mahusiano yanaweza kufeli kwa sababu nyingi na iwapo ndoa yako ilianguka na kufeli sababu kubwa yaweza kuwa na tofauti nyingine nyingi. Lakini, kuna sababu kadhaa za jumla na za kudumu kwenye ndoa zote zilizofeli.Hebu tazama orodha yangu ya sababu 8 za ndoa nyingi kuanguka na kufeli.

1) Kwa sababu ulitaka harusi badala ya ndoa:
Ni miongoni mwa ada za kijamii kushiriki katika furaha mbalimbali za wenzetu. Miongoni mwa furaha hizo ni shughuli za harusi pindi wahusika wanapoamua kuingia katika taasisi tukufu ya NDOA. Shamshamra zinazoandamana na tukio hilo adhimu hutuhamasisha kuingia katika taasisi hiyo muhimu kabisa katika maisha ya mwanadamu. Mavazi, mapambo ya maharusi na kushangiliwa na wenzetu huwafanya wanandoa wahisi kama nyota. Matukio hayo hukufanya uanze kutamani na hata kupanga namna harusi yako itakavyokuwa. Tazama: hapo umesukumwa na mvuto wa harusi badala ya uhalisia wa NDOA.Ni bahati mbaya kuwa maandalizi ya harusi yanakuwa makubwa kuliko hata maandalizi ya NDOA yenyewe.Nawashauri wazazi kuwashauri watoto wao kwamba: baada ya harusi kuna ndoa. Hivyo nguvu kubwa wazielekeze kwenye suala la pili.

2) Kwa sababu umeoana na mtu usiyeendana naye:
Wakati fulani jambo hili hutokana moja kwa moja na suala la kwanza nililolieleza hapo juu, lakini kuna sababu nyingine ambazo zinaweza kusababisha kufunga ndoa na mtu ambaye hamuendani kabisa. Yumkini ni mtu uliyemzoea; yumkini ni mtu uliyecheza naye tokea utotoni lakini licha ya kutokuwa mtu sahihi unajisemea moyoni na kujipa matumaini “siwezi kuuvunja moyo wake mambo yatabadilika tu”. Yumkini unaona kabisa amekuwa tofauti na ulivyotarajia, lakini umeshaweka ahadi naye. Kabla ya kuingia katika ndoa jitahidi umjue vilivyo mwenza wako wa maisha…. Usiangalie tu kwamba atapendeza ukisimama naye siku ya harusi.

3) Kwa sababu mtu mmoja hawezi kukidhi mahitaji yako yote:
Jambo hili ni miongoni mwa sababu kuu za ndoa nyingi kufeli na hata kuanguka. Tatizo ni kwamba hata kama mwenza wako anakidhi asilimia 75 ya mahitaji yako makubwa kabisa kila siku, asilimia nyingine 25 haitatimizwa moja kwa moja. Hivyo, kwa mfano ukiolewa na mwanaume mchapakazi, mwenye mvuto na anayekupa raha kitandani, lakini hakuiti kwa majina mazuri yenye kukupendeza na hakusikilizi, unatakiwa kujifunza kuridhika na hiyo asilimia 75, kwa sababu hakuna anayeweza kukidhi mahitaji yako kwa asilimia zote. Wengine huwa wanashindwa kiasi kwamba wanafikia hatua ya kutafuta sehemu wanayoweza kujaza hizo asilimia 25 wanazozikosa. Hata huko wanakokwenda hawawezi kupata mtu anayeweza kuwapa furaha kwa asilimia zote na hujikuta wakiingia katika matatizo makubwa zaidi.

4) Kwa sababu ya usaliti:
Baadhi ya watu baada ya kukosa baadhi ya mambo machache kutoka kwa wenzao, kama nilivyosema katika namba 3, hukosa kuridhika na hivyo kuanza kutafuta mahali wanapoweza kukidhi ombwe hilo. Yumkini ukawa na hitajio la jambo dogo lakini kumbe hata huko ukawa huwezi kulipata. Yumkini ulihitaji tendo la ndoa lakini yumkini hitajia lako halisi ni zaidi ya hilo. Usaliti ni jambo la hatari sana kwenye ndoa yoyote, na likishatokea basi mambo hayawezi kuendelea kuwa katika hali ya kawaida. Mara nyingi pigo hilo huipeleka ndoa kwenye maporomoko.

5) Kwa sababu umekata tamaa mapema:
Sio kila tatizo huvunja uhusiano. Ni kawaida kwa wanandoa kukutana na mambo mazito katika maisha yao. Hukutana na matatizo ya kiuchumi, kufiwa na watoto na hata kutukanwa lakini bado huendelea kuwa imara na kuwa pamoja na hakuna anayemkimbia mwenzake. Kuna wengine wanapokutana na matatizo mazito hukata tamaa mapema, huhisi kuwa hawawezi kufanya stahmala hudhani kuwa changamoto hizo hawatozipata wakienda sehemu nyingine.

6) Kwa sababu hakuna fedheha:
Katika miaka ya 1800, kiwango cha talaka kilikuwa kidogo mno. Mwaka 1915 katika baadhi ya maeneo ndoa ilikuwa asilimia 5 ya ndoa zote, na ilikuwa kwa matukio maalumu kama vile unyanyasaji, uzinifu au utelekezaji wa familia.Katika baadhi ya maeneo, ili watu kuachana walihitaji kuidhiniwa na viongozi wa kiroho, wazazi na hata jamii za wahusika. Hata hivyo, wanandoa wengi walipata changamoto kubwa sana kwa sababu walilazimika kuishi katika ndoa zenye machafuko kwa sababu wasingeweza kustahmili “aibu” ya talaka. Suala la talaka lilionekana kama ni fedheha na aibua katika jamii. Lakini leo hii suala la talaka limekuwa jambo la kawaida na ni rahisi kufanywa na kukubaliwa na jamii. Watu wengi hawajali gharama zinazotokana na kuachana.

7) Kwa sababu unadhani kuwa wengine ndio wanaokosea:
Kuna kasumba mbaya sana katika baadhi ya ndoa ambapo mtu mmoja huwa MKAMILIFU na mwingine huwa MKOSEFU. Mwanandoa mmoja anaweza kujiona kuwa yeye hakosei na kumuona kuwa mwenza wake ndiye mkosefu siku zote. Hili ni tatizo ambalo huzigharimu ndoa nyingi. Ni muhimu sana kama wanandoa watakuwa watu SAHIHI badala ya kuwa WAKAMILIFU. Kwa sababu hilo ni jambo lisilowezekana. (Rejea mada yangu ya KANUNI YA SEKUNDE 30).

8) Kwa sababu wewe unataka upendo wakati yeye anahitaji heshima:
Jambo la kawaida, lakini ndoa hufeli pindi wanandoa wanaposhindwa kulielewa. Kwa ujumla mke ana silika ya kuhitaji upendo, ilhali mume anahitaji vipawa vyake vitambuliwe na kuheshimiwa. Tatizo ni kwamba tunajaribu kuwapa wenza wetu mambo ambayo tunayataka sisi, sio yale yanayoendana na silika zao. Angalia kwa mfano mke anamkosoa mume wake mbele ya watoto, mbele ya watu au hata kumuandika vibaya katika mitandao ya kijamii, hakika hilo litamvunjia heshima mume. Angalia pia mume ambaye anayejigamba kwa wengine kuhusu mkewe lakini akiwa nyumbani anampuuza. Ewe mume onesha upendo kwa mkeo, ewe mke mheshimu mumeo, mtaona mabadiliko.
 
The only thing I can say we both women and men have to have the Fear of God inside of us even if we are by ourselves ( privately ) . Kuwa na hofu ya Mungu ndani ya mioyo yetu will make us to walk in Holiness and Righteous paths.. Watu wengi now these days , tunajidanganya nafsi ,mioyo yetu na Mungu wetu when it comes kuishi vile ipasavyo.. For example utakuta a man or woman yuko na MTU in relationship ambayo INA promise ya kuoana but one of those two amemuahidi mwingine outside the same thing kama alivyomuahidi aliye nae ... Aliyedanganywa akigundua na kuongea na mwenzie kuhusu hilo , mkosaji anakataa na kujifanya mmbabe .. So tell me is it fair? My question is why he / she has to do this and playing with other's heart ? .. I think its good to live honest life .. Ni bora uchukiwe na humans being kwa kuwa mkweli because it will save a lot of damage , kuliko to lie and cause broken heart , that will lead us to Hell... To live without knowing our purpose in this earth , it's a waste and God hates it .. Because He created us to be more productive unto Him .. We must know and remember we both are here in this Earth to do God's will hivyo basi ni muhimu tujue kusudi letu la kuwepo hapa duniani .. Hii itatusaidia kujua position zetu pale Mungu alipotuweka ikiwemo kwa ndoa na mahusiano . Na hii itatuepusha na confusion ambazo Devil alizoziandaa.. In every God's will hakukosi vita hivyo basi ni vyema tuwe Honest to our God and ourselves ili His will ichukue nafasi.. Amen. Thanks..
 
The only thing I can say we both women and men have to have the Fear of God inside of us even if we are by ourselves ( privately ) . Kuwa na hofu ya Mungu ndani ya mioyo yetu will make us to walk in Holiness and Righteous paths.. Watu wengi now these days , tunajidanganya nafsi ,mioyo yetu na Mungu wetu when it comes kuishi vile ipasavyo.. For example utakuta a man or woman yuko na MTU in relationship ambayo INA promise ya kuoana but one of those two amemuahidi mwingine outside the same thing kama alivyomuahidi aliye nae ... Aliyedanganywa akigundua na kuongea na mwenzie kuhusu hilo , mkosaji anakataa na kujifanya mmbabe .. So tell me is it fair? My question is why he / she has to do this and playing with other's heart ? .. I think its good to live honest life .. Ni bora uchukiwe na humans being kwa kuwa mkweli because it will save a lot of damage , kuliko to lie and cause broken heart , that will lead us to Hell... To live without knowing our purpose in this earth , it's a waste and God hates it .. Because He created us to be more productive unto Him .. We must know and remember we both are here in this Earth to do God's will hivyo basi ni muhimu tujue kusudi letu la kuwepo hapa duniani .. Hii itatusaidia kujua position zetu pale Mungu alipotuweka ikiwemo kwa ndoa na mahusiano . Na hii itatuepusha na confusion ambazo Devil alizoziandaa.. In every God's will hakukosi vita hivyo basi ni vyema tuwe Honest to our God and ourselves ili His will ichukue nafasi.. Amen. Thanks..
uko sahihi ndugu,....tatizo hiki kizazi ukiongea mambo ya ki Mungu wanaona ni mambo ambayo hayawezekanii,.hii ni kwasababu ibilisi kapewa sana nafasi na wanadamu na ibilisi kakamata mioyo ya watu,.watu wamebobea ktk kumuwaza Mungu mabaya tu,..hawawazi kutenda mema kuishi katka njia za kumpendezesha Mungu,.wanaamini mke mwema uwe na pesa..hiki ndo kizazi cha sasa kinawaza uchafu kwa Mungu,..wakisikia bible inasema Mke mwema anatoka kwa Bwana wanaona kama vitu ambavyo havipo,.wanadhani ni hadithi haziwahusu,. wanasaau kama Bwana hapingani na neno lake milele,..mithali inasema mke mwenye busara anapaikana kwa BWANA,.wao wanaamini mke mwema pochi ielewke...sio wao bali ni shetani anawavuta ktk kitanzi,..shetani hana urafiki na binadam,..hata siku1,...tumrudie Mungu tuishi katika njia zake,..awe kiongoz kwa kila jambo,...tupate wake wema
 
uko sahihi ndugu,....tatizo hiki kizazi ukiongea mambo ya ki Mungu wanaona ni mambo ambayo hayawezekanii,.hii ni kwasababu ibilisi kapewa sana nafasi na wanadamu na ibilisi kakamata mioyo ya watu,.watu wamebobea ktk kumuwaza Mungu mabaya tu,..hawawazi kutenda mema kuishi katka njia za kumpendezesha Mungu,.wanaamini mke mwema uwe na pesa..hiki ndo kizazi cha sasa kinawaza uchafu kwa Mungu,..wakisikia bible inasema Mke mwema anatoka kwa Bwana wanaona kama vitu ambavyo havipo,.wanadhani ni hadithi haziwahusu,. wanasaau kama Bwana hapingani na neno lake milele,..mithali inasema mke mwenye busara anapaikana kwa BWANA,.wao wanaamini mke mwema pochi ielewke...sio wao bali ni shetani anawavuta ktk kitanzi,..shetani hana urafiki na binadam,..hata siku1,...tumrudie Mungu tuishi katika njia zake,..awe kiongoz kwa kila jambo,...tupate wake wema


Amen.. Mungu atusaidie Sana, tuzijue nyakati tulizo Nazo.. Because the hour is near , there is no more time to play with God.. Either we are inn or out .. We can't be lukewarm anymore because God will spit us .. Ooh may the Lord forgive us , in Jesus name, Amen.. Thanks..
 
Si kweli kuwa ndoa nyingi hazidumu ... ndoa chache ndizo hazidumu. Ndoa ni level ya juu kabisa ya kukomaa kwa uhusiano ambapo uandaaji na utekelezaji wake hutumia muda mwingi na rasilimi, hivyo si kitu cha haraka na rahisi kama wengi wanavyofikiri. Tatizo lililopo ni kasumba ya mob phychology ya vijana walio wengi kuamini hivyo ... Binafsi kwa umri wangu wa utu uzima na kuwa ndani ya ndoa, ninayo mifano michache sana ya ndoa zilizofunjika ilhali NDOA nyingi zaidi zikiwa bado zimegangamala.

Wote kwa pamoja tufikiri ... ni NDOA ngapi tumeshuhudia zikivunjika??!Kumbuka, nazungumzia NDOA na si uhusiano wa kinyumba ....!!!Hope ni chache sana. Tatizo lililopo ni la idadi ya wanaoingia kwenye NDOA kupungua na hili lisifananishwe kama tatizo la NDOA kuvunjika bali tatizo la MAHUSIANO kuvunjika.

Pessimistic wa NDOA wanapotumia takwimu za zamani kulinganisha NDOA za mababu zetu na zetu ni vizuri pia wakakumbuka chamngamoto za karne ya 21 kama vile ;
  1. Ukosefu wa ajira
  2. Umuhimu wa elimu
  3. Kupanda kwa gharama za maisha i.e Food, Shelter, Clothes, Healthcare etc
  4. Urbanization and Internal immigration i.e Wapenzi wengi wapo on the move so ina adhiri coupling
  5. Kuzorota kwa hali ya hewa na uoto wa asili i.e Kilimo duni=Chakula duni/ghali=Less job orportunity etc
Mwisho, niwakumbushe tu NDOA zote zina changamoto za hapa na pale but still bado ndio sehemu pekee muhimu na salama ya kujificha katika kipindi chako cha malezi ya familia na hapa duniani, kubwa ni kwa bidii zako na kumuomba MUNGU, upate mtu mnayependana na kuheshimiana.


(Ni mtazamo binafsi)
 
Hadi mtu kufikia kuoa, kuna sababu zake, wengi wanaoa kwa sababu zisizo sahihi.
 
The only thing I can say we both women and men have to have the Fear of God inside of us even if we are by ourselves ( privately ) . Kuwa na hofu ya Mungu ndani ya mioyo yetu will make us to walk in Holiness and Righteous paths.. Watu wengi now these days , tunajidanganya nafsi ,mioyo yetu na Mungu wetu when it comes kuishi vile ipasavyo.. For example utakuta a man or woman yuko na MTU in relationship ambayo INA promise ya kuoana but one of those two amemuahidi mwingine outside the same thing kama alivyomuahidi aliye nae ... Aliyedanganywa akigundua na kuongea na mwenzie kuhusu hilo , mkosaji anakataa na kujifanya mmbabe .. So tell me is it fair? My question is why he / she has to do this and playing with other's heart ? .. I think its good to live honest life .. Ni bora uchukiwe na humans being kwa kuwa mkweli because it will save a lot of damage , kuliko to lie and cause broken heart , that will lead us to Hell... To live without knowing our purpose in this earth , it's a waste and God hates it .. Because He created us to be more productive unto Him .. We must know and remember we both are here in this Earth to do God's will hivyo basi ni muhimu tujue kusudi letu la kuwepo hapa duniani .. Hii itatusaidia kujua position zetu pale Mungu alipotuweka ikiwemo kwa ndoa na mahusiano . Na hii itatuepusha na confusion ambazo Devil alizoziandaa.. In every God's will hakukosi vita hivyo basi ni vyema tuwe Honest to our God and ourselves ili His will ichukue nafasi.. Amen. Thanks..
Yes Mungu niwa kumtanguliza ila unadhan binadamu wote wana mwogopa Mungu? Kuna manabii wa Mungu waliuliwa na kudharauliwa.
 
sababu kubwa ni watu kushindwa kutofautisha kati ya ndoa na harusi ... na kuipa uzito mkubwa jambo la masaa machache na kusahahu jambo la kila siku .. lingine watu hawana hofu kabisa now days
Wanawake wanapenda sana harusi. Wanapenda sifa za kuolewa kwa harusi kubwa. kuwashitua mashosti wake. Ila mateso wanayopata ni kwa ajili ya kuchagua watu ambao sio sahihi.
 
Si kweli kuwa ndoa nyingi hazidumu ... ndoa chache ndizo hazidumu. Ndoa ni level ya juu kabisa ya kukomaa kwa uhusiano ambapo uandaaji na utekelezaji wake hutumia muda mwingi na rasilimi, hivyo si kitu cha haraka na rahisi kama wengi wanavyofikiri. Tatizo lililopo ni kasumba ya mob phychology ya vijana walio wengi kuamini hivyo ... Binafsi kwa umri wangu wa utu uzima na kuwa ndani ya ndoa, ninayo mifano michache sana ya ndoa zilizofunjika ilhali NDOA nyingi zaidi zikiwa bado zimegangamala.

Wote kwa pamoja tufikiri ... ni NDOA ngapi tumeshuhudia zikivunjika??!Kumbuka, nazungumzia NDOA na si uhusiano wa kinyumba ....!!!Hope ni chache sana. Tatizo lililopo ni la idadi ya wanaoingia kwenye NDOA kupungua na hili lisifananishwe kama tatizo la NDOA kuvunjika bali tatizo la MAHUSIANO kuvunjika.

Pessimistic wa NDOA wanapotumia takwimu za zamani kulinganisha NDOA za mababu zetu na zetu ni vizuri pia wakakumbuka chamngamoto za karne ya 21 kama vile ;
  1. Ukosefu wa ajira
  2. Umuhimu wa elimu
  3. Kupanda kwa gharama za maisha i.e Food, Shelter, Clothes, Healthcare etc
  4. Urbanization and Internal immigration i.e Wapenzi wengi wapo on the move so ina adhiri coupling
  5. Kuzorota kwa hali ya hewa na uoto wa asili i.e Kilimo duni=Chakula duni/ghali=Less job orportunity etc
Mwisho, niwakumbushe tu NDOA zote zina changamoto za hapa na pale but still bado ndio sehemu pekee muhimu na salama ya kujificha katika kipindi chako cha malezi ya familia na hapa duniani, kubwa ni kwa bidii zako na kumuomba MUNGU, upate mtu mnayependana na kuheshimiana.


(Ni mtazamo binafsi)
Sio ndoa zote zina vunjika. Ila zikifungwa 10 leo kesho 3 hazipo. Na chanzo cha uvunjifu wa hizo ndoa ni hayo niliosema hapo juu.
 
Yes Mungu niwa kumtanguliza ila unadhan binadamu wote wana mwogopa Mungu? Kuna manabii wa Mungu waliuliwa na kudharauliwa.

I do understand your point but remember kwa wale waliozidi kumtumania Mungu , Hakika aliye above aliwapigania.. Even in the Bible talks about the anger of the Lord that was up on those who killed Prophets na kwa wale waliowadharau His servants .. There is no short cut way .. Its only Fear of God will make us to do well in our lives ... Tupende , tusipende ...Because the eyes of the Lord are up on His Righteous ... Mwenye masikio na asikie.. Thanks ..
 
ndoa ndoa ndoa...ukiwa kwenye ndoa ndio utajua wapi ulichemsha......ukiwa nje katu hutojua, unabahatisha tuu.
 
Katika taasisi yenye figisufigisu nyingi duniani ni hii."life is the most difficult exam many people fail because they try to copy others not realizing that every one has a different question paper."leo mkeo anakwambia umpeleke mwanenu penye hizi shule za Saint nininini sijui waqt mfuko hauruhusu au yupo penye hizo Saint nini but anakwambia kuna Saint nyingine nzuri kuliko hiyo mfanyakazi mwenzangu mtoto wake yupo huko.
Hapo ujue kuna ongezeko la malipo huja kaa sawa kakwambia kuna mchango wa kitchen party sijui tandiko(kigodoro)mara viatu fasion mpya aah kinachofuatia mpini hausimami moja mara mwezi bado kuna ndoa hapo?
Ukija kwa vidume ndo balaa macho juu kwa kila bint matokeo yake anakuwa ana wanawake wa tatu ana wahudumia stress kwa kwenda mbele visirani vya kufikia kuna ndoa hapo?.
 
I do understand your point but remember kwa wale waliozidi kumtumania Mungu , Hakika aliye above aliwapigania.. Even in the Bible talks about the anger of the Lord that was up on those who killed Prophets na kwa wale waliowadharau His servants .. There is no short cut way .. Its only Fear of God will make us to do well in our lives ... Tupende , tusipende ...Because the eyes of the Lord are up on His Righteous ... Mwenye masikio na asikie.. Thanks ..
Mungu yupo ila binadamu wameziba masikio. Thats was my point.
 
Katika taasisi yenye figisufigisu nyingi duniani ni hii."life is the most difficult exam many people fail because they try to copy others not realizing that every one has a different question paper."leo mkeo anakwambia umpeleke mwanenu penye hizi shule za Saint nininini sijui waqt mfuko hauruhusu au yupo penye hizo Saint nini but anakwambia kuna Saint nyingine nzuri kuliko hiyo mfanyakazi mwenzangu mtoto wake yupo huko.
Hapo ujue kuna ongezeko la malipo huja kaa sawa kakwambia kuna mchango wa kitchen party sijui tandiko(kigodoro)mara viatu fasion mpya aah kinachofuatia mpini hausimami moja mara mwezi bado kuna ndoa hapo?
Ukija kwa vidume ndo balaa macho juu kwa kila bint matokeo yake anakuwa ana wanawake wa tatu ana wahudumia stress kwa kwenda mbele visirani vya kufikia kuna ndoa hapo?.
Asante kwa maoni yako.
 
Back
Top Bottom