Kirchhoff
JF-Expert Member
- Nov 4, 2010
- 5,309
- 7,502
Tumsifu Yesu Kristu,
Naanza ujumbe huu Kwa Jina La Baba na La Mwana na La Roho Mtakatifu. Amina.
Ndugu katika Kristu Yesu,
Ni matumaini yangu kuwa waendelea vizuri na utume wako. Tumshukuru Mwenyenzi Mungu kwa afya njema.
Mara kwa mara mambo mengi yameibuliwa na kuwatuhumu viongozi wa chama cha CCM wakiwamo marais ambao ni wakatoliki kuhusishwa na kashfa mbali mbali za Ufisadi, Uhujumu Uchumi na Mauaji katika ngazi mbali mbali.
Yawezekana wameungama dhambi zao pale ambapo wametuhumiwa ukweli na wakaungama.
Taratibu za maungamo katika kanisa katoliki zajulikana kwa Wakristu wakatoliki popote ulimwenguni. Hapa nitazungumzia kipengele cha "Kutimiza Malipizi". Je Viongozi hawa wametimiza malipizi ya dhambi zao? Au wamekuja kuhitaji baraka za Mwenyezi Mungu kwa ile sala ya "Baba wasamehe, hawajui watendalo" kwetu sisi tunaowatuhumu?
Ni wakati sasa wa Kanisa kuwataka viongozi wa Nchi ambao ni wakatoliki kujisafisha Hadharani. Ni aibu kwa kanisa endapo kiongozi asiyejisafisha kuhudumiwa nalo. Yawezekana kusubiri wakati ambapo Roho Mtakatifu atawahimiza kufanya hivyo na Muda ndo huu ambapo Roho mtakatifu ameniagiza kutoa tamko hili.
Roho wa Bwana anataka kanisa liingilie kati mambo yanayoendelea Nchini. Kanisa lisifunge Mdomo.
Kanisa liwe na takwimu ya viongozi wa Nchi ambao ni wakatoliki na liwapatie mafunzo ya Uongozi wa Kimungu ili waweze kuhudumia kuhudumia watu wa Mungu kama apendavyo Mungu.
Kwa Jina La Baba na La Mwana Na La Roho Mtakatifu. Amina.
Naanza ujumbe huu Kwa Jina La Baba na La Mwana na La Roho Mtakatifu. Amina.
Ndugu katika Kristu Yesu,
Ni matumaini yangu kuwa waendelea vizuri na utume wako. Tumshukuru Mwenyenzi Mungu kwa afya njema.
Mara kwa mara mambo mengi yameibuliwa na kuwatuhumu viongozi wa chama cha CCM wakiwamo marais ambao ni wakatoliki kuhusishwa na kashfa mbali mbali za Ufisadi, Uhujumu Uchumi na Mauaji katika ngazi mbali mbali.
Yawezekana wameungama dhambi zao pale ambapo wametuhumiwa ukweli na wakaungama.
Taratibu za maungamo katika kanisa katoliki zajulikana kwa Wakristu wakatoliki popote ulimwenguni. Hapa nitazungumzia kipengele cha "Kutimiza Malipizi". Je Viongozi hawa wametimiza malipizi ya dhambi zao? Au wamekuja kuhitaji baraka za Mwenyezi Mungu kwa ile sala ya "Baba wasamehe, hawajui watendalo" kwetu sisi tunaowatuhumu?
Ni wakati sasa wa Kanisa kuwataka viongozi wa Nchi ambao ni wakatoliki kujisafisha Hadharani. Ni aibu kwa kanisa endapo kiongozi asiyejisafisha kuhudumiwa nalo. Yawezekana kusubiri wakati ambapo Roho Mtakatifu atawahimiza kufanya hivyo na Muda ndo huu ambapo Roho mtakatifu ameniagiza kutoa tamko hili.
Roho wa Bwana anataka kanisa liingilie kati mambo yanayoendelea Nchini. Kanisa lisifunge Mdomo.
Kanisa liwe na takwimu ya viongozi wa Nchi ambao ni wakatoliki na liwapatie mafunzo ya Uongozi wa Kimungu ili waweze kuhudumia kuhudumia watu wa Mungu kama apendavyo Mungu.
Kwa Jina La Baba na La Mwana Na La Roho Mtakatifu. Amina.