Kwa nini mmoja awe na virusi vya ukimwi na wingine hana?

Bra-joe

JF-Expert Member
Apr 2, 2012
1,562
986
Wakuu, kuna maswali huwa yananisumbua sana kuhusu watu wanaoishi kama mke na mume, halafu mmoja kaathirika na mwingine mzima na wanawatoto ambao hawajaathirika, na mara nyingi mwanamke ndio anakuwa kaathirika. Maswali yenyewe: 1. je, inakuwaje aliyeathirika asimuambukize mwenza wake wakati hawatumii kinga? 2. Je, mume huyu akizini na mwanamke mwingine aliyeathirika bila kinga atapata maambukizi? 3. Je, inawezekana mwanaume akawa na vvu halafu mwanamke hana?
 
1.Labda mume anamuandaa vizuri mke so michubuko inakua hamna
2.Labda m/me anapiga ki-star na sio kukomoa
3.Labda m/me ana dushelele dogo(bamia) na m/ke amboni pakubwa
 
1.Labda mume anamuandaa vizuri mke so michubuko inakua hamna
2.Labda m/me anapiga ki-star na sio kukomoa
3.Labda m/me ana dushelele dogo(bamia) na m/ke amboni pakubwa

hapa natafuta majibu ya kisayansi, na siyo mitaani, kama hujui siyo lazima kujibu, waachie wajuzi,
 
hizo couple kitaalamu , NO! kiingereza zinaitwa discordant couple sababu ni hii. virusi vya ukimwi huwa vina shambulia seli za kulinda mwili kwa kuingia ndani ya seli na kuanza kujizalisha na sio seli yoyote ile , sasa je kirusi kinajuaje hii seli niingie na hii nisiingie? kwenye ukuta wa hizi seli kunakuwa na alama zilizojichomoza ambazo kirusi kikiziona kinaitambua seli na kujishikiza na halama hizo au vishikio hivyo husaidia kirusi kuingia ndani, sasa kuna baadhi ya watu hawana hivyo vishikio/alama (cell surface receptors) kwenye cell zao kwa hiyo hata kirusi kikiingia kwenye damu kitashindwa kuingia ndani ya seli so unakuta mtu hata afanye ngono na mtu mwenye ngoma hapati ngoma
 
hapa natafuta majibu ya kisayansi, na siyo mitaani, kama hujui siyo lazima kujibu, waachie wajuzi,

Ukiacha hizo sababu unazoziamini na hizi zinachangia,usiwe mtumwa wa kisayansi,kama wewe mwanasayansi kati ya kuku na yai nani kaanza?
 
guys, probability ya kuambukizwa virusi vya ukimwi kwa kila unapofanya tendo la ndo ni only 2%. Na uwezekano wa maambukizo huwa ni rahisi zaidi kama mme na mke wataingiliana kwa kutumia nguvu, no maandalizi, kama wataingiliana kwa njia ya haja kubwa (ana sex), na kama game inakwenda mda mrefu sana na kusababisha maji ya ukeni kukauka. Na hivyo kuanzisha msuguano mkali. Kwa hiyo kama hawa watu wanafanya mapenzi ya kistaarabu na si kukomoana, ni kazi ngumu sana kuziangukia kwenye hii 2%.
 
hizo couple kitaalamu , NO! kiingereza zinaitwa discordant couple sababu ni hii. virusi vya ukimwi huwa vina shambulia seli za kulinda mwili kwa kuingia ndani ya seli na kuanza kujizalisha na sio seli yoyote ile , sasa je kirusi kinajuaje hii seli niingie na hii nisiingie? kwenye ukuta wa hizi seli kunakuwa na alama zilizojichomoza ambazo kirusi kikiziona kinaitambua seli na kujishikiza na halama hizo au vishikio hivyo husaidia kirusi kuingia ndani, sasa kuna baadhi ya watu hawana hivyo vishikio/alama (cell surface receptors) kwenye cell zao kwa hiyo hata kirusi kikiingia kwenye damu kitashindwa kuingia ndani ya seli so unakuta mtu hata afanye ngono na mtu mwenye ngoma hapati ngoma

Kwa hiyo huyo mtu anaweza kuwa na HIV bila kuwa na AIDS au inakuwaje doctor?
 
Kwa hiyo huyo mtu anaweza kuwa na HIV bila kuwa na AIDS au inakuwaje doctor?[/QUOTE
mara nying wakisema ana HIV lakini hana AIDS maana yake virusi vimeingia mwilini lakini havijasababisha upungufu wa kinga mwilini na tunategemea siku zinavyoenda atapata upungufu wa kingaAIDS/UKIMWI . lakini kwa hawa jamaa tunaweza kusema kweli ana HIV lakini kamwe hawezi kupata UKIMWI sababu virusi havitaweza kamwe shambulia seli za kinga na mara nyingi haviwezi dumu muda mrefu sababu vitashindwa kuzalina nadhani hata kumuambukiza mtu mwingine itakuwa ngumu ulichosema ni sahihi ila kinaweza tumika katika context mbalimbali,
 
mara nying wakisema ana HIV lakini hana AIDS maana yake virusi vimeingia mwilini lakini havijasababisha upungufu wa kinga mwilini na tunategemea siku zinavyoenda atapata upungufu wa kingaAIDS/UKIMWI . lakini kwa hawa jamaa tunaweza kusema kweli ana HIV lakini kamwe hawezi kupata UKIMWI sababu virusi havitaweza kamwe shambulia seli za kinga na mara nyingi haviwezi dumu muda mrefu sababu vitashindwa kuzalina nadhani hata kumuambukiza mtu mwingine itakuwa ngumu ulichosema ni sahihi ila kinaweza tumika katika context mbalimbali,

Asante doctor.
Hivi carriers nao wapo kwenye kundi gani hapa na vipimo vinasemaje juu yao?
 
Probabilities za "Normal" sexual HIV transmission rates:
•Receptive anal sex: 0.5%


•Insertive anal sex: 0.07%


•Receptive vaginal sex: 0.1%


•Insertive vaginal sex: 0.05%


•Receptive oral sex: 0.01%


•Insertive oral sex: 0.005%


– thus unprotected anal intercourse is the most efficient method of sexual transmission




Ole wenu mnaoabudu tiGO!!!
 
Ukiacha hizo sababu unazoziamini na hizi zinachangia,usiwe mtumwa wa kisayansi,kama wewe mwanasayansi kati ya kuku na yai nani kaanza?
acha kuongea ujinga wewe hamna mtu ambaye siyo mtumwa wa kisayansi karne hii kama wewe siyo mtumwa unatafuta nini hapa jf acha kuongea ujinga wewe....hii yote ni faida ya kisayansi sio unaongea tuu kwa kuwa umepewa mdomo.......afu chunga kauli zako
 
Asante doctor.
Hivi carriers nao wapo kwenye kundi gani hapa na vipimo vinasemaje juu yao?
carriers ni wale wenyeHIV lakini kinga yao haija athirika kiasi cha kupata magonjwa nyemelezi yaani hawana UKIMWI, na vipimo vyao huonyesha HIV positive
 
Sasa na mimi naomba ufafanuzi hapo.Labda mzee anaukimwi inawezekana mama akawa mjamzito asipate ukimwi na mtoto asipate ukimwi kweli.
 
hizo couple kitaalamu , NO! kiingereza zinaitwa discordant couple sababu ni hii. virusi vya ukimwi huwa vina shambulia seli za kulinda mwili kwa kuingia ndani ya seli na kuanza kujizalisha na sio seli yoyote ile , sasa je kirusi kinajuaje hii seli niingie na hii nisiingie? kwenye ukuta wa hizi seli kunakuwa na alama zilizojichomoza ambazo kirusi kikiziona kinaitambua seli na kujishikiza na halama hizo au vishikio hivyo husaidia kirusi kuingia ndani, sasa kuna baadhi ya watu hawana hivyo vishikio/alama (cell surface receptors) kwenye cell zao kwa hiyo hata kirusi kikiingia kwenye damu kitashindwa kuingia ndani ya seli so unakuta mtu hata afanye ngono na mtu mwenye ngoma hapati ngoma
Aksante sana mkuu, je kama mtu hana vishikio halafu akafanya ngono na mtu aliyeathirika bila kinga, na baadaye akafanya na mtu ambaye hana maabukizi, je anaweza kumuambukiza ukimwi? Je, mtu anaweza kupimwa kujua kama anavishikizo au la?
 
guys, probability ya kuambukizwa virusi vya ukimwi kwa kila unapofanya tendo la ndo ni only 2%. Na uwezekano wa maambukizo huwa ni rahisi zaidi kama mme na mke wataingiliana kwa kutumia nguvu, no maandalizi, kama wataingiliana kwa njia ya haja kubwa (ana sex), na kama game inakwenda mda mrefu sana na kusababisha maji ya ukeni kukauka. Na hivyo kuanzisha msuguano mkali. Kwa hiyo kama hawa watu wanafanya mapenzi ya kistaarabu na si kukomoana, ni kazi ngumu sana kuziangukia kwenye hii 2%.

aksante mkuu.
 
Probabilities za “Normal” sexual HIV transmission rates:
•Receptive anal sex: 0.5%


•Insertive anal sex: 0.07%


•Receptive vaginal sex: 0.1%


•Insertive vaginal sex: 0.05%


•Receptive oral sex: 0.01%


•Insertive oral sex: 0.005%


– thus unprotected anal intercourse is the most efficient method of sexual transmission




Ole wenu mnaoabudu tiGO!!!

Nashukuru sana ndugu.
 
Aksante sana mkuu, je kama mtu hana vishikio halafu akafanya ngono na mtu aliyeathirika bila kinga, na baadaye akafanya na mtu ambaye hana maabukizi, je anaweza kumuambukiza ukimwi? Je, mtu anaweza kupimwa kujua kama anavishikizo au la?
kwa kawaida ya magonjwa yote ya kuambukiza huwa kunakuwa na time toka kuambukizwa mpaka nae aweze kuambukiza. mfano siku za mwanzo mgonjwa wa ukimwi uwezo wake wa kuambukiza unakuwa mdogo lakini siku zinavyopita unakuta hata mate yanakuwa na virusi. tukirudi kwenye swali haiwezekani mtu huyu kuambukiza sababu vurusi vinatakiwa viingie kwenye damu kisha ndani ya seli kuzaliana na kusambaa sehemu mbalimbali za mwili kama vile kwenye mbegu za kiume sasa visipozaliana haviwezi kusurvive na pia concentration yao inakuwa ndogo mno to be infective
 
Sasa na mimi naomba ufafanuzi hapo.Labda mzee anaukimwi inawezekana mama akawa mjamzito asipate ukimwi na mtoto asipate ukimwi kweli.
mkuu sina data za kiniback up lakini kwa kufikiri naweza sema hivi. mama kama hana cell surface receptors hawezi kuambukizwa hata akiwa na mimba, halafu virusi kwa njia ya kujamiiana let say kupitia mbegu za kiume haviingii kwenye damu moja kwa moja zinapitia kwenye seli zilizopo kwenye uke ziitwazo dendritic cells so vikishindwa kuingia kwenye dendritic cells hata kwenye damu havitaweza kufika na mtoto hawezi ambukizwa. lakini kama virusi vikiwa introduced moja kwa moja kwenye damu na vikapata chansi ya kupita kwenye placenta na kukutana na damu ya mtoto ambaye anazo cell surface receptors naona kuna kachance ka kumuambukiza
 
Back
Top Bottom