Kwa nini Wahandisi Wetu wanaangusha Majengo.

ruzuku

Member
Sep 7, 2009
5
0
Nimeona nilete hii habari tuijadili wote wanajamii.Nilifurahi sana kwa kitendo cha kizalendo cha waziri wetu alipohutubia na kukerwa na kitendo cha Wahandisi wetu kuangusha Majengo.Mimi kutokana uewelewa wangu mdogo nilikuwa na machache ya kuongea.Fani ya uhandisi hapa nchini naona hatuko makini,naona siasa inaanza kuingizwa kwenye hii fani.Kwanza kuna Vyuo vingi vimeanzishwa hapa nchini kwa sasa vinavyotoa taaluma hii ya Uhandisi-shahada ya kwanza,hili ni jambo zuri kuongeza wahandisi nchini.Je bodi ya Wahandisi wameliona hilo?Kuna hizi shahada za Uhandisi shahada ya kwanza wanaziita Everning program nadhani na baadaye tutaanzisha shahada ya kwanza pale Muhimbili ya medicine everning program. Bodi ya uhandisi hapa nchini ina wasomi waliobobea kwenye hii fani.Wasipokuwa makini lawama za wahandisi kuangusha majengo zitawaelekea wao.Bodii waweke standard kupata wahandisi mahiri na si kwa sababu kaleta shahada yake sijui kutoka chuo gani halafu wewe unampa usajili hapohapo.Mimi naishia hapo,nakaribisha wachangia hoja karibuni.
 
Ungeanza kwa kuorodhesha majengo yaliyo anguka na wahandisi waliohusika na vyuo walivyopitia........
 
Tatizo tulilonalo kwetu ni uelewa kwa watu wa kawaida na ufisadi kwa watumishi wa umma.kwenye process za ujenzi zinahusisha watu wengi sana wakiwemo watu waliopewa dhamana na serikari kuangaalia shughuli za ujenzi.
Kama watu tunaelewa kweli ujenzi ni gharama kweli unaweza ukampa kazi mtu asiye na ujuzi bila kujali gharama na hasara zitakazo ingia baadaye.
Ujenzi unapoendelea ukaguzi unatakiwa kuwa unafanywa na watu waliohusika kwenye kubuni ujenzi huo kuamua kufisadi kwa kutoa approval wakiwa ofisini.
Binafsi sioni ubaya wa kuanzishwa kwa vyuo ikizingatiwa kwamba board ya wahandisi,wasanifu na wakadiriaji gharama za ujenzi hutaini watuwake nakuwapatia namba.
 
shida kubwa nayoiona kwa nchi hii,mtu anapopewa tender ya kujenga/kusimamia jengo amini usiamini kuna mlolongo wa walafi zaidi ya ishirini wanataka 10%,imagine unampa from waziri hadi mkurugenzi wa wilaya 10% huyu mjenzi yeye atabakiwa na faida gani?mahandisi analipwa sh ngapi kwa kazi ngumu namna hiyo?hivyo wanapunguza viwango hence poor work. Lakini nashauri au nasisitiza pia kwa wahandisi ile inayoitwa ETHIC hakuna kwa walio wengi,pia ratio ya huduma kwa mhandisi na population ni muhimu.nchi yetu ina jumla ya wahandisi 8000 tu all together, population ~40m, japan wapo wahandisi 2,400,000 population ~12m,unaweza kupata picha hapo ni namna gani tupo nyuma hii ikimaanisha ni katika fani zote,kama mhandisi akikosa elimu bora means waalimu bora wapo wachache,akikosa matibabu bora means Drs nao wapo wachache,so hii ni vicious circle!tupo interdependent so nchi hii ina kzi kubwa sana ya kufuatilia na kuaccomplish,inabidi tuvumbue kamodel maalum kwa nchi yetu,tukiiga kwa wenzetu hatutaweza hata kidogo.naamini walivyoibuka Uk si sawa na Germany,USA,Swiss etc,wote walikuwa na model zao.Finaly wote hawa wana sifa moja, waliheshimu na wanaheshimu fani ya uhandisi kwani ni ukweli usiopingika kuwa maendeleo ya nchi yoyote 90% yanategemea uhandisi,waza mwenyewe kwa unaeguna(infrasrtuctures,transportation,biomedical,agriculture,military) kila kitu!! thanks
 
shida kubwa nayoiona kwa nchi hii,mtu anapopewa tender ya kujenga/kusimamia jengo amini usiamini kuna mlolongo wa walafi zaidi ya ishirini wanataka 10%,imagine unampa from waziri hadi mkurugenzi wa wilaya 10% huyu mjenzi yeye atabakiwa na faida gani?mahandisi analipwa sh ngapi kwa kazi ngumu namna hiyo?hivyo wanapunguza viwango hence poor work. Lakini nashauri au nasisitiza pia kwa wahandisi ile inayoitwa ETHIC hakuna kwa walio wengi,pia ratio ya huduma kwa mhandisi na population ni muhimu.nchi yetu ina jumla ya wahandisi 8000 tu all together, population ~40m, japan wapo wahandisi 2,400,000 population ~12m,unaweza kupata picha hapo ni namna gani tupo nyuma hii ikimaanisha ni katika fani zote,kama mhandisi akikosa elimu bora means waalimu bora wapo wachache,akikosa matibabu bora means Drs nao wapo wachache,so hii ni vicious circle!tupo interdependent so nchi hii ina kzi kubwa sana ya kufuatilia na kuaccomplish,inabidi tuvumbue kamodel maalum kwa nchi yetu,tukiiga kwa wenzetu hatutaweza hata kidogo.naamini walivyoibuka Uk si sawa na Germany,USA,Swiss etc,wote walikuwa na model zao.Finaly wote hawa wana sifa moja, waliheshimu na wanaheshimu fani ya uhandisi kwani ni ukweli usiopingika kuwa maendeleo ya nchi yoyote 90% yanategemea uhandisi,waza mwenyewe kwa unaeguna(infrasrtuctures,transportation,biomedical,agriculture,military) kila kitu!! thanks
Kiasi nakubaliana na wewe kuhusu umuhimu wa kuwa na wahandisi wanaoweka maslahi ya Taifa mbele ili tuweze kupata maendeleo tunayokusudia.Ni ukweli pia kuna shortage ya wahandisi wa aina fulani fulani, mfano telecom engineers, water resources engineers, structural engineers na hata industrial and maintenance engineers.Kwa hali hiyo basi kuongezeka kwa idadi ya vyuo ni kitu cha kutia moyo ili kupata manufaa ya kuwa na watu hawa katika jamii zetu.
Panaponikera mimi ni suala zima la rushwa katika upatikanaji wa kazi za kihandisi. One of the papers presented during this year's engineers day ulizungumzia hili tatizo na gharama zake kwa taifa. Inatia aibu.
Zipo habari pia kuna baadhi ya registered engineers wanaouza mihuli yao kwa watu wasio competent wafanye kazi za kihandisi, kwa mfano, unaweza kuona jengo linajengwa, likionyesha kampuni au mtu fulani analisimamia wakati ukweli wa mambo hauko hivyo.
All in all, rushwa pia inaharibu umuhimu wa kazi za engineering na inawezekana ikawa sababu kubwa ya kuporomoka kwa majengo, kuharibika mapema kwa infrastructure kwasababu ya compromise ya viwango etc
 
Nimeona nilete hii habari tuijadili wote wanajamii.Nilifurahi sana kwa kitendo cha kizalendo cha waziri wetu alipohutubia na kukerwa na kitendo cha Wahandisi wetu kuangusha Majengo.Mimi kutokana uewelewa wangu mdogo nilikuwa na machache ya kuongea.Fani ya uhandisi hapa nchini naona hatuko makini,naona siasa inaanza kuingizwa kwenye hii fani.Kwanza kuna Vyuo vingi vimeanzishwa hapa nchini kwa sasa vinavyotoa taaluma hii ya Uhandisi-shahada ya kwanza,hili ni jambo zuri kuongeza wahandisi nchini.Je bodi ya Wahandisi wameliona hilo?Kuna hizi shahada za Uhandisi shahada ya kwanza wanaziita Everning program nadhani na baadaye tutaanzisha shahada ya kwanza pale Muhimbili ya medicine everning program. Bodi ya uhandisi hapa nchini ina wasomi waliobobea kwenye hii fani.Wasipokuwa makini lawama za wahandisi kuangusha majengo zitawaelekea wao.Bodii waweke standard kupata wahandisi mahiri na si kwa sababu kaleta shahada yake sijui kutoka chuo gani halafu wewe unampa usajili hapohapo.Mimi naishia hapo,nakaribisha wachangia hoja karibuni.

Everning programs za engineering - yaani kama zile za MBA etc.? Huu ni mchezo wa hatari mno. Sidhani unaweza kumpata engineer aliyeiva kupitia Everning programs. Labda ahudhurie Everning programs kwa miaka 10 au zaidi.
 
Lengo si kunyosheana vidole,Tujadili hasa chanzo ni nini cha kuanguka haya majengo?

Kama lengo si kunyosheana vidole, mbona heading umeandika wahandisi wanaangusha majengo? Nafikiri heading ingekuwa nini chanzo cha majengo kuanguka.

Kwa ufupi tu, majengo yote yanayoanguka si uzembe tu wa wahandisi. Kuna watu wamechukuwa majukumu ya uhandisi, kwa kukwepa gharama na kufanya mambo kiujanjaujanja , kiasi wana-compromise technical requirement na hivyo kusababisha majengo kuanguka. Kwa sababu kumekuwa na tabia ya kukwepa consulting fees, watu wanaamua kufanya vitu kwa jinsi wanavyoona wao inafaa, na matokeo yake ndio hayo tena.
 
Back
Top Bottom