Thadei Ole Mushi
R I P
- Oct 13, 2018
- 35
- 259
Na Thadei Ole Mushi.
Someni Ripoti ya CAG, Kuna madudu mengi mno mengine yanatia kinyaa kabisa. Ukurasa wa 70 wa Ripoti hiyo unazungumzia issue ya Kucheleweshwa ujenzi wa kiwanda Cha Pamba kule Simiyu. Naomba kuinukuu hiyo Ripoti neno kwa neno:
"Mnamo tarehe 11 Novemba 2016 Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Mfuko wa Taifa wa Bima wa Afya (NHIF), Mfuko wa Fidia kwa Wafanyakazi (WCF), Bohari Kuu ya Dawa (MSD), Benki ya Uwekezaji Tanzania (TIB), Shirika la Utafiti na Maendeleo ya Viwanda Tanzania (TIRDO), Shirika la Viwango Tanzania (TBS), na Mamlaka ya Dawa na Vifaatiba Tanzani (TMDA) (kabla ilikuwa Mamlaka ya Udhibiti wa Chakula na Dawa (TFDA)) walisaini Randama ya Makubaliano kwa ajili ya kuanzisha kiwanda cha vifaatiba vitokanavyo na zao la pamba katika eneo la Dutwa mkoani Bariadi.
Katika makubaliano hayo Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Simiyu ilikubali kutoa Ardhi kwa ajili ya kiwanda bure, MSD ilikubali kuwa mteja
mkuu wa bidhaa hizo, TMDA walikubali kutoa ushauri wa uzalishaji wa bidhaa hizo ili ziwe na ubora unaotakiwa, TBS walikubali kutoa
ushauri wa viwango vinavyohitajika ili bidhaa hizo ziwe na ubora unaotakiwa, na Benki ya Maendeleo ya TIB ilikubali kutoa ushauri
wa kifedha pamoja na mkopo wa mtaji.
Aidha, mnamo tarehe 13 Juni 2018 WCF na NHIF zilifungua kampuni inayoitwa Simiyu Medical Products Company Limited kwa ajili ya
usimamizi wa shughuli zote za uanzishaji wa kiwanda. Kufuatia Randama na Hati ya Ushirikiano ya Kampuni, mnamo tarehe 12 Juni 2019, Bodi ya usimamizi wa Kampuni hiyo iliteuliwa na Waziri wa Afya.
Aidha, nilibaini kuwa timu ya uchunguzi wa teknolojia ya kiwanda ilienda Uturuki mwezi Machi, 2019 na India na China mwezi Disemba 2019. Kwa mujibu wa taarifa ya uchunguzi gharama za mashine pamoja na mtaji unaohitajika ni shilingi bilioni 69.2.
Aidha, kiwanda kitakuwa na uwezo wa kuzalisha bidhaa 19 zinazotokana na pamba. Pia, mpaka muda wa ukaguzi nilibaini jumla ya shilingi milioni 915.98 zimetumika katika maandalizi ya mwazo ya kiwanda ikiwemo kufanya upembuzi yakinifu.
Pia, kwa mujibu wa taarifa ya upembuzi yakinifu uliofanywa na TIRDO, kiwanda kitatoa jumla ya ajira za moja kwa moja zaidi ya
600 pamoja na ajira zisizo za moja kwa moja zaidi ya 1000.
Pamoja na hayo kitasaidia kupunguza uagizaji wa bidhaa za hospitali kutoka nje ya nchi zinazotokana na pamba, hivyo, kusaidiakupunguza mahitaji ya fedha za kigeni.
NHIF na WCF kupitia Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee, na Watoto iliomba kibali cha ujenzi wa kiwanda hiki kutoka Wizara ya Fedha na Mipango mnamo tarehe 26 Juni, 2019 ila mpaka ninakamilisha ukaguzi wangu katika mashirika haya mnamo tarehe 15 Disemba 2020 kibali hicho kilikuwa bado hakijatolewa, hivyo, kibali hicho kimechelewa kutolewa kwa siku 538 toka kiombwe mpaka kufikia tarehe ya kukamilisha ukaguzi huu." MWISHO wa kunukuu......
Haya maelezo yapo kwenye Ripoti ya CAG kuanzia Ukurasa wa 70. Sasa turudi kwenye Hoja.
Faida za kujengwa kiwanda hiki ni Kubwa mno, kwa mwaka Tanzania huagiza nje ya nchi vifaa tiba vinavyotokana na Pamba vifaa vyenye Thamani ya Shilingi bilioni 79 hadi 75. Gharama za kujenga kiwanda hiki ni Shilingi bilioni 69 tu na kingeokoa bilioni 75 zingebaki hapa nchini. Fedha zipo kila kitu kimeshafanyika ni Mtu alitakiwa asaini tu pale Wizara ya Fedha lakini hakufanya hivyo.
Nani hajui kilio Cha Wakulima wa Pamba waliopo kwenye mikoa ya Kanda ya Ziwa? Kila siku wanalia kukopwa pamba au Pamba kuozea kwenye magodown. Nani anayejali as Long as yupo kwenye kiyoyozi Cha V8? Kiwanda hiki kingefyonza Pamba yote na Wala isingetosha na Wakulima wangelikuwa wamenufaika Sana.
Tanzania ilipewa tenda ya kusambaza vifaa tiba kwenye nchi za SADC Kama kiwanda hiki kingejengwa ukiachana na Soko la ndani bado tungepata Soko Kusini mwa Africa Soko la uhakika kabisa.
CAG amesema kingetoa ajira kwa vijana wetu nk.
Nani anajali?
Cha kushangaza watu hao hao walioacha kusaini kibali Hicho bado wapo Serikalini. Hakuna aliyewajibishwa..... Ingelikuwa Mataifa ambayo yapo Serious kabisa Hawa watu walisakula Kitanzi mapema Sana. Yaani kusaini tu.
Ole Mushi
0712702602.
Someni Ripoti ya CAG, Kuna madudu mengi mno mengine yanatia kinyaa kabisa. Ukurasa wa 70 wa Ripoti hiyo unazungumzia issue ya Kucheleweshwa ujenzi wa kiwanda Cha Pamba kule Simiyu. Naomba kuinukuu hiyo Ripoti neno kwa neno:
"Mnamo tarehe 11 Novemba 2016 Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Mfuko wa Taifa wa Bima wa Afya (NHIF), Mfuko wa Fidia kwa Wafanyakazi (WCF), Bohari Kuu ya Dawa (MSD), Benki ya Uwekezaji Tanzania (TIB), Shirika la Utafiti na Maendeleo ya Viwanda Tanzania (TIRDO), Shirika la Viwango Tanzania (TBS), na Mamlaka ya Dawa na Vifaatiba Tanzani (TMDA) (kabla ilikuwa Mamlaka ya Udhibiti wa Chakula na Dawa (TFDA)) walisaini Randama ya Makubaliano kwa ajili ya kuanzisha kiwanda cha vifaatiba vitokanavyo na zao la pamba katika eneo la Dutwa mkoani Bariadi.
Katika makubaliano hayo Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Simiyu ilikubali kutoa Ardhi kwa ajili ya kiwanda bure, MSD ilikubali kuwa mteja
mkuu wa bidhaa hizo, TMDA walikubali kutoa ushauri wa uzalishaji wa bidhaa hizo ili ziwe na ubora unaotakiwa, TBS walikubali kutoa
ushauri wa viwango vinavyohitajika ili bidhaa hizo ziwe na ubora unaotakiwa, na Benki ya Maendeleo ya TIB ilikubali kutoa ushauri
wa kifedha pamoja na mkopo wa mtaji.
Aidha, mnamo tarehe 13 Juni 2018 WCF na NHIF zilifungua kampuni inayoitwa Simiyu Medical Products Company Limited kwa ajili ya
usimamizi wa shughuli zote za uanzishaji wa kiwanda. Kufuatia Randama na Hati ya Ushirikiano ya Kampuni, mnamo tarehe 12 Juni 2019, Bodi ya usimamizi wa Kampuni hiyo iliteuliwa na Waziri wa Afya.
Aidha, nilibaini kuwa timu ya uchunguzi wa teknolojia ya kiwanda ilienda Uturuki mwezi Machi, 2019 na India na China mwezi Disemba 2019. Kwa mujibu wa taarifa ya uchunguzi gharama za mashine pamoja na mtaji unaohitajika ni shilingi bilioni 69.2.
Aidha, kiwanda kitakuwa na uwezo wa kuzalisha bidhaa 19 zinazotokana na pamba. Pia, mpaka muda wa ukaguzi nilibaini jumla ya shilingi milioni 915.98 zimetumika katika maandalizi ya mwazo ya kiwanda ikiwemo kufanya upembuzi yakinifu.
Pia, kwa mujibu wa taarifa ya upembuzi yakinifu uliofanywa na TIRDO, kiwanda kitatoa jumla ya ajira za moja kwa moja zaidi ya
600 pamoja na ajira zisizo za moja kwa moja zaidi ya 1000.
Pamoja na hayo kitasaidia kupunguza uagizaji wa bidhaa za hospitali kutoka nje ya nchi zinazotokana na pamba, hivyo, kusaidiakupunguza mahitaji ya fedha za kigeni.
NHIF na WCF kupitia Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee, na Watoto iliomba kibali cha ujenzi wa kiwanda hiki kutoka Wizara ya Fedha na Mipango mnamo tarehe 26 Juni, 2019 ila mpaka ninakamilisha ukaguzi wangu katika mashirika haya mnamo tarehe 15 Disemba 2020 kibali hicho kilikuwa bado hakijatolewa, hivyo, kibali hicho kimechelewa kutolewa kwa siku 538 toka kiombwe mpaka kufikia tarehe ya kukamilisha ukaguzi huu." MWISHO wa kunukuu......
Haya maelezo yapo kwenye Ripoti ya CAG kuanzia Ukurasa wa 70. Sasa turudi kwenye Hoja.
Faida za kujengwa kiwanda hiki ni Kubwa mno, kwa mwaka Tanzania huagiza nje ya nchi vifaa tiba vinavyotokana na Pamba vifaa vyenye Thamani ya Shilingi bilioni 79 hadi 75. Gharama za kujenga kiwanda hiki ni Shilingi bilioni 69 tu na kingeokoa bilioni 75 zingebaki hapa nchini. Fedha zipo kila kitu kimeshafanyika ni Mtu alitakiwa asaini tu pale Wizara ya Fedha lakini hakufanya hivyo.
Nani hajui kilio Cha Wakulima wa Pamba waliopo kwenye mikoa ya Kanda ya Ziwa? Kila siku wanalia kukopwa pamba au Pamba kuozea kwenye magodown. Nani anayejali as Long as yupo kwenye kiyoyozi Cha V8? Kiwanda hiki kingefyonza Pamba yote na Wala isingetosha na Wakulima wangelikuwa wamenufaika Sana.
Tanzania ilipewa tenda ya kusambaza vifaa tiba kwenye nchi za SADC Kama kiwanda hiki kingejengwa ukiachana na Soko la ndani bado tungepata Soko Kusini mwa Africa Soko la uhakika kabisa.
CAG amesema kingetoa ajira kwa vijana wetu nk.
Nani anajali?
Cha kushangaza watu hao hao walioacha kusaini kibali Hicho bado wapo Serikalini. Hakuna aliyewajibishwa..... Ingelikuwa Mataifa ambayo yapo Serious kabisa Hawa watu walisakula Kitanzi mapema Sana. Yaani kusaini tu.
Ole Mushi
0712702602.