Kwa porojo hizi za TRA ndiyo maana hata mapato ya kila mwezi yamebaki "midomoni" mwao

G Sam

JF-Expert Member
Apr 20, 2013
11,555
35,874
Jana nilisikia taarifa kutoka TRA kuhusiana na ongezeko la kodi yaani V.A.T kwenye miamala ya simu na benki pia huduma zote za kifedha nikaanza kujiuliza maswali mengi bila majibu.

Eti TRA wanasema kuwa hiyo nyongeza ya asilimia 18 watakatwa mawakala wao kwamba mwananchi hakitakiwi kuguswa. Hizi ni porojo za aina yake kutolewa na taasisi nyeti ya kiserikali kama TRA.

Mimi moja kwa moja baada ya kusikia taarifa ile mbiombio nikawaza kuwa, ina maana TRA wamemega mapato yao ya mwisho wa mwaka yaani income tax? Kwamba mwisho wa mwaka pale tarehe 30 December wakati wa kulipa kodi ya income tax tayari tutaondoa ongezeko la 18% tulilolipa kama mawakala kwa kila muamala wateja wetu waliofanya? Nikamuuliza kidogo mmoja wa TRA akaniambia lah hasha bali mzigo huo ni wa mawakala bila kugusa makodi ya TRA ya mwisho wa mwaka na makodi mengine ya bodi mbalimbali. Nikastaajabu na kumuuliza, hiyo kodi inayotakiwa kulipwa nje ya utaratibu itatoka wapi?

Bahati mbaya au nzuri hata sheria ya kodi ya fedha "finance act imeeleza bayana kuwa mteja wa wakala ndiye atakayelipia kodi hiyo (Nyongeza) iliyopendekezwa na serikali.

Baada ya kuona jambo dogo kama lile likiwachanganya TRA, sasa nimekata jawabu la yale mapato yanayotangazwa kwa mbwembwe mbona hayaonekani? Na kwa ghafla sana nimeanza kuzipuuza taarifa mbalimbali zinazotolewa na TRA kwani nimegundua kuwa wamekalia tu siasa na porojo ila uhalisia unaonekana waziwazi.
 
TRA hawajaacha Taaluma hawajui kitu kabisa wanafanya madudu mengi waangaliwe hao...wameweka VAT kwa mizigo ya Transit wakati nchi zingine VAT mgeni unarudishiwa unapotoka iwe boarder unayotoka au airport...
Fafanua hapo mkuu
 
Wahuni kweli hawa TRA ya Magu.
kwanza tujiulize swali dogo , ungezeko la thamani maana yake ni nini? Anathaminisha nani bidhaa na kisha aweke ongezeko? Hilo ongezeko litalipwa na mthaminishaji ama mteja? Ukipata majibu sahihi ya maswali haya utgundua kuwa hilo ongezeko ni mzigo wa mlaji wa mwisho na sii vinginevyo
 
NIMEGUNDUA KUWA WANAOWAPINGA TRA HAPA NA KUWAPONDA NI MAWAKALA. SAS PANDISHENI VIWANGO VILIVYOWEPO MUONE CHA MTEMA KUNI.
 
Kwa kweli taaruma ya tax naona inapotea live live.sikutegemea kuona hata CAG anashisndwa kupambanua ni namna gani kodi ya ongezeko la thamani inavyotakiwa kulipwa.asiwahadae watanzania hasa Kwa kukosa taaluma ya kodi na kudhani watanzania wote hawajui kodi.ieleweke kuwa final consumer ndiyo mlipaji wa VAT na final consumer siyo benki wala siyo mitandao ya simu .final consumer ni mwananchi.alichokielezea Gavana wa benki kuu ni sahihi kabisa lakini alichokielezea CAG Kwa kweli sijui hii taaluma kaitolea wapi.mi sishangai sababu kila kitu naona hakifuati sheria au act Kama inavyotaka Bali ni maamuzi binafsi
 
Budget ya Mwaka huu ina kusanya mapato tu.. bila kuangalia inayakusanyeje!!

Hiyo ni kodi1 tu na tiyari ishagonga mwamba. Wa kuumia hapa ni Raia siyo benki. Lazima No tutasoma wote na za kila rangi. Kosa ni huyu Tulia kufukuza vichwa Bungeni na kuacha V.ilaz,,a.
 
....niko upande wa TRA,kwanini mabenki yatulipishe wananchi pesa ambayo wangetakiwa kulipa wao?, wao mabenki si tayari walikuwa wanakata 800/- kwenye ATM, then serikali ilipotangaza kuwadai kodi wakapandisha mpaka 944/-!, ina maana wao wanataka faida yao ibaki palepale ila sisi wananchi ndio tuumie kwa niaba yao? HAIWEZEKANI.
 
Walifikiria wanawakomoa Ukawa bungeni kumbe wananchi wanaenda kuumia na kususia kila kitu anzia huduma z banki na simu ukawa wangekuwepo wangejadiliana na kufikia muafaka! Wabunge w ccm vilaza wanajali maslahi yao tu! Tunawasubiri waje waibe tena kura!! nchi itasimama.....kodi hizo hazikubaliki kwa wananchi wala mabenki hawataki!
 
Wahuni kweli hawa TRA ya Magu.
kwanza tujiulize swali dogo , ungezeko la thamani maana yake ni nini? Anathaminisha nani bidhaa na kisha aweke ongezeko? Hilo ongezeko litalipwa na mthaminishaji ama mteja? Ukipata majibu sahihi ya maswali haya utgundua kuwa hilo ongezeko ni mzigo wa mlaji wa mwisho na sii vinginevyo
Yaani mimi nimeshangaa sana jinsi TRA walivojidhalilisha jana. Hivi ina maana TRA hakuna wasomi wanaojua maana ya VAT??. Hiyo kodi hulipwa na mlaji wa mwisho. Nikashangaa sana eti wanasema sio ya mlaji, nikajiuliza mabenki yatapata wapi pesa hiyo kwani income/profit tax imefutwa??? Baadala yake wameweka VAT?? Kwakweli ni bora kukaa kimya kuliko kutoa ufafanuzi wa namna ile.
 
....niko upande wa TRA,kwanini mabenki yatulipishe wananchi pesa ambayo wangetakiwa kulipa wao?, wao mabenki si tayari walikuwa wanakata 800/- kwenye ATM, then serikali ilipotangaza kuwadai kodi wakapandisha mpaka 944/-!, ina maana wao wanataka faida yao ibaki palepale ila sisi wananchi ndio tuumie kwa niaba yao? HAIWEZEKANI.
Umeeleza vizuri mkuu, wanaosema beno nduru yuko sahihi nashindwa kuwaelewa,kila kampuni inayofanya biashara ni lazima ilipe kodi na kodi hiyo inakatwa kwenye mapato ya kampuni husika.Hii ni hesabu rahisi lakn wenye mabenki wanatufanya tuwe kama wajinga wao.
 
....niko upande wa TRA,kwanini mabenki yatulipishe wananchi pesa ambayo wangetakiwa kulipa wao?, wao mabenki si tayari walikuwa wanakata 800/- kwenye ATM, then serikali ilipotangaza kuwadai kodi wakapandisha mpaka 944/-!, ina maana wao wanataka faida yao ibaki palepale ila sisi wananchi ndio tuumie kwa niaba yao? HAIWEZEKANI.
nini maana ya VAT?...........
 
....niko upande wa TRA,kwanini mabenki yatulipishe wananchi pesa ambayo wangetakiwa kulipa wao?, wao mabenki si tayari walikuwa wanakata 800/- kwenye ATM, then serikali ilipotangaza kuwadai kodi wakapandisha mpaka 944/-!, ina maana wao wanataka faida yao ibaki palepale ila sisi wananchi ndio tuumie kwa niaba yao? HAIWEZEKANI.
Mkuu ww hujui sera za biashara. Kila kampuni ina profit policy yake interms of percentage. Kwamba kwenye kila muamala benki imejiwekea sera ipate faida kiasi gani, sasa unapomwongezea cost nayeye atatafuta namna ya kumaintiain profit yake ileile ambapo kimsingi ni lazima ataongeza bei ya bidhaa husika. Kwahiyo hamna namna ni lazima benki zitaongeza bei zao. Mfano mdogo. Ulikuwa unanunua mzigo wa jumla kwa bei X na ww unsuza kwa bei Z. sasa hivi bei ya mzigo wa jumla imepanda hadi bei Y, je ukienda kuuza kwa reja reja utauza kwa bei ileile uliyokuwa unauza mwanzo au nawewe utaongeza??
Ni jambo la kibiashara wala si wizi.
 
10 Reactions
Reply
Back
Top Bottom