lyinga
JF-Expert Member
- Nov 18, 2013
- 2,496
- 1,035
Ndugu hembu tuulizane hili swali na kuwazua ni kwa nini fisadi au wezi wa mali za uma wana uchungu na kile wanachoona wamekipata lakini pale wanapoona wananazidiwa nguvu na wananchi kwa njia yeyote na kwa nguvu zote watatumia nguvu zao kufanikisha udhulumati wao lakini sisi wananchi wenye mali ambao tumeibiwa wala hatuna shida tunaona nisawa tu natolea mfano wizi wa epa, richmond, mikataba mibovu, tembo kuuwawa bilioni 200 hazijulikani zilipo lakini sie wananchi tupo kama vile hakujatokea kitu lakini hawa jamaa wapo imara hata umpeleke mahakamani ataibuka kidedea na faini juu tunalipishwa wananchi nauliza kunani hapo? Tumelogwaa au tuna mapepo tuombewe?