Kwa nini watu ambao hawajatoa hata Shilingi (KGR), wana kelele sana?

Barbarosa

JF-Expert Member
Apr 16, 2015
22,584
27,782
Tangu kutokea kwa tetemeko la ardhi huko Mkoani Kagera michango mingi sana imetolewa ya hali na mali, lkn kinachonishangaza waliotoa michango mingi ya mali kama fedha na vifaa vya ujenzi ambao wengi wao ni wageni kama Ofisi za Kibalozi, nchi jirani kama Uganda na Kenya hawalalamiki na wala hawajalalamika na kuhusu michango yao ilivyotumika na walisha move on!

Lkn watu ambao hawajatoa hata shilingi wala hata tu kujali maisha ya wana Kagera leo wanahoji matumizi ya misaada, watu ambao (chadema) kwanza walifurahia na kusherehekea kutokea kwa tetemeko na walikuwa wanasema Mungu kamuadhibu Raisi Magufuli, iweje leo hii wanajifanya ni wataalamu wa kuipangia Serikali jinsi ya kutumia misaada iliyotolewa na wasamalia wema ambao wao walisha-move on?
 
ukweli ni ukweli na uongo ni uongo we mama,haviingiliani hivi vitu.tunajua mlichofanya hakuna haja ya Maelezo mengi kila siku mnaumiza watu tu kwa kuwakumbusha ushetani wenu......
 
Sawa mawazo yako ila tambua kuthamini binadam wenzako ni mhimu


Kwa nini ikuume wewe kuiliko aliyetoa fedha na mali? Mbona yeye halalamiki? Tumeona Balozi wa Uingereza akiwa na raisi Magufuli huko Kagera mbona yeye na nchi yake hawajalalamikia misaada yao kutumiwa kwenye Miundo mbinu yetu?
 
Nimeshangaa sana Nduli akiwalaumu wakazi wa Kagera eti ukimwi wao, tetemeko wao, mnyauko wa migomba wao....

Nduli Mungu anakuona.
 
Unapofikia kumuita binadamu mwenzako takataka kwa sababu yoyote ile ujue uwezo wako wa kufikiri uko kwenye "freezing point". Wewe umekuwa ukitoa mawazo humu tena mengine ya ovyo kuliko ovyo yenyewe mbona wenye hekima hawajawahi kukuita hivyo? Mods tenganisheni watu kama hawa na watu wenye busara kwa kuanzisha jukwaa la vichaa. Huko wataelezana mambo yao kihayawanihayawani, na hata wakigombana msiwaingilie. Tumechoka kukaa jukwaa moja na watu wasioheshimu wenzao kwa sababu tu ya tofauti ya mawazo. Wewe Mtanzania gani ukiamka matusi ukilala matusi? Mi siamini kama kweli wewe ni KE maana hakuna mwanaume anayeweza kuwa na hawala sampuli yako sembuse kuoa.
 
Kwa nini ikuume wewe kuiliko aliyetoa fedha na mali? Mbona yeye halalamiki? Tumeona Balozi wa Uingereza akiwa na raisi Magufuli huko Kagera mbona yeye na nchi yake hawajalalamikia misaada yao kutumiwa kwenye Miundo mbinu yetu?
Je unauhakika hatukutoa michango?
 
Kwa nini ikuume wewe kuiliko aliyetoa fedha na mali? Mbona yeye halalamiki? Tumeona Balozi wa Uingereza akiwa na raisi Magufuli huko Kagera mbona yeye na nchi yake hawajalalamikia misaada yao kutumiwa kwenye Miundo mbinu yetu?
Umejuaje kuwa hawakutoa? Kumbuka hata elfu moja ina thamani kubwa
 
Kwa nini ikuume wewe kuiliko aliyetoa fedha na mali? Mbona yeye halalamiki? Tumeona Balozi wa Uingereza akiwa na raisi Magufuli huko Kagera mbona yeye na nchi yake hawajalalamikia misaada yao kutumiwa kwenye Miundo mbinu yetu?
Unajuaje kama hawajatoa? Umeoneshwa na roho au? Acha unafiki na kujipendekeza. Na wanaojipendekeza always huwa si watu wazuri,kwahiyo hujipendekeza kutafuta ulinzi.
 
wahisani wakitoa hata wasipofuatilia zimetumikaje dhahabu watachukua tu,sasa sisi tukitoa tunataka kujua na jee zimesaidia watanzania wenzetu?
 
Unajuaje kama hawajatoa? Umeoneshwa na roho au? Acha unafiki na kujipendekeza. Na wanaojipendekeza always huwa si watu wazuri,kwahiyo hujipendekeza kutafuta ulinzi.


Kwa nini waliotoa hela nyingi na mali hawalalamiki fedha zao kutumiwa kwa ajili ya Miundo mbinu? Nchi kama Korea, Uganda , Kenya hata walituma malori yaliyojaa misaada, mbona kwao siyo ishu, ije kuwa ishu kwenu ninyi ambao hamjatoa chochote zaidi ya kukaa nyuma ya computer siku nzima kutafuta negativity?
 
Wewe mleta Uzi nikuulize, unafahamu maana ya msemo huu ..' Kama asiposema mwanadamu mawe yatasema' ..unaielewa vizuri maana yake? Katika kusaidia, aliyetoa kingi na yule aliyetoa kidogo kwa vile hana wote ni sawa mbele ya Manaani. Usimshushe aliyetoa mia kisa katoa kidogo ama ambaye hajatoa kwa vile hana na ukafikiri yule aliyetoa 10,000 ndo wa thamani ... Siku nyingine jifunze.
 
Tangu kutokea kwa tetemeko la ardhi huko Mkoani Kagera michango mingi sana imetolewa ya hali na mali, lkn kinachonishangaza waliotoa michango mingi ya mali kama fedha na vifaa vya ujenzi ambao wengi wao ni wageni kama Ofisi za Kibalozi, nchi jirani kama Uganda na Kenya hawalalamiki na wala hawajalalamika na kuhusu michango yao ilivyotumika na walisha move on!

Lkn watu ambao hawajatoa hata shilingi wala hata tu kujali maisha ya wana Kagera leo wanahoji matumizi ya misaada, watu ambao (chadema) kwanza walifurahia na kusherehekea kutokea kwa tetemeko na walikuwa wanasema Mungu kamuadhibu Raisi Magufuli, iweje leo hii wanajifanya ni wataalamu wa kuipangia Serikali jinsi ya kutumia misaada iliyotolewa na wasamalia wema ambao wao walisha-move on?
Kweli Mungu alitaka atuonyeshe aina ya rais tuliye naye. Ametuonyesha kwamba tuna rais chuki
 
Kweli Mungu alitaka atuonyeshe aina ya rais tuliye naye. Ametuonyesha kwamba tuna rais chuki


Na ndo TZ inajengwa sasa, hata Mababu zetu waliwaita Wazungu hivyo hivyo lkn Reli ilijengwa, br, mipango miji n.k hivyo siyo geni ni watu wavivu tu kama wewe ndo husema hivyo!
 
ni heri hao unaosema hawakutoa misaada lakini wanapiga kelele kuliko yule aliyepokea hiyo misaada halafu badala ya kuwafikishia walengwa anaitaifisha na kuipangia matumizi mengine na kisha kuwakejeli waathirika kuwa serikali siyo iliyoleta tetemeko.
 
1 Reactions
Reply
Back
Top Bottom