Kwa nini ni hayari kuvuka Mediterenia kuelekea Ulaya?

Kashi

JF-Expert Member
Jan 6, 2013
897
742
Habari wana Jf? Nimekuwa nikisikia kwa muda mrefu sasa wahamiaji haramu kutoka Afrika Kaskazini hasa Libya wakizama katika bahari hii katika harakati za kuelekea Ulaya, mara nyingi taarifa zinazosikika ni za maafa ya kuzama kwa boti. Maswali kadhaa yamekuwa yakinisumbua kuhusu suala hili.
1.Je,ni kwamba wahamiaji hawa wanatumia vyombo hafifu sana kuvuka?
2. Mediterania ni bahari hatari sana kuvuka?
3.Mataifa ya Ulaya hushambulia vuombo hivi?
Tafadhali mwenye uelewa wa jambo hili nasubiria mchango wako.
 
Ni hatari sana hilo eneo kuna upepo mkali na bahari ina mawimbi makubwa kipindi inachotulia kwa mwaka mzima ni kifupi sana na hilo eneo lina kina kirefu sana achilia mbali wanatumia wanatumia vile vifaa vinavyojazwa upepo na watu wanakua wengi...sehemu yenyewe sio mbali kutoka upande mmoja kwenda upande mwingine mtu yeyote anaamini kule anafika kumbe sio kirahisi hivyo na waafrika walianza muda sana kuvuka pale sema kipindi cha nyuma walikua watu wachache wanavuka na ajali hazitangazwi ni kama mexico kuitafuta USA wabongo kibao wamepita ile njia sasa hivi imekua tatizo...
 
Ni hatari kwa sababu wana tumia vyombo dhaifu na wanajazana kwa wingi ni safari yenye mashaka ebu fikilia baridi lote la bahari mawimbi mazito unavuka na mashua ya kubeba watu hamsini mko 100 hiyo ndio hatari yenyewe
 
hawa wakiwa kwenye puto lao,halafu hao sio walibya ni afrika magharibi.
1150387
 
Ni hatari sana hilo eneo kuna upepo mkali na bahari ina mawimbi makubwa kipindi inachotulia kwa mwaka mzima ni kifupi sana na hilo eneo lina kina kirefu sana achilia mbali wanatumia wanatumia vile vifaa vinavyojazwa upepo na watu wanakua wengi...sehemu yenyewe sio mbali kutoka upande mmoja kwenda upande mwingine mtu yeyote anaamini kule anafika kumbe sio kirahisi hivyo na waafrika walianza muda sana kuvuka pale sema kipindi cha nyuma walikua watu wachache wanavuka na ajali hazitangazwi ni kama mexico kuitafuta USA wabongo kibao wamepita ile njia sasa hivi imekua tatizo...
Asante kiongozi kwa maelezo murua, nilikuwa nashangaa ajali za kuzama ni nyingi sana.
 
Waafrika sijui tukoje yani hata kununua life jacket na kuzivaa imekuwa shida yani watu wanarisk maisha kiasi hicho!
 
Hao waafrika magharibi waliotii sera za kufyatua ili wawe wengi nchi zao ziwe na uchumi mkubwa sasa wanakwenda kusumbua wale wanaodai walibania mayai ya uzazi.
sasa mtu anayekwambia kunya nitazoa,nawewe unayekunya bila kujiuliza ni kwanini azoe yeye mavi yako,nani atakuwa na matatizo kichwani hapo.
 
Back
Top Bottom