Kwanini Watanzania hamjiungi na ALIBABA small business website

mara wakaushie usiwajibu mara then unanijibu-unaniqoute.

Toka huu uz uanze hapa nimefanya majaribio kibao kuwasiliana na hao sellers na manufacturers ni kama nilikuwa natafiti nikaja kujua yafatayo:-

Alibaba ni B2B site hafifu sana na haina usalama kwa asilimia kubwa kama si kabisa, kwanza day 1 nili contact manufacturer mmoja tu kilichofata zilikuja e mail zaid ya 10 ya seller na manufacturers tofauti tofauti na quote za bidhaa zao, zikiwa zimegawanywa kutoka, simu, laptop, kamera, led tv mpka memory kadi.

Udhaifu wa kwanza hapo e mail yangu ime leak ovyo.

Pili katika wote hata niliporudia rudia hakuna aliekubali malipo ya escrow mnazosema wala Paypal.
Ispikuwa TT, moneygram na western union

Wakati huohuo, vitu vyao vyote vilionekana cheap kupita maelezo, unakuta laptop kakuondikia toshiba yenye specs za kuuzwa bongo lak 7 yeye anauza $ 95.

Samsung led tv 70" anauza us $ 175, 32" dola 100

Nikaanza kuwa na wasi wasi kutoka kwa bei izo, na iyo si kwa mmoja seller wote walinitumia ivo na nina e mail zaid ya 30 kutoka kwa seller mbalimbali tena waliokuwa verified na rated lakn ndo hao wasio nihakikishia usalama.

Kitu kingine baada ya kujisajili hii web yenyewe ya Alibaba walikiwa wananitumia e mail ile za news n.k
Wakielezea labda way inafanya kazi hii web yao na waki suggest sellers lakn none of them hata pale juu akionesha anakubali escrow ukianza wasiliana nae anakwambia haikubali.

Worse enough ni hivi izo news letter zenyewe za alibaba hazitoi onyo wala kusisitiza wanunuzi wasitume pesa kwa njia zisizo salama.

Kwa mf unapo ingia kwenye web zinazokusanya sellers kama Tradrcarview ya japan, unapokea warning na alert nying za usalama wa pesa yako kama vile kutumia paypal tu.

Lakn hawa alibaba sikuona hata caution moja ya kuelezea kutumia iyo mnayodai ni escrow.

Sasa what i came to conferm wadau this is a worse B2B website for ur money safety, kwa utafiti wangu.

Kama kuna seller mzuri naomba watetezi wa alibaba mniunganishe nae nami ni trade nae otherwise. FAKE
 
ndugu huwa unajifanya unajua sana na kumbe hujui chochote, na una maneno ya dharau!

kama niliwahi ibiwa alibaba.com ulitaka nikae kimya??

mawazo yangu ya kutoiamini alibaba.com ni lazima uyabebe kama wewe umeamua kuiamini??

huu ni uzi wa pili kuhusu alibaba na nimeona wadau kadhaa kama watano nao wakisema walishawahi ibiwa ndani ya alibaba, hivyo wote ni waongo? hao wote hawajahi nunua hata mswaki ndani ya alibaba??

au umetumwa na mmliki wa ailbaba???

Aliyesema mimi najua ni wewe, sijawahi kukwambia kwamba mimi najua kwa sababu najua kwamba nachojua ni kidogo mno katika hii dunia, ni kama punje moja ndogo sana ya mchanga katika mchanga wa jangwani.

Wewe unayejua unaona ni sahihi kusema "alibaba wezi tu" kwa sababu watu kadhaa waliibiwa? watu wanafanya biashara na maisha yanaendelea, kuibiwa kupo tu, hata ebay, amazon, sijui newegg watu wanaibiwa tu, mwizi hazuiliki, haina maana kudiscredit kampuni nzima ya alibaba kwa sababu uliibiwa na muuzaji mmoja! Muhimu kuwa makini wakati wa manunuzi.

Alibaba ni kampuni kubwa mno ndugu yangu hata wao wanakumbana na hizo challenge za wezi na hawazifurahii, ndiyo maana wanazidi kuanzisha mbinu za kupunguza au kukomesha wizi, ndiyo maana kwa sasa si ebay wala amazon wanaikaribia alibaba kwa mauzo, na next year wanaanzisha site ambayo itakuwa based US.

Sisi kuidiscredit based on a few cases wakati watu wanapiga biashara tutakuwa tunajinyima fursa sisi, si wao kuwanyima fursa! btw, hatushindani, tunaeleweshana!
 
Aliyesema mimi najua ni wewe, sijawahi kukwambia kwamba mimi najua kwa sababu najua kwamba nachojua ni kidogo mno katika hii dunia, ni kama punje moja ndogo sana ya mchanga katika mchanga wa jangwani. Wewe unayejua unaona ni sahihi kusema "alibaba wezi tu" kwa sababu watu kadhaa waliibiwa? watu wanafanya biashara na maisha yanaendelea, kuibiwa kupo tu, hata ebay, amazon, sijui newegg watu wanaibiwa tu, mwizi hazuiliki, haina maana kudiscredit kampuni nzima ya alibaba kwa sababu uliibiwa na muuzaji mmoja! Muhimu kuwa makini wakati wa manunuzi. Alibaba ni kampuni kubwa mno ndugu yangu hata wao wanakumbana na hizo challenge za wezi na hawazifurahii, ndiyo maana wanazidi kuanzisha mbinu za kupunguza au kukomesha wizi, ndiyo maana kwa sasa si ebay wala amazon wanaikaribia alibaba kwa mauzo, na next year wanaanzisha site ambayo itakuwa based US. sisi kuidiscredit based on a few cases wakati watu wanapiga biashara tutakuwa tunajinyima fursa sisi, si wao kuwanyima fursa! btw, hatushindani, tunaeleweshana!

Mkuu nimekutumia pm mbona kimya.
 
Wapo wengi sana na makampuni mengi wanatumia hasa ya export na wano import ni wengi uwezi jua watu wanatumiaje but if u have a dill ndipo utakapokutana na watu huko from tz.... na pia kuna mitandao mingi ya kufanya biashara more thana alibaba ... kuna kama trade key,dragon na mingine mingi so tupo ila sana
kwa kuwasaidia,tumieni mtandao wa paypal pale munapofanya malipo,inapotokea hitilafu yoyote, kama umeibiwa unawaliana na paypal wanakurudishia pesa wako.

Mimi ninatumia paypal kwa muda sasa,na nishapata Matatizo ya kuibiwa au kudqnganywa, au mzigo kuishia njiani na kuibiwa na post. Pesa zangu hurudishiwa na paypal pale ninapofanya claim.

Nilikuwa natumia mtandao kama ioffer, wanauza reja reja na jumla.
 
kwa kuwasaidia,tumieni mtandao wa paypal pale munapofanya malipo,inapotokea hitilafu yoyote, kama umeibiwa unawaliana na paypal wanakurudishia pesa wako.

Mimi ninatumia paypal kwa muda sasa,na nishapata Matatizo ya kuibiwa au kudqnganywa, au mzigo kuishia njiani na kuibiwa na post. Pesa zangu hurudishiwa na paypal pale ninapofanya claim.

Nilikuwa natumia mtandao kama ioffer, wanauza reja reja na jumla.

Asante mkuu
 
Kwa wale wazoefu wa alibaba. Unakuta katika Freight on Board (FOB ) price wanaweka in form of range.

Kwa mfano inakuwa hivi. FOB $33- $100. Hapa wanakuwa wanamaanisha nini.? Nataka kufanya bishara kupitia alibaba sasa.
 
mkuu nimekutumia pm mbona kimya

Mkuu pm yako niliiona, nikaanza kuijibu umeme ukakatika siku hiyo wakati nimeshaandika palagraph kadhaa nikakasrika, sasa nimerudi kutoka likizo ya shamba nikikaa ndani nitakuandikia kwa kirefu mkuu ondoa shaka.
 
Mimi mwenyewe nilikuwa najiuliza sana unakuta saa imeandikwa dola 1-40 hii inamaanisha nini????
 
www.Alibaba .com .kwenye search engine type biashara yoyote unavyotaka Kama " women clothes or containers or mobile houses .Wafanya biashara kibao watajitikeza hapo register na Anza kuwasiliana .I feel safe and secure sasa Hivi Yaani mpaka kiwandani unaenda unaona bidhaa na kununua Kama ni china India USA .nimeamua kuwashtua mliolala usingizi .

Akhsante mkuu, yaani sisi wengine tuko usingizine hasa.
 
Ni kweli mkuu,TRA wana urasimu sana tu,sijui ni kutojua au kukomoana tu,sometime naonaga kama kuna option ya kodi kulipiwa kule na wewe kufika hapa ni kusign na kuchukua mzigo tu,uwa ni nzuri zaidi
Unafanyaje ili ulipie ushuru wakati wa kununua Mkuu?
 
mkuu pm yako niliiona, nikaanza kuijibu umeme ukakatika siku hiyo wakati nimeshaandika palagraph kadhaa nikakasrika, sasa nimerudi kutoka likizo ya shamba nikikaa ndani nitakuandikia kwa kirefu mkuu ondoa shaka
Namimi naitaji msaada wako my no 0653441748,nitumie msg nitakupigia
 
Mkuu hilo ulisemalo sio kweli kabisa.
Usije ukawaponza waTz hapa.

ALIBABA.COM Hawatoi Guarantee yyt kwa Washiriki waliomo humo na makampuni mengi yaliomo humo ALIBABA.COM hayakubali PAYPAL as a source of payments.
Kwa sababu PAYPAL inakuhakikishua Usalama wa Pesa zako.
Wengi wao wanataka utume pesa kwa Moneygram au Western Union.

Na njia hizi zote HAKUNA USALAMA WAPESA ZAKO.

Ukiwaambia utume kwa (LOC) kupitia benki yako ASILIMIA 90% ya makampuni hayo WANAKATAA.

WIZI WENGI MNO kupita WAAMINIFU.
Mwenye kutaka bidhaa CHINA ni bora mara milioni upoteze hio NAULI uende mwenyewe.
mkuu kwenye alibaba kuna ALIBABA TRADE ASSURANCE na pendelea kununua kupitia GOLD SUPPLIERS kuliko suplliers wa kawaida. Pia fanya malipo na mawasiliano yote NDANI ya alibaba na sio nje .

Bank payment lupia kwenye akaunti ya kampuni na sio private account na hakikisha kuwa bidhaa unayonunua inalindwa na Trade assurance.

Alibaba is SAFE isipokuwa wengi hawapendi kufuata utaratibu ndio mana wanalizwa.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Stori ni ndefu mno.
Kwa kifupi nimekuja washtukia kwenye malipo.
Tumeshakubaliana bei na kila kitu mwisho kwenye kutuma malipo mimi nilihimiza aidha kutumia Paypal au (Lc) letter of Credit kipitia benki yangu, jamaa wanahimiza Western Union yaani utafikiri namtumia shangazi hela ya Sikukuu!

Kuwauliza sababu ya Kukataa hizi njia Ambazo zinakubalika Ulimwenguni kote eti wanasema Pesa inachelewa!
Pumbaff kabisa.

Wizi hawa mi nakwambia.
Na km ukipata muaminifu basi ni mmoja kati ya milioni.
mkuu hii peke yake sio sababu ya kuhalalisha kuwaita "matapeli". Hata ebay si kila muuzaji anakubali paypal. Na nikujuze tu kwamba njia zilizo salama sio paypal peke yake. Unaweza hata kulipa kwa Wiretransfer/western union na bado ikawa ni safe way IKIWA TU account unayolipa/bidhaa unayolipia inalindwa na Alibaba trade assurance. ukilipa nje ya akaunti hiyo utalizwa

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Back
Top Bottom