Kwame Nkrumah
JF-Expert Member
- Dec 2, 2008
- 886
- 376
Nilikua nasoma mada hapo chini ya jinsi spika aliyepita anavyoendelea kukaa kwenye nyumba ya serikali kwa kisingizio cha ustaafu.
Kila kukicha viongozi wetu wanashindana kufanya ufisadi bila uoga na maamuzi yenye kuogofya.
Licha ya mabadiliko yote yanayotokea ulimwengu wa sasa viongozi wetu wanakua kama wanaishi ulimwengu mwingine ambao wao hawataguswa na chochote.
Tunashuhudia nchi zilizokua zinatawaliwa kipolisi ambapo ukienda kinyume na matakwa ya watawala unapotea , lakini leo wananchi wamechukua maamuzi ya kudai haki zao.
Vyombo vyote vya ugandamizaji , na viongozi wake ni wa kwanza kusulubiwa wananchi wanapotwaa haki zao.
Sasa viongozi wetu wanajiweka kwenye kundi gani? kwa nini hawaogopi umma wa Watanzania utakapoamka?
Ni kwa nini hawana chembe ya uoga katika nafsi zao?
Kila kukicha viongozi wetu wanashindana kufanya ufisadi bila uoga na maamuzi yenye kuogofya.
Licha ya mabadiliko yote yanayotokea ulimwengu wa sasa viongozi wetu wanakua kama wanaishi ulimwengu mwingine ambao wao hawataguswa na chochote.
Tunashuhudia nchi zilizokua zinatawaliwa kipolisi ambapo ukienda kinyume na matakwa ya watawala unapotea , lakini leo wananchi wamechukua maamuzi ya kudai haki zao.
Vyombo vyote vya ugandamizaji , na viongozi wake ni wa kwanza kusulubiwa wananchi wanapotwaa haki zao.
Sasa viongozi wetu wanajiweka kwenye kundi gani? kwa nini hawaogopi umma wa Watanzania utakapoamka?
Ni kwa nini hawana chembe ya uoga katika nafsi zao?