Kwa nini Watu (Watz)Wanaamini sana BBC?

Samahani kama nitakosea,nisahihishwe. Unapozungumzia ulinganisho wa vyombo vya habari kuaminika au kutoaminika,ni lazima ujikite kwenye HABARI yenyewe kuambatanisha na facts (zenye kuthibitisha). Mfano : Wakati sakata la Tembo likiripotiwa na BBC,walitoa taarifa yenye vithibitisho vya kimaelezo. Ili chombo cha ndani kukanusha (TBC,IKULU) inapaswa waje the facts against siyo porojo. Ni katika mazingira hayo ndipo media kama BCC zinaaminika sana.

Generaly,vyombo vya umma kama TBC vimekua vya upande mmoja. Inatumika kutetea utawala na kusahau mantiki ya chombo cha umma. Uwepo wa private media umesaidia sana sana.

Kwa hiyo kwa taarifa hiyo ya BBC ndio umeamini kwa 100% kwamba walichokisema ni sahihi?
Yaani umeamini ya kwamba ni kweli Raisi/kiongozi wa Uchina alipakia Meno ya tembo kwenye ndege yake? Ni nini kimekufanya uamini hilo?
Ninaweza pia nikakupa mfano ni BBC hao hao waliotumiwa na Serikali ya Uingereza kusema ya kwamba Sadamu Huseni alikuwa Silaha za Nyuklia ili hali walijua ni Uongo na mpaka UN sasa wamethibitisha haikuwa kweli, sasa uaminifu wao unatoka wapi? kumbuka pia walionyesha vielelezo vyote kwamba Sadamu wana Silaha za Nyuklia!
 
hawa watu huwa hawatangazi hovyo kama vyombo vyetu,wanahakiki mambo,mpaka waandike kitu wamehakikisha,mfano angalia gazeti la uhuru leo imesema ccm imetisha kama tsunami ukawa waangukia pua halafu wameandika front page,hapo hata hajapata matokeo ya nchi nzima halafu uniambie niwaamini kwa pumba zao.

Lakini BBC pia wamedanganya Ulimwengu sana, na ndio maana kuna baadhi ya Nchi wamepigwa marufuku, rejea Vita ya Iraki, kila Mtu anajua sasa ulikuwa ni Uongo, sasa Hiyo imani yako kubwa kwao (BBC) inatoka wapi?
 
Nimekuwa nikijiuliza sana ni kwanini Watz wanakiamini sana hiki chombo cha Habari cha Nchi ya Uingereza BBC?
Yaani utakuta mtu anabishania kitu ukimuuliza atakwamba BBC wamesema, hata humu JF ukitaka hoja yako iaminiwe na kukubalika basi sema imetoka BBC unganisha na website ya BBC hapo utaaminika!

Lakini kama habari imetoka ITV, TBC au hata Star TV inayohusu nchi yetu hata tusema kuhusu tu Mitaa ya Manzese haitaaminika na utaambiwa ulete ushahidi ukileta wa BBC basi umeaminika, sasa ni kwa nini?

W
akati Dunia nzima inatambua ya kwamba BBC ni chombo cha Propaganda cha Serikali ya Uingereza hata Waingereza wenyewe ambao ndio walipa kodi hawakiamini sasa ni kwa nini sisi tunafikiri kila wanachosema kuhusu sisi ni sawa? kuna sababu yoyoyte ya Msingi?

Kuna mtu kapata Degree yake Uingereza na mwingine amepata degree yake UDSM , watu huwa wanamwamini nani???
 
Kuna mtu kapata Degree yake Uingereza na mwingine amepata degree yake UDSM , watu huwa wanamwamini nani???


Hilo ni swali lenye akili sana, angalau nimekutana na Mtu Intelligent! Nafikiri umemaliza Mjadala!
Nimekupata!
 
Back
Top Bottom