CHA The GREAT
JF-Expert Member
- Nov 11, 2010
- 651
- 853
Ni karibu wiki ya pili sasa kumekuwa na mjadala kuhusiana na kanuni/sheria mpya za mafao. Mjadala huo ambao ulimuibua Spika wa Bunge Job Ndugai hata kusema kuwa bunge halistahili lawama hizo kwa kuwa wao (bunge) sio waliotunga kanuni hizo, kutokana na wadau wengi kutupia lawama zake kwa bunge, umeangazia zaidi kwenye kile kinachoitwa kikokotoo, kwamba mfanyakazi, mara tu baada ya muda wake wa kustaafu kufika, basi atachukua asilimia 25, wakati asilimia 75 atapewa kidogokidogo kwa miaka 12. Kadhalika, suala la FAO LA KUJITOA nalo limezungumziwa na kulalamikiwa na wengi, nikiwamo mimi mwandishi wa mada hii. Pamoja na malalamiko yote hayo ya wafanyakazi, ambayo chanzo chake ni Mbunge wa CHADEMA, Esther Bulaya, bado vyama vya wafanyakazi chini ya shirikisho lao ambalo ni TUCTA, vimekuwa kimya na kigugumizi kana kwamba hakuna kinachoendelea kwa wanachama wake. Je, hii ina maana gani? Ni kwamba vyama vya wafanyakazi havioni tatizo kwa hicho kinacholalamikiwa, au vinatafuta muda muafaka ili vitoe msimao wake juu ya sheria na kanuni mpya ya pensheni?