Ritz
JF-Expert Member
- Jan 1, 2011
- 46,892
- 32,308
wanabodi,
imekuwa kama fasheni sasa kwa viongozi wa vyama vya upinzani chini kukutana na Rais Jakaya Kikwete Ikulu ya Dar es Salaam.
Wanaomba appointment Ikulu, wakisharuhusiwa wanakwenda kuzumgumza na Rais kisha wanapiga picha za pamoja na kuondoka, hapo tunaambiwa wanajadili sheria ya mabadiliko ya katiba.
Haya yalianzishwa na Chadema ambao walipinga muswada wa katiba mara mbili mwishoni mwa mwaka jana, chama hicho kilisusia mjadala wa katiba bungeni huku wabunge wake na wakiwemo baadhi ya wabunge wa NCCR Mageuzi, wakitoka nje ya ukumbi wa wabunge kuashria msimamo wao.
Baada ya bunge kumaliza mjadala wao, Chadema wakaomba kukutana na Rais Kikwete Ikulu, kujadili kile walichokuwa wakikipinga mkutano ukafanyika kwa muda wa siku mbili, walipomaliza Rais akausaini muswada waliokuwa wakiupinga Chadema ukawa sheria.
CUF nacho kikaomba appointment ya kumuona Rais, pamaja na kwamba chama hicho hakikususia mjadala wa shera ya mabadiliko ya katiba bado kikaenda kumuona Rais, sijui walimtaka Rais afanyaje wakati walishakubalina kila kitu bungeni.
NCCR Mageuzi nacho kikaomba appointment kwa Rais ili kutimiza wajibu wake, wamejadiliana walichojadili wakamaliza na kupiga picha na Rais Ikulu.
Mazungumzo ya Chadema yakajirudia safari hii na Slaa, nae alikuwepo, kitu cha kujiuliza hivi haya mazungumzo wananchi wameshilikishwa au na ni mawazo ya viongozi wa nyama vya siasa, tukumbuke kuwa kuna wananchi wasiokuwa na uanachama wa chama chochote, hao nao wanawakilishwa na nani Ikulu?
Kwa nini hivyo vikao vya katiba kama vinawakilisha mawazo ya wananchi visitangazwe moja kwa moja na televisheni ili angalau wananchi wasikie kilichojadiliwa? katiba hii sio ya Rais au vyama vya siasa, ni yetu sote.
Kwa nini wachache wajifungie Ikulu kujadili mustakabali wa maisha yetu???
imekuwa kama fasheni sasa kwa viongozi wa vyama vya upinzani chini kukutana na Rais Jakaya Kikwete Ikulu ya Dar es Salaam.
Wanaomba appointment Ikulu, wakisharuhusiwa wanakwenda kuzumgumza na Rais kisha wanapiga picha za pamoja na kuondoka, hapo tunaambiwa wanajadili sheria ya mabadiliko ya katiba.
Haya yalianzishwa na Chadema ambao walipinga muswada wa katiba mara mbili mwishoni mwa mwaka jana, chama hicho kilisusia mjadala wa katiba bungeni huku wabunge wake na wakiwemo baadhi ya wabunge wa NCCR Mageuzi, wakitoka nje ya ukumbi wa wabunge kuashria msimamo wao.
Baada ya bunge kumaliza mjadala wao, Chadema wakaomba kukutana na Rais Kikwete Ikulu, kujadili kile walichokuwa wakikipinga mkutano ukafanyika kwa muda wa siku mbili, walipomaliza Rais akausaini muswada waliokuwa wakiupinga Chadema ukawa sheria.
CUF nacho kikaomba appointment ya kumuona Rais, pamaja na kwamba chama hicho hakikususia mjadala wa shera ya mabadiliko ya katiba bado kikaenda kumuona Rais, sijui walimtaka Rais afanyaje wakati walishakubalina kila kitu bungeni.
NCCR Mageuzi nacho kikaomba appointment kwa Rais ili kutimiza wajibu wake, wamejadiliana walichojadili wakamaliza na kupiga picha na Rais Ikulu.
Mazungumzo ya Chadema yakajirudia safari hii na Slaa, nae alikuwepo, kitu cha kujiuliza hivi haya mazungumzo wananchi wameshilikishwa au na ni mawazo ya viongozi wa nyama vya siasa, tukumbuke kuwa kuna wananchi wasiokuwa na uanachama wa chama chochote, hao nao wanawakilishwa na nani Ikulu?
Kwa nini hivyo vikao vya katiba kama vinawakilisha mawazo ya wananchi visitangazwe moja kwa moja na televisheni ili angalau wananchi wasikie kilichojadiliwa? katiba hii sio ya Rais au vyama vya siasa, ni yetu sote.
Kwa nini wachache wajifungie Ikulu kujadili mustakabali wa maisha yetu???