Kwa “nonsense” ya Sukari, Rais Samia anastahili pongezi. Je, tuishie kwenye "nonsense" ya Sukari tu au tuangazie na "nonsense" nyingine zote?

View attachment 2036704

Wanabodi,

Hili ni bandiko lililotokana na makala yangu hii, kwenye Safu yangu ya "Kwa Maslahi ya Taifa", kwenye gazeti la Nipashe kila siku za Jumapili. Kila nipatapo muda, huja na hizi makala zangu za "Kwa Maslahi ya Taifa" ambazo huja kwa mtindo wa swali, halafu jibu utatoa wewe msomaji mwenyewe.

Makala ya leo, ni makala ya pongezi kwa Rais Samia, kwa “nonsense” ya sukari, Rais Samia, anastahili pongezi za dhati, swali ni jee tuishie kwenye nonsense ya sukari tuu, au tuangazie na nonsense nyingine zote tuziache tusonge mbele? .

Naomba kuanza mada yangu ya leo, kwa kufundisha lugha kidogo, neno “nonsense” ni neno la kizungu lenye kumaanisha “ujinga”, hivyo uamuzi wowote unaiotwa “nonsense” ni “uamuzi wa kijinga”, Baba wa Taifa, alilitumia sana neno hili “nonsense”, ila yeye Baba wa Taifa, haikuishia tuu kwenye kulaumu maamuzi ya kijinga, “nonsense”, bali pia aliwaita watoa maamuzi hayo “wajinga”, ninanayo mifano mingi ya Mwalimu Nyerere kutumia neno “nonsense”

Mfano mzuri kabisa ni wakati Mwalimu Nyerere anaaga na kungatuka kwenye urais, alikiri serikali yake imefanya makosa mengi tuu , akakiri kuna baadhi ya maamuzi yalikuwa ni “nonsense”, makosa, lakini pia akasema “kufanya kosa sii kosa, kosa kurudia kosa”.

Wakati tukijiandaa kwa uchaguzi wa kwanza wa vyama vingi, ile 1995, Mwalimu alizungumza na sisi waandishi wa habari, kwenye ukumbi wa Hoteli ya Kilimanjaro, na mimi nilikuwepo, akizungungumzia ubinafsishaji wa benki ya NBC, Mwalimu akaishangaa serikali kukubali masherti ya nchi mabeberu, kuwa NBC ni li benki likubwa sana, lenye nguvu sana, lazima livunjwe, ndipo turuhusu ushindani wa mabenki, Mwalimu akauli NBC ina ukubwa gani?, “a mere NBC?!, this is “nonsense”.


Hata hapa, kwenye video hii

kwa hisani ya Dada yangu, Maria Sarungi, Baba wa Taifa alitumia neno nonsense.

Mtu kuambiwa mjinga, ni kweli umetukanwa lakini ujinga sio tusi, ni kutojua tuu, mtu mjinga akiisha elimishwa, ujinga unamtoka, anakuwa mwerevu. Mtu mjinga akiisha elimishwa, ujinga usipomtoka, huyo sasa sio mjinga, huyo ni mpumbavu!.


Rais Mkapa wakati wa uzinduzi wa kampeni za CCM kwa uchaguzi mkuu wa mwaka 2015, aliwaita watu fulani “malofa na wapumbavu”,
na haikuwa habari kubwa.

Rais Magufuli, aliwahi kumuita mawaziri fulani “mpumbavu” na haikuwa habari kubwa.


Juzi kati katika ziara za Rais Yoweri Museveni nchini Tanzania, katika kuzungumzia hoja ya sukari, Rais Samia pia alitumia neno “nonsense”.

Baada ya kutumika kwa neno hilo, huku kwenye mitandao ya kijamii kukalipuka “Rais Samia Katukana”, aliyetoa msimamo kuwa Tanzania hatutanunua sukari ya Uganda ni Waziri wa Kilimo, Prof. Adolf Mkenda. Baadhi ya mitandao ya kijamii ikamchagiza Prof. Mkenda kuwa asikubali kutukanwa hadharani, bora ajiuzulu kutunza heshima yake na asipojiuzulu atatumbuliwa!.

Sio mara moja nimeongea katika makala zangu, kuwa media ya Tanzania, hatuna watu wazuri wa kufanya uchambuzi wa habari, “news analysis”, Rais Samia alipotumia neno “Nonsense”, hakumtukana Waziri Prof. Mkenda ni “nonsense”, ameishangaa uamuzi ule wa kugomea sukari ya Uganda kwa kisingizio cha kulinda viwanda vya ndani, hivyo lile neno “nonsense” ni neno kwa ajili ya uamuzi ule na sio kwa ajili ya kumlenga mtu Prof. Mkenda.

Naomba tukubaliane, kama neno “nonsense” ni kwa uamuzi ule wa kugomea kuagiza sukari kutoka nchini Uganda, au auamuzi wa kugomea kuagiza bidhaa zozote kwa nia njema na lengo zuri la kulinda viwanda vya ndani, uamuzi kuhusu sukuri, haukutolewa na Waziri Prof. Mkenda kusema ni uamuzi wake binafsi, pia nilimsikia Waziri Mkuu, Majaliwa Kassin Majaliwa akiuzungumza. Huu ni uamuzi wa Baraza la Mawaziri lililopita, hivyo kauli ya rais Samia haimlengi mtu, inalenga uamuzi wa kugomea kuagiza sukari ya jirani Uganda.

Sasa twende kwenye ukweli wenyewe wa alichokisema Rais Samia uamuzi ule kweli ni “nonsense”. Hii maana yake ni kile niliwahi kukisema katika makala zangu za nyuma, kuwa viongozi wetu sio malaika, ni binaadamu, hivyo wanaweza kabisa kufanya makosa na kutoa muuamuzi “nonsense”, kama bazara la mawaziri limeweza kupitisha uamuzi kama huo, hili la sukari ni uthibitisho tuu wa uwezokano seriali yetu kufanya maamuzi “nonsense”.

Tena nonsense kubwa kuliko ya sukari, sio kwa serikali yetu kugomea kuingiza nchini sukari ya jirani zetu wa Uganda, serikali yetu iligomea kuingiza Tanzania Bara sukari kutoka Zanzibar!. Wakati huku bara tuna uhaba wa sukari, sukari ilipanda bei kutoka shilingi 1,800 kwa kilo, hadi shilingi 2,500 kwa kilo. Kule Zanzibar bei ilibaki 1,500 hadi 2,000.

Kiwanda cha sukari Zanzibar, kilikuwa na sukari ya kutosheleza kabisa kumaliza upungufu wa sukari huku bara, hivyo kikaomba kuleta sukari yake Bara kukabili upungufu, haswa kwa kuzingatia bei ya huku Bara imechangamka kuliko bei ya Zanzibar, ilikataliwa.

Waziri wa Viwanda na Biashara wa Zanzibar, Amina Salum Ali, akavuka bahari, kuja bara kusemezana na waziri mwenzake…lakini wapi, alikataliwa!. Waziri Amina Salum Ali akaigeukia taasisi ya TradeMark East Afrika inayoshughulika na kuondoa vikwazo vya kibiashara visivyo vywa kikodi (non tariff barriers), na kukiripoti hicho kikwazo cha sukari.

Yaani Tanzania bara inakabiliwa na uhababa wa sukari, Zanzibar inayo sukari ya ziada bwelele, Zanzibar inakataliwa kuingiza sukari yake bara, na badala yake, wenye viwanda ndio wanaoruhusiwa kuagiza sukari ya bei chee kutoka ng’ambo, kufidia huo upungufu!, kwa uamuzi kama huu, ni neno gani zuri zaidi ya kulitumia zaidi ya neno “nonsense?”.

Nampungeza sana rais Samia kwa kukemea na kukomesha hii nonsense ya kwenye sukari, na sasa nitoe wito kwa rais wetu Mama Samia, hizi nonsense za kwenye sukari, zisiishie tuu kwenye sukari, tende na kwenye nonsense nyingine zote za uondoshaji wa vikwazo vya uingizaji nchini bidhaa muhimu ambza viwanda vya ndani vimeshindwa kutosheleza mahitaji ya bidhaa hizo.

Kwa sasa taifa linakabiliwa na upungufu wa sementi, mfuko wa sementi ya Tanzania kwa mikoa ya pembezoni, kama Arusha, na Moshi, imefikia bei ya shilingi 24,000 kwa mfuko. Sementi ya Kenya ni shilingi 12,000 kwa mfuko mpaka inafika dukani Tanzania. Watu wanahitaji sementi haipo, hapo kwa jirani yetu sementi bwelele, bei chee, lakini hairuhusiwi kuingia Tanzania, kwa lengo la kulinda viwanda vya ndani. Hii pia ni nonsense!. Hivyo baada yah ii nonsense ya sukari, twende kwenye nonse nyingine zote za vikwazo vya uingizaji bidhaa.

Angalizo: Kuunga mkono huu msimamo wa rais Samia kuondoa nonsense ya sukari, na kutaka nonsense nyingine zote ziondoshwe, namaanisha kufungua milango ya soko huria kwa zile bidhaa tuu za muhimu ambazo viwanda vyetu vya ndani, vimeshindwa kuzalisha kukidhi mahitaji ya kutosheleza soko la ndani, na sio soko holela. Viwanda vya ndani vikifanikiwa kuzalisha kutosheleza soko, tuendelee kuvilinda, hata kama ulizi huo utatuumiza sisi wananchi kulazimika kununua bidhaa zate zinazozalishwa nchini kwa bei kubwa, ndioko kujenga nchi kwenyewe na sio kukimbilia cheap imports kwasababu tuu ni cheap!.

Wasalaam.

Paskali.

Mtoa mada huna akili.
 
Kwa taarifa zilizopo, inasemekana kuwa kampuni zote za kikandarasi iwe ujenzi, umeme, nakadhalika zilizosajiliwa Tanzania bara zimeondolewa haki ya kuomba kazi Zanzibar kama kampuni zilizosajiliwa katika Jamhuri ya Muungano Tanzania. Kwa sasa kampuni hizi za kandarasi zinawekwa sawa kama kampuni zinazotoka nje ya Jamhuri ya Muungano Tanzania. Yaani kampuni hizi za Tanzania bara zinatozwa kodi sawa na kampuni za kifaransa, kichina, kituruki, kimisri nakadhalika!!! (Kama taarifa hizi siyo sahihi nitaomba nipewe taarifa sahihi)

Nadhani mambo kama haya ndiyo yanazidisha "nonsense"!
Kuna ukweli, rafiki yangu mmoja aliniambia inabidi waregiste upya kampuni yao Zanzibar ili waweze kufanya kazi Zanzibar an kulipa kodi zote Zanzibar Kampuni hii imafanyakazi Zanzibar kwa zaidi ya miaka 20. Ila hata mimi sijajua ni sawa na wageni au la.
 
Kwa taarifa zilizopo, inasemekana kuwa kampuni zote za kikandarasi iwe ujenzi, umeme, nakadhalika zilizosajiliwa Tanzania bara zimeondolewa haki ya kuomba kazi Zanzibar kama kampuni zilizosajiliwa katika Jamhuri ya Muungano Tanzania. Kwa sasa kampuni hizi za kandarasi zinawekwa sawa kama kampuni zinazotoka nje ya Jamhuri ya Muungano Tanzania. Yaani kampuni hizi za Tanzania bara zinatozwa kodi sawa na kampuni za kifaransa, kichina, kituruki, kimisri nakadhalika!!! (Kama taarifa hizi siyo sahihi nitaomba nipewe taarifa sahihi)

Nadhani mambo kama haya ndiyo yanazidisha "nonsense"!
Ni mwendo wa nonsense hadi kukuche
 
Kuna ukweli, rafiki yangu mmoja aliniambia inabidi waregiste upya kampuni yao Zanzibar ili waweze kufanya kazi Zanzibar an kulipa kodi zote Zanzibar Kampuni hii imafanyakazi Zanzibar kwa zaidi ya miaka 20. Ila hata mimi sijajua ni sawa na wageni au la.
Asante sana mkuu kwa kudhibitisha taarifa hizi.
=====
Sasa kama utaratibu ndiyo huo, "nonsense " ni muhimu mpaka Zanzibar ifuate utaratibu wakuingiza sukari Tanzania bara .
 
Ninafikiri kutugeuza soko la bidhaa za nje na wakati huohuo tunajinasibu na sera za kustawisha viwanda ndiyo nonsense kamili.
Kama hatuwezi ,ndo hatuwezi tuu.
Sukari ya Brazili ikiingia TZ baada ya kodi zote itasimama kwa T shs. 1600/= Dukani reja reja.
Hii NonSense ya serikali kuwakandmiza Raia kwa kisingizio cha kulinda Kiwanda cha Bepari fulani wala si cha serikali,huu ni upotolo na ni foolishness beyond nonsence.
 
tunajigamba kujenga Fly over kwa bei ghali sana ,inavyoonesha TZ hatuna uwezo kabisa wa kiutaalamu wa kubuni,kuchora na kujenga hayo ma fly over.
Lkini baya zaidi hata kuchagua aina ya fly over pia hatujui, matokeo yake tunajengaflyover za kizamani za miaka ya 70 na kuacah kwenda na wakati,
Mfugale

Mr. Alphayo J. Kidata
Commissioner General


Mfugale Flyover at the Junction of Nyerere and Mandela roads in Tazara Dar es Salaam, of which are the results of Tanzanian Taxes

hili ni aina ya zamani ya madraja.
msongamano umehama upande mmoja umehamia upande mwingine.
Bado foleni za Mandela road zipo pale pale.
 
Kama hatuwezi ,ndo hatuwezi tuu.
Sukari ya Brazili ikiingia TZ baada ya kodi zote itasimama kwa T shs. 1600/= Dukani reja reja.
Hii NonSense ya serikali kuwakandmiza Raia kwa kisingizio cha kulinda Kiwanda cha Bepari fulani wala si cha serikali,huu ni upotolo na ni foolishness beyond nonsence.
Kwahiyo kama hamwezi ndiyo muendelee kutokuweza milele bila kuchukua hatua za mabadiliko!
 
Sijajadili hoja yake

Nimeuliza kwanini jamaa ana changamoto kubwa ya kupuuzwa?

I wonder why?

Jamaa ana muda mwingi kwenye hiyo tasnia ila yeye akitoa maneno 1,000 halafu Jenerali Ulimwengu akatoa just neno 1,huyu kiazi anaonekana mavi matupu

Ajiulize sana aisee

Ni changamoto yake nimejaribu kuiweka wazi tu aishughulikie yeye binafsi maana ndio anahusika
Sawa mkuu twende kwenye hoja ya msingi yapi maoni yako kuhusu sukari ?
 
Ninafikiri kutugeuza soko la bidhaa za nje na wakati huohuo tunajinasibu na sera za kustawisha viwanda ndiyo nonsense kamili.
Pia wenye viwanda wana wajibu ya kuweka bei affordable kwa wanainchi ili kuweka ushindani uliyo sawa na mwananchi akaweza kununua kulingana na hali halisi ya uchumi,sio kutegemea kulindwa na sheria tu za local industries,eti kwa sababu viwanda visife,mbona finance management zao zipo more active kuhakilisha viwanda avifilisiki kwa nn wasitegemee tu kulindwa na sheria za serikari?
 
Pia wenye viwanda wana wajibu ya kuweka bei affordable kwa wanainchi ili kuweka ushindani uliyo sawa na mwananchi akaweza kununua kulingana na hali halisi ya uchumi,sio kutegemea kulindwa na sheria tu za local industries,eti kwa sababu viwanda visife,mbona finance management zao zipo more active kuhakilisha viwanda avifilisiki kwa nn wasitegemee tu kulindwa na sheria za serikari?
Mitaji ya wawekezaji wengi wa ndani hailingani na wawekezaji wa nje wengi.

Wao kama wanataka kutuuzia walipaswa waje wajenge viwanda vyao hapa nchini kama Marekani walivyofanya kwa China.

Hapo itakuwa na manufaa kwa pande zote. Otherwise, serikali inapaswa kulinda viwanda vya ndani.
 
Mitaji ya wawekezaji wengi wa ndani hailingani na wawekezaji wa nje wengi.

Wao kama wanataka kutuuzia walipaswa waje wajenge viwanda vyao hapa nchini kama Marekani walivyofanya kwa China.

Hapo itakuwa na manufaa kwa pande zote. Otherwise, serikali inapaswa kulinda viwanda vya ndani.
serikalikilinda viwanda , mwananchi ndiye anayeumia, wala hakuna nafuu kwa raia.
Basi kama serikali ikitaka kulinda viwanda itowe subsidize(fidia kwa pengo la bei) ili mwananchi apate bidhaa kwa bei rahisi
 
"Nonsense" si sawa na ujinga. Maana yake mara nyingi ni karibu sana na "ujinga" lakini si sawa. Mara kwa mara nonsense ni pia dalili ya ujanja, au njia ya kufikisha ujumbe kwa njia ya kifumbo.

Ukiangalia neno lina pande mbili "non" + "sense". Kwa hiyo kimsingi maana yake ni "bila maana".
Ufafanuzi mfupi wa Kiingereza ni:
" spoken or written words that have no meaning or make no sense."
Kutoka hapa pia: "foolish or unacceptable behaviour" (ambako tumekaribia ujinga)

Wikipedia:
Nonsense is a communication, via speech, writing, or any other symbolic system, that lacks any coherent meaning. Sometimes in ordinary usage, nonsense is synonymous with absurdity or the ridiculous. Many poets, novelists and songwriters have used nonsense in their works, often creating entire works using it for reasons ranging from pure comic amusement or satire, to illustrating a point about language or reasoning.
In the philosophy of language and philosophy of science, nonsense is distinguished from sense or meaningfulness, and attempts have been made to come up with a coherent and consistent method of distinguishing sense from nonsense.

Kuhusu tamko la rais nadhani alielewa sawa. Ila maelezo ya kilugha hayakuwa sahihi.
 
T
Pia wenye viwanda wana wajibu ya kuweka bei affordable kwa wanainchi ili kuweka ushindani uliyo sawa na mwananchi akaweza kununua kulingana na hali halisi ya uchumi,sio kutegemea kulindwa na sheria tu za local industries,eti kwa sababu viwanda visife,mbona finance management zao zipo more active kuhakilisha viwanda avifilisiki kwa nn wasitegemee tu kulindwa na sheria za serikari?
Wananchi turuhusiwe kutengeza sukari guru kama wahindi na Indonesia huko! Turuhusiwe muone kama sukari haishuki bei!
 
Kama hatuwezi ,ndo hatuwezi tuu.
Sukari ya Brazili ikiingia TZ baada ya kodi zote itasimama kwa T shs. 1600/= Dukani reja reja.
Hii NonSense ya serikali kuwakandmiza Raia kwa kisingizio cha kulinda Kiwanda cha Bepari fulani wala si cha serikali,huu ni upotolo na ni foolishness beyond nonsence.
Na wanakandamiza kwenye bidhaa zisizoisha fasheni kama sukari na cement kwanini?
 
tunajigamba kujenga Fly over kwa bei ghali sana ,inavyoonesha TZ hatuna uwezo kabisa wa kiutaalamu wa kubuni,kuchora na kujenga hayo ma fly over.
Lkini baya zaidi hata kuchagua aina ya fly over pia hatujui, matokeo yake tunajengaflyover za kizamani za miaka ya 70 na kuacah kwenda na wakati,
Mfugale

Mr. Alphayo J. Kidata
Commissioner General


Mfugale Flyover at the Junction of Nyerere and Mandela roads in Tazara Dar es Salaam, of which are the results of Tanzanian Taxes

hili ni aina ya zamani ya madraja.
msongamano umehama upande mmoja umehamia upande mwingine.
Bado foleni za Mandela road zipo pale pale.
Mpaka Raisi aseme twende na fasheni mpya ila wataalamu wao hawana maono.
 
Back
Top Bottom