Madimba jr
JF-Expert Member
- Aug 12, 2017
- 1,577
- 3,143
Hakuna kitu sikipendi kama kuita mitaa au barabara majina ya watu ambao hawana impact kwa vizazi vyetu mfano Sam Nujoma,Namndi Azikiwe,Mwai Kibaki Road,wakati tuna majembe yetu Mkwawa,Chief Mareare,Chief Machemba,Mwinyigumba,King Majuto,Steve Kanumba,Diamond,Ali Kiba,Marijan Rajab,Tiex Mosh William,Ngurumo,Moses Nnauye,Kambona yan icons kibao tunawaacha wanapotea tu hivi hivi,Mzee Sykes vijana mnamjua? hata wasomi wapo kibao kama wakina Shivji kwa nini Iwe Nkurumah hall na sio Temeke Sanga Hall? hivi kuna anayemjua aliyetunga wimbo wa taifa,Tazama Ramani,Tanzania Tanzania? tumeshindwa hata kuwapa majina yao kwenye madaraja kama Mfugalle bridge? hizi ndo urithi zenyewe za taifa jamani sio kila siku Mkapa bridge,mkapa tower,BW Mkapa high school what a selfish.....atleast leo nimeona jambo watu wa sumbawanga wamefanya wamempa Shule Diamond hii anagalau inaleta heshima kwa wasanii wetu ambao kimsingi wanaonekana hawana maana ila kipindi cha kampeni ndo tunawaona wa thamani kubwa....kwa taifa letu lilipofikia hakuna namna hawa ndio wanaotuwakilisha vyema kimataifa na wala sio jiwe,Au Lusinde Kibajaji,wala taifa stars tuwape heshima yao ili jamii na vizazi vijavyo vione umuhimu wa wao kujituma na kuwa inspired,huo ndio uzalendo tunaoutaka na sio vinginevyo.Kwani haiwezekani kuwa na Ali Kiba road? Kwani haiwezekani kuwa na Steven Kanumba Hall?