Kwanini Wanajeshi wa Tanzania wanashambuliwa DRC?

Jeshi halikwenda kule kufuata pesa,Kusudio kuu ni kulinda amani,hata hivyo mambo mengi wanayojifunza kinadharia wanatakiwa wakayafanye kwenye medani.Hivyo pindi matukio kama ya kulinda amani nchi inaamua kupeleka wanajeshi wake wawe na uzoefu wa kutosha wa matukio halisi.Jeshi bora ni lile lenye uzoefu na ambalo limeshashikiri kwenye mapambano mengi.
Hapa umeongea point jeshi lisiloshiriki matukio kama haya ya kulinda amani nje ya mipaka yake linakuwa ni jeshi legelege.Jeshi letu lina sifa ya kuwa moja ya majeshi bora Afrika.Sababu kubwa constantly vijana wako kwenye mazoezi.Hii haikuanza leo toka enzi za baba wa taifa Nyerere.Nchi za kusini mwa Afrika uhuru wake haukupatikana bila mkono wa Tanzania.
Seycheles,Comoro,Uganda,Msumbiji,Angola,Namibia,RSA,Liberia,Congo,Sudan kote huko askari wetu walishiriki.
Mimi siafiki kutoa majeshi yetu huko ni kukubali kushindwa na kumpa adui kicheko cha ushindi.Matokeo yake tutatiwa vidole machoni watakuja kwetu kutuvamia ndani ya mipaka yetu.
Cha kufanya ni kubadili mbinu na kuziboresha tulipokosea tusahihishe.
Kwa masikitiko makubwa tumepoteza vijana wetu shupavu mungu awalaze pema peponi na kuwapa pole familia zao.
 
hao walikuwa walinzi wa amani ambao mpaka uwachokoze ndo wanajihami,wapo kule kwa ajili ya kuhakikisha maridhiano yanapatikana na kulinda raia.Nakuomba usipotoshe umma na itikadi zako za kisiasa;jeshi halipo kisiasa,wala urafiki wa mtu na mtu;kwani awamu ya JK;Hakuna walinzi wetu wa amani walio kufa huko kongo,sudani;lebanoni n.k.

Walikufa Congo wakati jeshi likiwa vitani, Tulipigana vita hasa, Tanzania na Malawi tulikuwa na Jeshi la Miguu na RSA wakiwa na Airbrne

Sasa tunapigana na nani?, tupo kuangalia Amani kama yalivyo majeshi ya Pakistan, India nk, Swali kwa nini tuvamiwe kwenye Camp yetu?, kwa nini camp za majeshi mengine hazivamiwi?
 
Mimi bado naamini Rwanda wanafanya kila njia kuhakikisha majeshi yetu yanaondoka Kongo.Baada ya M23 kufurumshwa yale majeshi ya Rwanda kwa mgongo wa M23 bila shaka wanatumia waasi wengine lakini kwa minajili ya kulipiza kisasi.maana bila jeshi letu Rwanda bado wangekuwa Kongo kuvuna rasilimali za huko.Tuwe macho na Rwanda si watu wazuri hata kidogo kwenye ukanda huu.

Mkuu umeongea kitu makini sana.
 
Subiri zamu yenu, na mkitwangana huko kwenu msije mkakimbilia kwetu, hatutaki wavamizi!

Mtasubiri sana tunawasubiri nyie mzabuliwe mje kupiga Magoti ya msaada wa kijeshi kwa King of Kigali The man himself ye ndo aliemweka Kabila baba Pale James kabarebe Anaijua Kongo kuliko nyie na alikua Chief of Staff wa ikulu ya Kongo mtuacheee ndo mana tunawachora pale DRC kesi sio yenu
 
Mtasubiri sana tunawasubiri nyie mzabuliwe mje kupiga Magoti ya msaada wa kijeshi kwa King of Kigali The man himself ye ndo aliemweka Kabila baba Pale James kabarebe Anaijua Kongo kuliko nyie na alikua Chief of Staff wa ikulu ya Kongo mtuacheee ndo mana tunawachora pale DRC kesi sio yenu


umawatusi wakunga wakati una mimba.

Dera bila chura ni kanzu tuu.
 
Kiusalama kuna sababu ya watanzania kukubali kuwa DRC Congo. Tufikirie kwa mapana tatizo liko wapi. Tukitafuta njia ya mkato lazima tutakimbia siku wakihamia huku
 
Back
Top Bottom