Kwa nini Vita zidi ya Ugaidi/Terrorism visiitwe kuwa ni Vita kuu ya tatu ya Dunia?

Kevin.A

Member
Apr 3, 2012
12
4
Heshima kwenu wana-JF,

Nimekuwa nikijiuliza mara kwa mara ni vigezo gani vinatumika ili vita yeyote kuwa mentioned kama ni Vita kuu ya Dunia?Na ni nani anajukumu la kusema kuwa hii ni Vita kuu ya Dunia (is it UN)?.Mpaka sasa kuna Vita kuu ya Dunia I & II.
Nilikuwa nafikiri kuwa moja ya kigezo ni idadi ya nchi zinazoshiriki kupigana ktk hiyo vita.Nikajiuliza kama hiki ni kigezo kimojawapo basi ni kwa nini vita zidi ya Ugaidi/terrorism visiitwe ni Vita kuu ya tatu ya Dunia?Maana karibu nchi zote duniani zinapambana ktk hii vita na magaidi/terrorist wamezagaa karibu dunia kote.

Naomba mawazo yenu ktk hili.
 
Heshima kwenu wana-JF,

Nimekuwa nikijiuliza mara kwa mara ni vigezo gani vinatumika ili vita yeyote kuwa mentioned kama ni Vita kuu ya Dunia?Na ni nani anajukumu la kusema kuwa hii ni Vita kuu ya Dunia (is it UN)?.Mpaka sasa kuna Vita kuu ya Dunia I & II.
Nilikuwa nafikiri kuwa moja ya kigezo ni idadi ya nchi zinazoshiriki kupigana ktk hiyo vita.Nikajiuliza kama hiki ni kigezo kimojawapo basi ni kwa nini vita zidi ya Ugaidi/terrorism visiitwe ni Vita kuu ya tatu ya Dunia?Maana karibu nchi zote duniani zinapambana ktk hii vita na magaidi/terrorist wamezagaa karibu dunia kote.

Naomba mawazo yenu ktk hili.

hujafafanua vizuri hapo, karibu nchi zote unamaanisha nini?? hebu zitaje hizo nchi japo 10 tu. nijuavyo mimi, kwanza neno GAIDI kila anayelitamka ana maana yake, MIMI NIKIKUITA WEWE GAIDI, NA WEWE UTANIITA GAIDI. kwa sisi tunaoamini katika kila linalosemwa na matajiri wa dunia yaani marekani, israel, uingereza na marafiki zao, tunafuata tafsiri yao ambapo kwao yeyote ambaye anapingana na matakwa yao, huwa wanambatiza GAIDI ili wahalalishe kumtandika wanavyotaka (rejea Iraq, Libya, Palestina n.k). hizi nchi, hata wanafiki UN hawakuridhia zichapwe, lakini zilitandikwa.
Kwa upande mwingine, ukifuatilia nchi kama Venezuela, Irani, Korea Kaskazini, Libya, Iraq, Palestina, Zimbabwe nao wanadai haya mataifa ya kimagharibi (marekani, israel, uingereza) ndo magaidi, sasa hapo inategemea wewe mwenyewe akili yako inayapima vipi mambo. Na msingi wa hayo yote nionavyo mie ni nchi zingine kutumia mabavu kutaka waitawale dunia wanavyotaka wao, wakiwaambia sasa muanze KUOANA WANAUME KWA WANAUME au WANAWAKE KWA WANAWAKE mseme, ndio mkuu, mkigoma HAKUNA MISAADA.
 
Back
Top Bottom