Mwishokambi
JF-Expert Member
- Nov 23, 2020
- 303
- 1,158
Leo kwenye press conference nimeona Ceo wa Simba na afisa habari wakiwakilisha klabu yao ya Simba, kwa upande wa GSM walikuwepo Haji Manara, Senzo Mazingiza na afisa habari wa Yanga Hassan Bumbuli.
Kwa kweli nashindwa kuelewa kwann shughuli za Yanga siwaoni Msolla wala Mwakalebela ambao ndio viongozi halali wa Yanga kwa mujibu wa katiba, hao akina Senzo na Manara ni wawakilishi wa GSM ndani ya Yanga, je, nani analinda maslahi ya Yanga kwa sasa, je kwa vile Yanga wanafanya vzr basi mashabiki na wanachama hawaoni sababu ya kuhoji lolote, kwamba wao furaha ni matokeo ya ushindi tu?
Kwann waandishi wa habari hasa popoma Kitenge hawamuulizi Msolla na Mwakalebela maswali haya, kwamba kazi yao ni kufungua mashina, vikao na kufunga vikao? Wana faida gani ya kuwepo Yanga sasa, je hawaoni kuwa wakiwepo au wasiwepo Yanga haiwezi kutetereka? Kwann GSM ameteka madaraka ya akina Msolla, kwann Bumbuli anapewa nafasi ndogo au anadharaulika sana Yanga kuliko zungu pori?
Kwa kweli nashindwa kuelewa kwann shughuli za Yanga siwaoni Msolla wala Mwakalebela ambao ndio viongozi halali wa Yanga kwa mujibu wa katiba, hao akina Senzo na Manara ni wawakilishi wa GSM ndani ya Yanga, je, nani analinda maslahi ya Yanga kwa sasa, je kwa vile Yanga wanafanya vzr basi mashabiki na wanachama hawaoni sababu ya kuhoji lolote, kwamba wao furaha ni matokeo ya ushindi tu?
Kwann waandishi wa habari hasa popoma Kitenge hawamuulizi Msolla na Mwakalebela maswali haya, kwamba kazi yao ni kufungua mashina, vikao na kufunga vikao? Wana faida gani ya kuwepo Yanga sasa, je hawaoni kuwa wakiwepo au wasiwepo Yanga haiwezi kutetereka? Kwann GSM ameteka madaraka ya akina Msolla, kwann Bumbuli anapewa nafasi ndogo au anadharaulika sana Yanga kuliko zungu pori?