Allen Kilewella
JF-Expert Member
- Sep 30, 2011
- 18,070
- 33,553
Nimesikia taarifa kwamba Rais John Pombe Magufuli akimshauri Mkurugenzi wa DAWASA Archad Mutalemwa kujistaafisha kwani ni "Mzee" ili awaachie "vijana". Lakini wakati Rais anamshauri Mutalemwa Askari wawili wa Usalama Barabarani waliuawa huko Mkoani Pwani ikiwa ni muendelezo wa mauaji ya watu na Askari kwenye mkoa huo.
Hivi ni mpaka nani auawe ndipo itaonekana Waziri wa Mambo ya ndani ya nchi Mwigulu Nchemba anatakiwa kujiuzulu. Hivi mauaji haya si kiashiria kwamba Waziri naye anatakiwa ajiuzulu ili apewe mtu mwingine mwenye maono tofauti na yeye?
Hivi ni mpaka nani auawe ndipo itaonekana Waziri wa Mambo ya ndani ya nchi Mwigulu Nchemba anatakiwa kujiuzulu. Hivi mauaji haya si kiashiria kwamba Waziri naye anatakiwa ajiuzulu ili apewe mtu mwingine mwenye maono tofauti na yeye?