Kwa nini ulinimwaga? "Why did you dump me"

frank m

Member
Feb 8, 2012
54
49
Mabinti muwe mnauliza! Unapopigwa chini na usichunguze kujua sababu then ukakimbilia kwenye mahusiono mengine....

Jumapili mi bachela, sipiki, nikitoka church hupendelea kutafuta sehemu nzuri ya kula, mara moja kwa wiki sioni tabu kula chakula cha alfu saba hadi kumi na tano, navyojibanaga katika ya wiki. Leo kama desturi yangu nikachagua restaurant moja ya bei ya juu kidogo, niko kwenye korido ya kuingia mawazo yapo mbali mara naskia sauti nyororo "jamani Frank" mbele yangu yu mrembo wa haja, binti kajaliwa kila kitu na kuvaa anajua, ni x wangu flani ila kapendezaa, inahitaji moyo. Roho paa ikanipiga, hatukuachana vizuri sana, nkashangaa napewa hagi kubwa ananishika mkono kuniongoza ndani, uko na kademu kako nini? Mbona unasita sita? Hapana bibie, ni mwenyewe natafuta menu. Tukae meza hii hapa, na mimi nakula.

Ehhee niambie Frank, nilikuwa na Betty akanionesha kidemu chako, yaani uliponimwaga nikajua utachukua bonge la demu, sasa demu gani yule hafiki hata robo ya uzuri wangu! Nikajibu kupotezea tu, c unajua Sophia mapenzi hayana macho.

We demu gani unadhani uzuri wa sura na umbo ndo kila kitu, demu huna mipango yako binafsi ya maisha, hujui unataka nini kwenye maisha, ukiambiwa geuka kushoto unaendea kulia unaenda! Huna vitu unavyovisimamia kwenye maisha ambavyo kamwe huta vicompromise! Tulipofahamiana nilikueleza ukweli ndoa si lazima tuchunguzane uone kama nafaa kuwa mume na mimi wewe mke! Cha ajabu hukuwahi kutaka kuanya jitihada kunifahamu licha ya mimi kukuchunguza kwa undani tena wazi wazi of course sa nyingine kwa kificho. Unachowaza ni ndo tu tena kwa maana ya sherehe ya harusi maana kwa ufupi wa akili yako hauko tayari kuwa mke wala hujui what being a wife is suppose to mean. Mrembo ndoa is much much more than ile sherehe ya harusi, kuitwa mke/mama si kazi ndogo. Kulea watoto hadi wakawa responsible citizens of tmrw bado huwezi kabisa. Unadai we msomi well and good ila hujaelimika mama! Degree yako inafaida gani? Yaani we ni mweupe kabisa kwenye mambo mengine, mvivu wa kufikiri, makusudi kabisa nilikuwa nakuuliza ushauri kwenye mambo kadhaa wa kadha, hakuna kilichokuwa kinanikera kama jibu la "mi sijua bwana" Kinachonikera zaidi ni kwamba you are not stupid, I do not know who put it in your head that beautiful ladies are supposed to be stupit. You know what impression you create unapokutanata na mwanaume? "Niahidi ndoa ntakuwa wako" That is a huge turn off kwa wanaume. Mbaya zaid unadhani pesa na umaarufu wa baba yako ni mtaji, yes babayako ni tajiri na maarufu lakini hilo si la msingi kwa mwanaume wa maana. Baba yangu ana hiki, baba yangu alifanya hivi, nikitaja jina tu kila mtu anamfahamu baba yangu. Hivi uliwahi kujua baba yangu mimi ni nani? Kama ulidhani kueleza alivyokuahidi babako wewe na mumeo mtarajiwa ingesaidi kuhamasisha ndoa pole sasa mama.

Sikumpasulia haya huyu binti, mwenyewe anadhani ana kila kitu mwanaume anachohitaji kuoa ila she's so wrong! I wish i had the courage to tell her, ana kazi kubwa sana ya kufanya!

Ushauri wa bure, na si kwa mabinti tu labda hata kwa wanaume, ukiachwa tafuta nafasi na x wako mwambie kwa nini alikupiga chini, ni mambo gani hakufurahishwa nayo kwako, una mapungufu gani

Ukijua haya utakuwa na mafanikio zaidi katika your nxt rlshp.

Lakini kumbuka 4 every rule there are exceptions!
 
hata yeye atampata wake...na mapungufu yake,sio wanaume wote wanahitaji mwanamke focused na career minded.
 
asante kaka, kuna wadada wao wanaganda tu harusi. Harusi! Harusi! Ukimchunguza kwenye quality za domestic hayupo kabisa. Nani anapenda maisha ya kula hotelini huku ameoa? Ukimwambia nina mpango wa kuanzisha mashamba anakwambia mi siwezi kulima labda utasimamia mwenyewe. Khaa! Huwezi kulima,hata kusimamia vibarua? Utaambiwa naogopa nyoka. Of coz wanawake wapo wa aina nyingi,wa show bararani,wa kutafuta maisha nk. Yaani hata ukimwambia ntaanzisha biashara,anajibu ntakuwa nimechoka nikitoka kazini! Mshahara wenyewe upi? Bado anataka na gari mnunue ili akatanue kwa wafanyakazi wenzie. Unapotafuta mke mchalenge na mambo ya kimaisha kwanza. Wengine ni wasichana!
 
jamani, wanamme wanalalamika hakuna wanawake, wanawake wanalalamika hakuna wanamme.

Bora wanyama hawajaacha asili yao.
 
asante kaka, kuna wadada wao wanaganda tu harusi. Harusi! Harusi! Ukimchunguza kwenye quality za domestic hayupo kabisa. Nani anapenda maisha ya kula hotelini huku ameoa? Ukimwambia nina mpango wa kuanzisha mashamba anakwambia mi siwezi kulima labda utasimamia mwenyewe. Khaa! Huwezi kulima,hata kusimamia vibarua? Utaambiwa naogopa nyoka. Of coz wanawake wapo wa aina nyingi,wa show bararani,wa kutafuta maisha nk. Yaani hata ukimwambia ntaanzisha biashara,anajibu ntakuwa nimechoka nikitoka kazini! Mshahara wenyewe upi? Bado anataka na gari mnunue ili akatanue kwa wafanyakazi wenzie. Unapotafuta mke mchalenge na mambo ya kimaisha kwanza. Wengine ni wasichana!

Anakupa na masharti, eti kama unamnunulia gari isiwe Vits!
 
hakuna kipindi nilipata wakati mgumu kama wakati nikitaka kuoa,kweli wadada wanajisahau sana.bt thanks to the almighty god maana pasipo muongozo na usimamizi wake sasa ningalikuwa ktk majuto.bt safari inaenda vizuri! vijana mna kazi ktk kuwapata ambao mnahita kushare nao maisha yanayobaki after commitment.well said frank
 
Alikua sio saizi yako. alikua in the wrong bt bado ukamgwaya kumwambia ukweli?
 
Back
Top Bottom