Rutashubanyuma
JF-Expert Member
- Sep 24, 2010
- 219,470
- 911,173
unapoona wanasiasa wengi wanafukuzia PHDs za heshima (Honoury Doctorates) ndani na nje ya nchi ni wakati mwafaka tukaanza kujiuliza ni msukumo upi unaowatuma wajidhalilishe heshima zao (kama zipo) mbele ya jamii kwa kujivika vilemba vya ukoka...............................................??????????????????????
baadhi ya misukumo walionayo ni pamoja na:-
a) kukidhi mahitaji yao binafsi ya elimu bandia baada ya kubaini ya kuwa hawana uwezo wa kukaa darasani na kuipata kihalali.............hivyo kuinunua inakuwa ni jibu la kutimiza ndoto zao ghiliba............hawa ni wa kuwaogopa kwa kuwa maisha yao yote hutegemea kudhulumu kwa kuchakachua haki za wenzao..........
b) kiu yao ya elimu tajwa ni kuiitishia jamii kuwa wamesoma na hivyo wana kiona mbali na kutarajia jamii itawaogopa na kukaa kimya kuvumilia faulo nyingi wanazozicheza dhidi yetu...................wakisahau kuwa jamii itawapima siyo kwa makabrasha wanayotudobosha nayo bali kwa huduma wanazozitoa kwa jamii wanayoishi..............na faulo za hapa na pale siyo huduma stahiki ambayo jamii inatarajia kwa viongozi wao wawe na PHD feki au la..........................
c) viongozi wengi wa nchi masikini kama hii yetu huabudu makaratasi lakini wenzetu wa nchi zilizoendelea huona hata aibu kuzungumzia elimu yao kwenye nafasi za umma kwa sababu hujua kazi ya siasa ni kutimiza wajibu uliopo mbele yao tu na wala siyo kujivunia sifa zilizopo kwenye makaratasi..............uhalali wao wanasiasa tajwa ni kuhudumia jamii tu na wala siyo uhalali huo kupatikana katika sifa ziliopo kwenye makaratasi tajwa............mfano Condoleesa Rice alikuwa ni profesa wa Russian studies na profesa kabla ya kuwa kwenye serikali ya Bush lakini kamwe akiwa waziri wa marekani hakuwahi kuitwa kwa uprofesa wake au udaktari wake................lakini kwetu huku kwa wanasiasa uchwara na wababaishaji uprofesa na udaktari hutukuzwa sana kama sifa za uongozi bora!!!!!!!!!!!!!
d) wengi wa wanasiasa wenye PHD tata utawakuta ni waathirika wa kisaikolojia kwa sababu wanajuafika utendaji wao ni goigoi lakini hupata msukumo wa kutafuta sifa bandia ili kutuhadaa kuwa wako imara wakati ni la hasha.............................angallia PHD tata na utaona utendaji wake ni bomu tupu....................
e) upo uhusiano wa moja kwa moja kati ya uteuzi wa senati na mabaraza ya vyuo vikuu vyetu haswa vinavyomilikiwa na serikali pamoja na upeanaji wa PHDs bandia............................wengi ya wajumbe wa senati za vyuo vikuu tajwa hawana sifa za kuwa wajumbe wa taasisi tajwa na namna ya kushukuru nao kuvikwa vilemba vya ukoka huamua kwa makusudi mazima kuwavika wababe wao serikalini vilemba tajwa..............................na ndiyo maana siyo rahisi kuona chuo kikuu cha serikali kumpa PHD ya heshima raia yeyote yule ambaye si waziri au raisi...ambaye anastahili kupewa heshima tajwa kwenye mchango wake kwenye jamii.........na wastaafu wa uwaziri na uraisi katika nyadhifa tajwa.............................kamchezo haka kanashusha hadhi za vyuo vikuu vya serikali kwa kuonyesha kumbe taasisi tajwa ndiyo chimbuko la kuanguka kwa maadili ya jamii.......
f) kwa kuelewa wanasiasa tajwa hawana sifa vyuo vikuu aidha hushindwa kutoa maelezo ya kuhalalisha vigezo walivyovitumia kumbeba mwanasiasa tajwa na alilinganishwa na akina nani katika tanuru la kutenda haki...........................na hivyo senate tajwa huishia kutoa maelezo ya kiujumla tu................................nchi ya namna hii kama yetu ambayo wasomi wake kwenye vyuo vikuu wanawaabudu wanasiasa haiwezi kuwa na nuru ya maendeleo na itaishia kujitetea kuwa "kwas sabau zisizoweza kuzuilika wameshindwa kuleta maendeleo.............................."
g) wengi ya wanasiasa uchwara tajwa utakuta hii laana ya kujitafutia vitu kwa wizi na udanganyifu tayari wamewaambukiza hata watoto wao.......................matokeo yake watoto wao hujikuta wakiletewa mitihani ya wizi na wazazi wao ili waonekane na jamii kuwa wanauwezo mkubwa wa darasani jambo ambalo siyo kweli....................................uwezo bandia wa darasani unakuwa ni kigezo cha kupata nafasi za elimu ya juu na nyadhifa serikalini na makampuni binafsi.........................................huku watoto wa hoehae wakibidiishwa kujiajiri tu..........
baadhi ya hawa wanasiasa babaishi ni pamoja na...............................................ninawaachia mjazilize wenyewe...............
baadhi ya misukumo walionayo ni pamoja na:-
a) kukidhi mahitaji yao binafsi ya elimu bandia baada ya kubaini ya kuwa hawana uwezo wa kukaa darasani na kuipata kihalali.............hivyo kuinunua inakuwa ni jibu la kutimiza ndoto zao ghiliba............hawa ni wa kuwaogopa kwa kuwa maisha yao yote hutegemea kudhulumu kwa kuchakachua haki za wenzao..........
b) kiu yao ya elimu tajwa ni kuiitishia jamii kuwa wamesoma na hivyo wana kiona mbali na kutarajia jamii itawaogopa na kukaa kimya kuvumilia faulo nyingi wanazozicheza dhidi yetu...................wakisahau kuwa jamii itawapima siyo kwa makabrasha wanayotudobosha nayo bali kwa huduma wanazozitoa kwa jamii wanayoishi..............na faulo za hapa na pale siyo huduma stahiki ambayo jamii inatarajia kwa viongozi wao wawe na PHD feki au la..........................
c) viongozi wengi wa nchi masikini kama hii yetu huabudu makaratasi lakini wenzetu wa nchi zilizoendelea huona hata aibu kuzungumzia elimu yao kwenye nafasi za umma kwa sababu hujua kazi ya siasa ni kutimiza wajibu uliopo mbele yao tu na wala siyo kujivunia sifa zilizopo kwenye makaratasi..............uhalali wao wanasiasa tajwa ni kuhudumia jamii tu na wala siyo uhalali huo kupatikana katika sifa ziliopo kwenye makaratasi tajwa............mfano Condoleesa Rice alikuwa ni profesa wa Russian studies na profesa kabla ya kuwa kwenye serikali ya Bush lakini kamwe akiwa waziri wa marekani hakuwahi kuitwa kwa uprofesa wake au udaktari wake................lakini kwetu huku kwa wanasiasa uchwara na wababaishaji uprofesa na udaktari hutukuzwa sana kama sifa za uongozi bora!!!!!!!!!!!!!
d) wengi wa wanasiasa wenye PHD tata utawakuta ni waathirika wa kisaikolojia kwa sababu wanajuafika utendaji wao ni goigoi lakini hupata msukumo wa kutafuta sifa bandia ili kutuhadaa kuwa wako imara wakati ni la hasha.............................angallia PHD tata na utaona utendaji wake ni bomu tupu....................
e) upo uhusiano wa moja kwa moja kati ya uteuzi wa senati na mabaraza ya vyuo vikuu vyetu haswa vinavyomilikiwa na serikali pamoja na upeanaji wa PHDs bandia............................wengi ya wajumbe wa senati za vyuo vikuu tajwa hawana sifa za kuwa wajumbe wa taasisi tajwa na namna ya kushukuru nao kuvikwa vilemba vya ukoka huamua kwa makusudi mazima kuwavika wababe wao serikalini vilemba tajwa..............................na ndiyo maana siyo rahisi kuona chuo kikuu cha serikali kumpa PHD ya heshima raia yeyote yule ambaye si waziri au raisi...ambaye anastahili kupewa heshima tajwa kwenye mchango wake kwenye jamii.........na wastaafu wa uwaziri na uraisi katika nyadhifa tajwa.............................kamchezo haka kanashusha hadhi za vyuo vikuu vya serikali kwa kuonyesha kumbe taasisi tajwa ndiyo chimbuko la kuanguka kwa maadili ya jamii.......
f) kwa kuelewa wanasiasa tajwa hawana sifa vyuo vikuu aidha hushindwa kutoa maelezo ya kuhalalisha vigezo walivyovitumia kumbeba mwanasiasa tajwa na alilinganishwa na akina nani katika tanuru la kutenda haki...........................na hivyo senate tajwa huishia kutoa maelezo ya kiujumla tu................................nchi ya namna hii kama yetu ambayo wasomi wake kwenye vyuo vikuu wanawaabudu wanasiasa haiwezi kuwa na nuru ya maendeleo na itaishia kujitetea kuwa "kwas sabau zisizoweza kuzuilika wameshindwa kuleta maendeleo.............................."
g) wengi ya wanasiasa uchwara tajwa utakuta hii laana ya kujitafutia vitu kwa wizi na udanganyifu tayari wamewaambukiza hata watoto wao.......................matokeo yake watoto wao hujikuta wakiletewa mitihani ya wizi na wazazi wao ili waonekane na jamii kuwa wanauwezo mkubwa wa darasani jambo ambalo siyo kweli....................................uwezo bandia wa darasani unakuwa ni kigezo cha kupata nafasi za elimu ya juu na nyadhifa serikalini na makampuni binafsi.........................................huku watoto wa hoehae wakibidiishwa kujiajiri tu..........
baadhi ya hawa wanasiasa babaishi ni pamoja na...............................................ninawaachia mjazilize wenyewe...............