Kwa nini kwenye ndege hakuna Parachuti?

Usedcountrynewpipo

JF-Expert Member
Aug 1, 2012
3,638
2,720
Nilitokwa na jicho nilipopanda ndege kwa mara ya kwanza. Air hostes akatangaza kuwa ikitokea umeme ukakatika ndani ya ndege (utadhani vile TANESCO) basi kuna life jacket, au boya la kuogelea chini ya kiti. Nikawaza kwa nini wasingeweka parachuti na badala yake wameweka boya?
 
Kimbilio la kwanza ndege inapoanguka ni Baharini !
!
Thats why
 
Parachuti inahitaji mafunzo chuoni kuitumia. Haitamsaidia abiria wa kawaida hata ikiwekwa katika ndege.
 
Mmh, kuna zile parachuti za ku eject, huwa zinawekwa kwenye ndege za kijeshi. Yani ndege likibuma tu, rubani ana eject ile siti yake na kupotelea anakokujua!
 
Hata ukipewa ukae nalo Mkononi hiyo panic tu,hutakumbuka kama umebeba Parachuti Mkuu. Kama kuogelea hujawahi, Kuruka Angani utaweza!? Ok, Sawa. Let's Assume kwamba Plan A works out good, I mean unajua kulitumia Hilo Parachuti, What if Plan B ya kujiokoa, ukajikuta Umeshuka Salama hadi Chini Lakini Destination yako ikawa sehemu kama Ngorongoro/Serengeti au Amazon/Panama Forest(Home of Giant and Killer Sneaks-ANACONDA)!? Hapo napo utakuwa Ume-save!???
 
Nilitokwa na jicho nilipopanda ndege kwa mara ya kwanza. Air hostes akatangaza kuwa ikitokea umeme ukakatika ndani ya ndege (utadhani vile TANESCO) basi kuna life jacket, au boya la kuogelea chini ya kiti. Nikawaza kwa nini wasingeweka parachuti na badala yake wameweka boya?

Mkuu, nimecheka sana baada ya kuisoma thread yako, parachute huwa linahitaji mtu mwenye mafunzo ya jinsi ya kuliongoza na jinsi ya kutua unapofika karibu na ardhi, si kila apandae ndege ana mafunzo ya jinsi ya kutua na parachute, hata wale wote unaowaona wanaruka na parachute huwa wana mafunzo na uzoefu wa jinsi ya kutua na parachute
 
Back
Top Bottom