chanawaleti
Senior Member
- Jul 4, 2016
- 176
- 209
jana kwa mwembe naenda zangu ofisi za ppf Morocco pale nikiwa sijui hili wala nini nikiwa tayari nishaset malengo yangu kwa kuwa nilishaacha kazi nilipokuwa miez kadhaa iliyopita nikisema mzigo nilio nao ppf unatosha kujiajiri kabisa nikichukua niende kulima maana nimechoka na dharau za kuajiriwa kupelekeshwa bora nijiajiri kufikia pale mapokezi zile ofisi zipo pole Morocco ppf karibu na eartel Kuna dada Ana dharau pale acha unamuuliza kitu anajibu kwa jodo utadhani ofisi ni ya baba yake alinijibu kwa dharau sana adi nilinyongonyea nisubir miaka 55 sasa mimi nina 28 je 55 nitafika na tayari nishaumia? nilijitoa pale nikaenda pale ccra ni hapo hapo Morocco pia hawakua na jibu na moja kwa moja walichosema wao ppf ndiyo hawatoi kabisa ila nssf na mifuko mingine wanatoa hivi hawa ppf kwa nn wao wasitoe hawaoni wanatunyanyasa hv mm mpaka nifikishe hiyo 55 ni lini wakati nataka kujiajiri?