Kwa nini Wahehe na Tanzania nzima hatumuenzi Mkwawa ipasavyo?

mnyikungu

JF-Expert Member
Jul 26, 2009
1,960
2,464
wandugu, MKWAWA ni mtu mhimu sana kama alama ya ushujaa wakweli na utetezi wa mwafrika dhidi ya ukoloni, mtu huyu enzi zake aliogopwa mno. utawala wake ni moja kati ya tawala pekee zilizopigana na mjerumani na kumshinda.aliwafanya wahehe wajurikane kama the most powerful military people in German East Africa.ni mtu huyu pekee africa aliyekataa kulipa kodi kwa mkoloni na badala yake ni yeye ndiye aliyetaka alipwe kodi na wajerumani.najua hstoria yetu imeandikwa na wazungu na ndiyo maana vitabu vyetu vya historia havimuelezei kiundani mtu huyu kwani ni aibu kwao, ni huyu ambaye kifo chake kimejaa utata, wajerumani wanaamini alijiua na wao walimkata kichwa japo wengi hatuamini hivyo, fikra kubwa aliyokuwa nayo ni kwamba hata baada ya kifo chake hakupenda maiti yake iguswe na wazungu hivyo alikoka moto na kujipiga risasi mwili wake ukaangukia kwenye moto na kuteketea kabisa, hivyo hata kama walipata kichwa basi hakikuwa chake ila cha moja kati ya wafuasi wake. hiyo ni moja kati ya dhana zinazobishaniwa uheheni kwani wengine wanaamini alijidumbukiza mto kikombo na kupotea na wengine wanaamin aliendakujificha mapangoni na kufia huko. huyu mtu ni shujaa kweli! lakini kinachonishangaza mtu huyu kamwe haenziwi ipasavyo, wahehe wa leo utadhani hakuwa chifu wao na tanzania pia nayo imemsahau mtu huyu, mi nafikiri vya kale ni dhahabu apewe heshima yake kama inavyostahili maana huyu ndiyo kioo cha ushujaa wetu. hebu ona alivyopambana nao
(Lt. Tettenborn believed that if it had not been for the death of a large number of Wahehe chiefs, Mkwawa incorrectly included, no one would have survived. Saving the main 'part of the baggage' is also incorrect, it was not saved. Zelewski had started with 13 Europeans, some 320 Askaris, 170 porters, machine guns, and field artillery. Of these ten Europeans, 256 Askaris, and 96 porters had been lost. The German defeat made a truly enormous impression and the Hehe had now gained reputation as the most powerful military people in German East Africa and the Schutztruppe was no longer in a position to continue attacking the Wahehe.) kwa jeshi lenye vifaa kama hili alilopigana nalo mkwawa na akalishinda je ni kweli hastahili heshima?
 
ni kweli kwanza nawalaumu sana wahehe hasa viongozi wao waliowahi kushika nyadhifa serikalini akiwemo marehem Adam Sapi Mkwawa kweli walishindwa kuorganize hata kupata kumbukumbu au siku maalum ya kumkumbuka huyu shujaa
 
Mie naona Mkwawa bado anakumbukwa kwa namna yake kupitia kwenye historia. Maana ukienda Tabora na sehem nyingine wapo Machifu waliofanya vyema. Tukianzisha namna ya kumuenzi, itakuwa ni kutengeza chaka lingine la ufisadi.
Kama ipo haja saana ya kufanya hivyo, basi ifanyike harambee na kufanya mradi mkubwa kwa ajili yake ila watu wa serikalini wasiusishwe na pesa zao maana bili zao huwa ni kubwa saana.
Mapesa matalam!!!
 
Kalenga, ilipokuwa ngome yake Mkwawa kuna Museum ya kumbukumbu ya Mkwawa kikiwepo na kichwa chake (kama ni chake au siyo hiyo mie sijui). Nimefika pale. Kuna information ya kutosha kuhusu Mkwawa na utamaduni wa wahehe kwa ujumla. Museum hiyo iko chini ya Idara ya Kumbukumbu za Taifa lakini hawajafanya jitihada za kutosha kui-promote ili ijulikane zaidi. Inayo potential ya kuwa tourist attraction. Jambo lingine ni kwamba pamoja na marehemu Adam Sapi bado wapo vizazi vya Mkwawa ambao ni hai lakini hawaonyeshi kujivunia jina hilo, ukoo wao pamoja na utamaduni wa Kihehe kwa ujumla. Lakini kwa ujumla ndugu zetu wahehe bado wamelala. Vijana wa kiume wame-specialize katika ukorokoroni (security guards) na wasichana u-hausigeli. Waliosoma hawataki kurudi huko.
 
ni kweli kwanza nawalaumu sana wahehe hasa viongozi wao waliowahi kushika nyadhifa serikalini akiwemo marehem Adam Sapi Mkwawa kweli walishindwa kuorganize hata kupata kumbukumbu au siku maalum ya kumkumbuka huyu shujaa
huyu mtu ni mmja wa watu ambao mi nawaita wapuuzi sana kwenye jamii ya kihehe, iringa hatunalolote la kujivunia juu ya mtu huyu, ni kweli kuna viongozi wengi mno wa uheheni waliopo selikalini lakini hawaoni umuhimu wa jambo hili ila wanataka waenziwe wao kwa ujinga wao na kuacha kuwaenzi mashujaa waliopita.tatizo tulilonalo kwa selikali yetu ni kwamba hawajui kama harakati za kuiletea uhurutanganyika zilianzia kwa watu kama mkwawa, wao wanachojua ni tanu tu ndo ilileta uhuru na ni nyerer tu ndo alipigania uhuru.
 
Mie naona Mkwawa bado anakumbukwa kwa namna yake kupitia kwenye historia. Maana ukienda Tabora na sehem nyingine wapo Machifu waliofanya vyema. Tukianzisha namna ya kumuenzi, itakuwa ni kutengeza chaka lingine la ufisadi.
Kama ipo haja saana ya kufanya hivyo, basi ifanyike harambee na kufanya mradi mkubwa kwa ajili yake ila watu wa serikalini wasiusishwe na pesa zao maana bili zao huwa ni kubwa saana.
Mapesa matalam!!!
historia gani hiyo, maana kama ni darasani utafundiwa habari za zwangendaba zaidi kuliko za mkwawa. mtu huyu ni mhimu kuenziwa kwa namna ya pekee hata kama sio kwa NGGAZI YA TAIFA BASI KWA NGAZI YA MKOA KUWE NA SIKU MAALUM YA KUMKUMBUKA, KWA KUFANYA HIVYO TUTA ENFELEZA HITORIA KWA VIZAZI NA VIZAZI.
 
apa nilikua naangalia "website" ya mkwawa
kweli tumesahau kabisa hii historia muhimu sana
na ukiangalia kalenga haijaendelezwa/haijatangazwa kiivo
so watu wengi sana hawajui hii historia

miundombinu kalenga na ruaha imesahaulika sana
nyela vakuboma
 
watani zangu wahehe......si kweli kwamba hawamuenzi mkwawa......wanamuenzi kwa KU-COMMIT SUICIDE
 
mahesabu kweli una mahesabu,inawezekana ulicho andika kina ukweli.
Tufanyeni uchuguzi swala hili
 
Back
Top Bottom