Kwa nini NEC wanatangaza wagombea urais kwa ujimbo?

Boramaisha

JF-Expert Member
Apr 29, 2009
820
18
Wenye ueledi wa jambo hili tunaomba watufahamishe. Nimekuwa nikiwasikia NEC wakitaja matokeo ya urais na mwisho wanataja nafasi za wagombea watatu wa kwanza kwa misingi ya majimbo badala ya idadi ya kura na kwa hali hiyo Dk. Slaa anatangazwa kwamba ameshika nafasi ya tatu badala ya kuwa nafasi ya pili kutokana na wingi wa kura. Je jambo hilo ni sahihi ama ni mbinu tu za makusudi za kutotaka kumpa "Kaisari yaliyo ya Kaisari?'
 
Nafikiri hili ni kosa kubwa linalofanyika na NEC. Majimbo mengine yana wapiga kura chini ya elfu tano wakati mengine yana wapiga kura laki moja. Kuwa wa kwanza kwenye jimbo lenye wapiga kura elfu tano si sawa na kuwa wa pili kwenye jimbo lenye wapiga kura elfu sabini ambapo umepata kura elfu thelathini.
 
Spin masters wa hii kitu ni ITV/Radio One, jamaa kila wakitangaza utasikia wanasema number 1.ni JK 2 ni Lipumba na 3 ni Daktari, Lakini ukenda kwenye number ya kura, mambo tofauti kabisa...huu ni upotoshaji wa wazi kabisa.
 
KAKA HAPA NI SABABU ZA NEC NI UIZI MTUPU ANGALIA HAPA. ANGALIA KATI YA GEITA NA NYANG`HWALE:A S angry:
Mojawapo ya majimbo aliyoyataja Dr Slaa jana ni utofauti wa matokeo ya jimbo la Geita, katika pita pita yangu nimegundua matokeo ya Geita na jimbo la Nyang'hwale yanafanana kila kitu.

Je walipitwa au ni uzembe, kama ni kweli je kuna majimbo mangapi yenye dosari za namna hii au zingine???

Jionee mwenyewe kwenye hii spread sheet. Au unaweza kugonga hapa: The National Electrol Commission of Tanzania - Homepage





au

Hivi ndivyo inavyoonekana mpaka leo tarehe 04.11.2010 Saa kumi na mbili na dakika 28 za jioni (12.28 kwa Kiswahili) za Tanzania, Saa za Afrika Mashariki. Mkuu tuwekee na wewe muda uliozinakili pamoja na tarehe. Weka chini ya jedwali lako hapo mwanzo.
 
0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom