TzComedy
JF-Expert Member
- Jul 15, 2017
- 890
- 700
Juzi nusura nivunjwe Jicho langu la kulia baada ya kurushiwa ngumi moja takatifu, kilichonishangaza sio kurushwa kwa ngumi hiyo ispokuwa mtu mwenyewe alienirushia hiyo ngumi takatifu.
Kwakweli yule mtu kama ni chuvi, hakika nawaambia kaila na sio kaila tu, bali kaila vilivyo.
Chanzo ni huu utamaduni wetu wa shikamoo kwa yule unaeona kakuzidi umri, ni kawaida yangu na ndio nilivolelewa na kufundishwa na wazazi na hata walezi pia kuwa kwa mujibu wa utamaduni wetu sisi watz, mtu aliekutangulia kuliona Jua kumpa Shikamoo si jambo la mjadara bali ni la mtekerezo, kwahiyo tangia hapo najiona mwenye fahari kubwa kukupa haki yako ya Shikamoo wewe ulienizidi kwa umri.
Hasa inakuwaje mimi mtoto mwema natekeleza wajibu wangu kwako kwa kukupa Shikamoo yako alafu unataka kunipa kilema cha maisha?!, mboni kwenye Daradara nikikupisha kwenye siti kwa kuamini wewe ni Mkubwa kwangu kwa hiyo unastahili kukaa kuliko mimi kwa utamaduni wetu, hauwi Mbogo?.
Waenga shikamoo ni haki yenu, mboni hamuitendei haki Shikamoo kwa nini??.
Kwakweli yule mtu kama ni chuvi, hakika nawaambia kaila na sio kaila tu, bali kaila vilivyo.
Chanzo ni huu utamaduni wetu wa shikamoo kwa yule unaeona kakuzidi umri, ni kawaida yangu na ndio nilivolelewa na kufundishwa na wazazi na hata walezi pia kuwa kwa mujibu wa utamaduni wetu sisi watz, mtu aliekutangulia kuliona Jua kumpa Shikamoo si jambo la mjadara bali ni la mtekerezo, kwahiyo tangia hapo najiona mwenye fahari kubwa kukupa haki yako ya Shikamoo wewe ulienizidi kwa umri.
Hasa inakuwaje mimi mtoto mwema natekeleza wajibu wangu kwako kwa kukupa Shikamoo yako alafu unataka kunipa kilema cha maisha?!, mboni kwenye Daradara nikikupisha kwenye siti kwa kuamini wewe ni Mkubwa kwangu kwa hiyo unastahili kukaa kuliko mimi kwa utamaduni wetu, hauwi Mbogo?.
Waenga shikamoo ni haki yenu, mboni hamuitendei haki Shikamoo kwa nini??.