Albedo
JF-Expert Member
- Feb 24, 2008
- 5,559
- 1,452
Nimekuwa nikifuatilia mijadala hapa JF inachokihusu Chama Cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), lakini mijadala hii mara nyingi imekuwa ikiishia kwenye Malumbano, watu kuitana Majina ya Ajabu ambayo naamini kabisa kama tungekuwa tunatumia majina yetu halisi basi ni wazi wakati mwingine huwa tunawatukana hata Baba zetu.
Nimejaribu kuwa mfwatiliaji (Kuliko Mchangiaji) katika hizi mada na nimefanikiwa kugundua ni kwa nini basi hii mijadala haina Manufaa kwa CHADEMA wala kwa Taifa
1: Mijadala mingi ya JF Imejenga makundi makuu mawili na sasa hata hiyo mijadala imekuwa na Mabishano na Matukanano kati ya hayo makundi Mawili ( Mimi nawaita Watu wazima Hovyo)
2: Kuweko kwa makundi hayo Mawili kumesababisha baadhi ya Member Makini wa JF kutochangia hiyo Mijadala kwa kuogopa kuwekwa katika moja ya hayo makundi na kwa sababu watu wengi wamekuwa wakichangia kimajungu na kivisa.
3: Makundi hayo ni
1: Zitto Haters: Hawa ni wale ambao wanaona au wanadhani kwamba Zitto ndiye hasa Tatizo kubwa lililopo katika chama na ni Mtu ambaye hafai kabisa kuwa hata Mwanachama wa CHADEMA. Kundi hili limekosa support ya Member wa JF ambao kwa michango yao wanafahamika kabisa kwamba wao ni CCM ( Chama ambacho kwao ustawi wa CHADEMA ni tishio la Maisha na Ulaji wao)
2: Mbowe Haters: Hawa ni wale ambao wanaona au wanadhani kwamba Mbowe ndiye hasa Tatizo kubwa lililopo katika chama na ni Mtu ambaye hafai kabisa kuwa Mwenyekiti wa CHADEMA. Kundi hili ( Sijui ni Bahati Mbaya au Nzuri) linaungwa mkono na Member wengi kama si wote ambao kutokana na Michango yao wanafahamika kabisa kwamba wao ni CCM damu (Chama ambacho Maslahi na Ustawi wake unategemea zaidi na namna gani uongozi wa CHADEMA uko, eidha weak au strong)mfano Dar Es Salaam, Malaria Sugu, JayKey na wengine wengi tu.
Lengo la kuweka hii topic ni kuwafanya Wana CHADEMA wote makini ( Namaanisha wale wanaoamini kwamba Chama hakijengwi na Mtu Mmoja) kupima na kuangalia juu ya ama kuchangia ama kuipuuza mijadala yeyote inayolenga kuvunja umoja na Mshikamano ulioko ndani ya Chama
Asanteni
Nimejaribu kuwa mfwatiliaji (Kuliko Mchangiaji) katika hizi mada na nimefanikiwa kugundua ni kwa nini basi hii mijadala haina Manufaa kwa CHADEMA wala kwa Taifa
1: Mijadala mingi ya JF Imejenga makundi makuu mawili na sasa hata hiyo mijadala imekuwa na Mabishano na Matukanano kati ya hayo makundi Mawili ( Mimi nawaita Watu wazima Hovyo)
2: Kuweko kwa makundi hayo Mawili kumesababisha baadhi ya Member Makini wa JF kutochangia hiyo Mijadala kwa kuogopa kuwekwa katika moja ya hayo makundi na kwa sababu watu wengi wamekuwa wakichangia kimajungu na kivisa.
3: Makundi hayo ni
1: Zitto Haters: Hawa ni wale ambao wanaona au wanadhani kwamba Zitto ndiye hasa Tatizo kubwa lililopo katika chama na ni Mtu ambaye hafai kabisa kuwa hata Mwanachama wa CHADEMA. Kundi hili limekosa support ya Member wa JF ambao kwa michango yao wanafahamika kabisa kwamba wao ni CCM ( Chama ambacho kwao ustawi wa CHADEMA ni tishio la Maisha na Ulaji wao)
2: Mbowe Haters: Hawa ni wale ambao wanaona au wanadhani kwamba Mbowe ndiye hasa Tatizo kubwa lililopo katika chama na ni Mtu ambaye hafai kabisa kuwa Mwenyekiti wa CHADEMA. Kundi hili ( Sijui ni Bahati Mbaya au Nzuri) linaungwa mkono na Member wengi kama si wote ambao kutokana na Michango yao wanafahamika kabisa kwamba wao ni CCM damu (Chama ambacho Maslahi na Ustawi wake unategemea zaidi na namna gani uongozi wa CHADEMA uko, eidha weak au strong)mfano Dar Es Salaam, Malaria Sugu, JayKey na wengine wengi tu.
Lengo la kuweka hii topic ni kuwafanya Wana CHADEMA wote makini ( Namaanisha wale wanaoamini kwamba Chama hakijengwi na Mtu Mmoja) kupima na kuangalia juu ya ama kuchangia ama kuipuuza mijadala yeyote inayolenga kuvunja umoja na Mshikamano ulioko ndani ya Chama
Asanteni