Kwa nini JMK hastahili na hafai kuongezewa kipindi kingine !!

Mag3

Platinum Member
May 31, 2008
13,063
22,755
Baada ya kumsikiliza Mzee Cigwiyemwisi John Samwel Malecela kuhusu utamaduni wa ndani wa CCM kumwongezea kipindi kingine cha miaka mitano Raisi aliyeko madarakani, inabidi tukae chini kama wananchi tujiulize maswali kadhaa. Mwaka 2005, Raisi Col. Dr. Al Haj Jakaya Mrisho Kikwete alitoa ahadi na malengo kadha wa kadha na kuahidi kuyatimiza kwa ari, kasi na nguvu mpya.

Huu ni muda muafaka wa kutazama amefanikiwa kwa kiwango gani katika kufikia hayo malengo. Naomba tushirikiane kwa kuyaanika na kuyajadili hayo malengo na kupima kama yapo mafanikio na mapungufu. Mimi naanza na moja linalohusu nishati na hasa umeme ambapo miezi minne tu baada ya kuchaguliwa, Raisi alitamka haya kuhusu sakata la kupatikana kwa umeme wa uhakika.

We have been grappling with this problem for quite some time now – but only with ad hoc measures.The recent power problems have afforded us the opportunity to rethink our energy strategy in holistic terms. We have learnt that ad hoc measures are costly in the long run and have their own limits. As we grapple with our energy problem, we are witnessing an upsurge of interest for investments in power generation in Tanzania. We are confident that in two years time, we will be on course to realize reliable power supply in Tanzania.

Ni wazi hapa aliwaahidi wananchi kuwa chini ya miaka mitatu tatizo la umeme lingeshughulikiwa na tungeweza kuwa na mipango madhubuti ya umeme wa kuaminika. Sasa baada ya miaka karibu minne na tukikaribia uchaguzi mwingine mwaka kesho, kuna dalili zozote kuwa tumepiga hatua katika kutatua hili tatizo ? Je, kuna sababu yoyote ya kuendelea kumwamini Raisi kwenye hili na na kumwongezea kipindi kingine ?

Naomba na wengine mtafute ahadi zingine alizozitoa tuweze kuzijadili - nawasilisha.​
 
Napinga kujiuzulu kwa Kikwete,kujiuzulu ni kukimbia na mjeshi hakimbii ,kama ameamua kuwa mpiganaji basi apigane hadi risasi ya mwisho ,na tujue kama mmoja wa kiongozi wa Tanzania alikuwa Mwanajeshi kwa ufupi mimi kama mwanajeshi naona Mheshimiwa anatuaibisha ,jeshi hawi goigoi kwa kuwaogopa kuwachukulia hatua marafiki ,nafikiri ni wakati wa kureact as a military personal na yupo frontline na amekutana na adui ambae ni rafiki yake ,nini la kufanya bila ya shaka yeye kama mwanajeshi hatuhitaji kusemea hapa.
 
Ahadi nyingi Mkuu alitowa na kipindi chake cha miaka mitano hakijaisha. Tutakuja kupima aliyotekeleza na aliyoshindwa na bila shaka sababu atatowa. Kwani JMK au CCM ni Mungu kila walichahidi lazima watekeleze? Mangapi tunashindwa kutekeleza ya majumbani mwetu kila siku? Tuwe wastarabu kupima na sio kung'ang'ania siasa kwa malengo ya kukosoa tu.
 
Wajameni!!! hizi threads za JK or JMK or else kama zinakuwa nyingi na hivyo kukata stimu ya ufuatiliaji; NAOMBA KAMA MODS MNAWEZA KUUNGANISHA ILI TUPATE PILAU NA KACHUMBARI YAKE NA KACHUMBARI KWAKE, PILAU KWAKE NA NDIZI KWAKE

NI MAONI TU, DELETE IF INAPPROPRIATE
 
Baada ya kumsikiliza Mzee Cigwiyemwisi John Samwel Malecela kuhusu utamaduni wa ndani wa CCM kumwongezea kipindi kingine cha miaka mitano Raisi aliyeko madarakani, inabidi tukae chini kama wananchi tujiulize maswali kadhaa. Mwaka 2005, Raisi Col. Dr. Al Haj Jakaya Mrisho Kikwete alitoa ahadi na malengo kadha wa kadha na kuahidi kuyatimiza kwa ari, kasi na nguvu mpya.

Huu ni muda muafaka wa kutazama amefanikiwa kwa kiwango gani katika kufikia hayo malengo. Naomba tushirikiane kwa kuyaanika na kuyajadili hayo malengo na kupima kama yapo mafanikio na mapungufu. Mimi naanza na moja linalohusu nishati na hasa umeme ambapo miezi minne tu baada ya kuchaguliwa, Raisi alitamka haya kuhusu sakata la kupatikana kwa umeme wa uhakika.



Ni wazi hapa aliwaahidi wananchi kuwa chini ya miaka mitatu tatizo la umeme lingeshughulikiwa na tungeweza kuwa na mipango madhubuti ya umeme wa kuaminika. Sasa baada ya miaka karibu minne na tukikaribia uchaguzi mwingine mwaka kesho, kuna dalili zozote kuwa tumepiga hatua katika kutatua hili tatizo ? Je, kuna sababu yoyote ya kuendelea kumwamini Raisi kwenye hili na na kumwongezea kipindi kingine ?

Naomba na wengine mtafute ahadi zingine alizozitoa tuweze kuzijadili - nawasilisha.​


Alipoeleza hayo ni kabla ya hali ya uchumi haijaparaganyika na kama ujuavyo kutokana na uvivu wetu mimi, wewe, JK na watanzania wengi kwa ujumla huwa tunategemea kutembeza bakuli. Wenye mapesa wana yao hawayajui.
Pia alipowaamini watu katika kumsaidia kutafuta ufumbuzi wamemuendesha mkenge. Na la Tatu kwa mujibu wa mambo yanavyofichuka sidhani kama tunae aliepunguwa uchafu kuliko JK. Jee unataka tujaribu kwa mapanki Lipumba au DJ Mbowe au kigugumizi Mrema?
 
Ahadi nyingi Mkuu alitowa na kipindi chake cha miaka mitano hakijaisha.

Aliahidi kushughulikia matatizo ya umeme ndani ya miaka mitatu. Huo muda umepita na ndio bado kabisa tunaongelea kununua mitambo si tu ya dharura na chakavu - nchi inayumbishwa na matapeli.



Tutakuja kupima aliyotekeleza na aliyoshindwa na bila shaka sababu atatowa.

Uchaguzi ni mwakani na tayari tunaambiwa ataongezewa miaka mingine mitano. Kipindi cha lala salama kinajulikana kama kipindi ambapo viongozi hufanya madudu wakijua hawatarudi kuomba kura. Can we risk it kwa huyu bwana ambaye hata hana cha kuonyesha katika awamu yake ya kwanza ?

Kwani JMK au CCM ni Mungu kila walichahidi lazima watekeleze?

Kwanza tuliambiwa ni chaguo la Mungu (joke), pili kwa nini aahidi asichokiweza ? Na kama kashindwa kutekeleza alichoahidi, kwa nini tuzidi kumwamini ? - kama kashindwa mzigo, ya nini kumwongezea zaidi ? Labda utuambie kwa nini alishindwa wakati yeye mwenyewe alijigamba anaweza.

Mangapi tunashindwa kutekeleza ya majumbani mwetu kila siku?

Kama unashindwa kutekeleza uliyoahidi nyumbani kwako ni juu ya hao uliowaahidi wakuwajibishe. Unamwahidi mwanao nguo ya sikukuu halafu huleti - kwa nini asilalamike na kulia ? Tofauti hapa ni kwamba mtoto hachagui mzazi lakini wananchi tukimchagua kiongozi akashindwa, lazima tuulize kulikoni ?

Tuwe wastarabu kupima na sio kung'ang'ania siasa kwa malengo ya kukosoa tu.

Mstaarabu ni yule anayekubali kuwa jukumu tulilompa linamzidi kimo na hivyo kuachia ngazi. Wengine tumekuwa sana wastaarabu tukampima na kuona kuwa mpaka sasa hajaonyesha uwezo na hivyo hafai kuongezewa kipindi kingine - kosa letu liko wapi ?
 
Alipoeleza hayo ni kabla ya hali ya uchumi haijaparaganyika na kama ujuavyo kutokana na uvivu wetu mimi, wewe, JK na watanzania wengi kwa ujumla huwa tunategemea kutembeza bakuli. Wenye mapesa wana yao hawayajui.

Yaani hata hayo mamilioni yanayoliwa ni kutokana na hali ya uchumi duniani kuparaganyika !! Kushindwa kusimamia utawala wa sheria na haki ni matokeo ya kuparaganyika kwa uchumi wa dunia !! Je alijua haya yote wakati anatoa ahadi ?

Pia alipowaamini watu katika kumsaidia kutafuta ufumbuzi wamemuendesha mkenge.

Aliahidi kuwa hangekuwa na ubia na yeyote kwenye utawala wake - iweje aendeshwe mkenge na wasaidizi anaowateua yeye. Kwamba hiyo imewezekana ina maana moja tu kuwa hana uwezo, period - mengine ni bla bla tu.

Na la Tatu kwa mujibu wa mambo yanavyofichuka sidhani kama tunae aliepunguwa uchafu kuliko JK.

Kati ya watu milioni arobaini hakuna mwingine ila KJ tu - wengine wote ni wachafu kuliko yeye !! La haula ! ashakum si matusi.

Jee unataka tujaribu kwa mapanki Lipumba au DJ Mbowe au kigugumizi Mrema?

Unapofanya mtihani na kushika nafasi ya mwisho darasani, huwezi kusema ati wewe una akili kuliko ambao hawajapewa mtihani. Hakuna nafasi ambayo ni chini ya mwisho - after hitting the bottom line, one can only go up !!
 
It's high time for the nation to choose someone with the right agenda for the top job. Hii tabia ya kuwaachia wanafiki katika chama kile kile kwa miaka nenda rudi kutuchagulia mtu wa kutuongoza haitatupeleka kokote. Mnaweza kukataa, lakini ukweli ndio huo. Siku zote chaguzi zetu zinatabirika, kwa sababu inajulikana watakayempitisha Chimwaga ndio huyohuyo, inaonyesha ni namna gani fikra za watz wote zimetawaliwa na siasa zilezile. Haiingii akilini kabisa kuona kuwa miaka yote hii watz hatuoni kiini cha matatizo yetu kuwa ni uongozi mbovu tunaoupanda sisi wenyewe. Watu wanaingia madarakani kwa ajili ya kutafuta umaarufu tu, hawana agenda yeyote, hawana mipango, uraisi sio kwa ajili ya kumake fun, it's a serious job for serious people. Mark my words, mpaka tutakapokuwa serious, nchi hii imekodishwa kwa the wrong people with the wrong agenda. Na bahati mbaya, hata wasomi wetu hawana agenda yoyote!!!
 
Mimi naanza na moja linalohusu nishati na hasa umeme ambapo miezi minne tu baada ya kuchaguliwa, Raisi alitamka haya kuhusu sakata la kupatikana kwa umeme wa uhakika.

Quote:
We have been grappling with this problem for quite some time now – but only with ad hoc measures.The recent power problems have afforded us the opportunity to rethink our energy strategy in holistic terms. We have learnt that ad hoc measures are costly in the long run and have their own limits. As we grapple with our energy problem, we are witnessing an upsurge of interest for investments in power generation in Tanzania. We are confident that in two years time, we will be on course to realize reliable power supply in Tanzania.


*****************

Mag3: Siyo tu miezi minne baada ya kuchaguliwa alitoa hiyo ahadi, bali pia baada ya miezi sita tu watu wake wakapiga ufisadi mmoja kabambe wa kihistoria (Richmond), uliotetemesha nchi na hatimaye kujiuzulu kwa mawaziri wake 3 akiwemo PM (EL).

Hii pekee iikuwa tosha kwa yeye mwenyewe kubwaga manyanga kwani suala alilikowa analitolea ahadi ndilo hilo hilo watu wake wa karibu wakalikung'uta! tuna rais kweli?
 
Mimi naanza na moja linalohusu nishati na hasa umeme ambapo miezi minne tu baada ya kuchaguliwa, Raisi alitamka haya kuhusu sakata la kupatikana kwa umeme wa uhakika.

Quote:
We have been grappling with this problem for quite some time now – but only with ad hoc measures.The recent power problems have afforded us the opportunity to rethink our energy strategy in holistic terms. We have learnt that ad hoc measures are costly in the long run and have their own limits. As we grapple with our energy problem, we are witnessing an upsurge of interest for investments in power generation in Tanzania. We are confident that in two years time, we will be on course to realize reliable power supply in Tanzania.


*****************

Mag3: Siyo tu miezi minne baada ya kuchaguliwa alitoa hiyo ahadi, bali pia baada ya miezi sita tu watu wake wakapiga ufisadi mmoja kabambe wa kihistoria (Richmond), uliotetemesha nchi na hatimaye kujiuzulu kwa mawaziri wake 3 akiwemo PM (EL).

Hii pekee iikuwa tosha kwa yeye mwenyewe kubwaga manyanga kwani suala alilikowa analitolea ahadi ndilo hilo hilo watu wake wa karibu wakalikung'uta! tuna rais kweli?

Kwa kweli jamaa ameshindwa kutekeleza hata moja ambalo aliahidi, sasa amebakia kuvunja baraza la mawaziri mara kufanya mabadiliko kwa wakuu wa wilaya! inamaana hakuwa makini wakati anawateuwa!!
 
Mimi sidhani kama anastahili kuongezewa muda, yeye akiwa kama raisi information zote nyeti za nchi huwa wa kwanza kuzipata, na sidhani kama anafanyaga uteuzi wa mawaziri peke yake bila watu wa usalama. Kama information za lowasa, karamagi, mramba, chenge na wengineo alikuwanazo ilikuwaje awachague hao mabwana kuwa mawaziri na ni watu wachafu, inamaana kulikuwa hakuna watu safi tanzania wakuweza kukamata hizo nafasi, ok jamaa wamejiuzuru lakini mkuu anakwambia hizo ni ajali za kisiasa!
Tangu aingie madarakani mpaka sasa term yake ya 1 inaenda ukingoni mimi sijaona hata kitu kimoja huyo bwana alichokifanya zaidi ya kuangaika na system, watu wamechoka mpaka wanafikia hatua ya kupopolewa kwa mawe kwa sababu alichokiahidi hata hajaanza kukigusa sasa anataka kutuambia miaka hiyo mitano ya lala salama ndio ataanza kutekeleza ahadi,

m2 mwenye busara ukishindwa unakaa pembeni na kuwapisha wengine, nyerere pamoja na misimamo yake na kujiamini lakini ilifika kipindi alichemsha na akaamua kukaa pembeni,
 
It's high time for the nation to choose someone with the right agenda for the top job. Hii tabia ya kuwaachia wanafiki katika chama kile kile kwa miaka nenda rudi kutuchagulia mtu wa kutuongoza haitatupeleka kokote. Mnaweza kukataa, lakini ukweli ndio huo. Siku zote chaguzi zetu zinatabirika, kwa sababu inajulikana watakayempitisha Chimwaga ndio huyohuyo, inaonyesha ni namna gani fikra za watz wote zimetawaliwa na siasa zilezile. Haiingii akilini kabisa kuona kuwa miaka yote hii watz hatuoni kiini cha matatizo yetu kuwa ni uongozi mbovu tunaoupanda sisi wenyewe. Watu wanaingia madarakani kwa ajili ya kutafuta umaarufu tu, hawana agenda yeyote, hawana mipango, uraisi sio kwa ajili ya kumake fun, it's a serious job for serious people. Mark my words, mpaka tutakapokuwa serious, nchi hii imekodishwa kwa the wrong people with the wrong agenda. Na bahati mbaya, hata wasomi wetu hawana agenda yoyote!!!

hawa wenye right agenda for the top job ni akina nani? tehetehe tuweni wawazi jamani 2010 inabisha hodi
 
hawa wenye right agenda for the top job ni akina nani? tehetehe tuweni wawazi jamani 2010 inabisha hodi

Mchakato ndio uanze, naamini mtu mwenye right agenda yupo. Sidhani kama unataka kunisadikisha kwamba hatuna mtz mwenye upeo wa kututoa hapa tulipo, na kwamba huyu jamaa ndio bora zaidi. Kama ni hivyo basi we are in a hell a lot of shit than we think we are already in right now!
 
Baada ya kumsikiliza Mzee Cigwiyemwisi John Samwel Malecela kuhusu utamaduni wa ndani wa CCM kumwongezea kipindi kingine cha miaka mitano Raisi aliyeko madarakani, inabidi tukae chini kama wananchi tujiulize maswali kadhaa. Mwaka 2005, Raisi Col. Dr. Al Haj Jakaya Mrisho Kikwete alitoa ahadi na malengo kadha wa kadha na kuahidi kuyatimiza kwa ari, kasi na nguvu mpya.

Huu ni muda muafaka wa kutazama amefanikiwa kwa kiwango gani katika kufikia hayo malengo. Naomba tushirikiane kwa kuyaanika na kuyajadili hayo malengo na kupima kama yapo mafanikio na mapungufu. Mimi naanza na moja linalohusu nishati na hasa umeme ambapo miezi minne tu baada ya kuchaguliwa, Raisi alitamka haya kuhusu sakata la kupatikana kwa umeme wa uhakika. Ni wazi hapa aliwaahidi wananchi kuwa chini ya miaka mitatu tatizo la umeme lingeshughulikiwa na tungeweza kuwa na mipango madhubuti ya umeme wa kuaminika. Sasa baada ya miaka karibu minne na tukikaribia uchaguzi mwingine mwaka kesho, kuna dalili zozote kuwa tumepiga hatua katika kutatua hili tatizo ? Je, kuna sababu yoyote ya kuendelea kumwamini Raisi kwenye hili na na kumwongezea kipindi kingine ?

Naomba na wengine mtafute ahadi zingine alizozitoa tuweze kuzijadili - nawasilisha.​

- Rais wa jamhuri ana mapungufu mengi sana, lakini la umeme sio lake, amejitahidi sana kwenye hilo lakini ameangushwa sana watekelezaji wake, on rais part nia ilikuwepo, lakini tizama waliyoyafanya kina Msabaha, Karamagi, Lowassa, Rostam, na sasa mpaka kina Zitto, I mean kwenye hili la umeme rais angefanya nini zaidi?

- Maaana labda sasa inabidi aache urais awe Waziri wa Nishati, rais ni bin-adam mmoja, hawezi kuwepo kila mahali all the time, hapa kwenye la umeme tumejiangusha wenyewe, halafu tunapongelea uchaguzi wa rais tuwe tunatoa alternative badala ya kuwaacha wananchi hewani, kwa sababu political realty iko wazi kwamba Muungwana atashinda tena kwa 90%, ndio maana viongozi wengi mashuhuri wa upinzani wameamua kutafuta ubunge kuepuka aibu, huo ndio ukweli ulio wazi.

- Ndani ya CCM kuna vikundi vinavojaribu kuamini kwamba wanaweza kumtoa JK 2010 that is a dreaming big time, so far wameshaonyesha kwamba hawana smart political strategies, kwa sababu huwezi kupata nafasi ya kugombea CCM mpaka uwe sawa na watu muhimu mle ndani, sasa the fact kwamba kina Malecela wanajitokeza mapema kama majuzi ni kwamba hawa makundi wameshindwa kuwa-consult na kutafuta support ya watu kama yeye, thinking kwamba sio muhimu sana matokeo yake ndio haya sasa, wazee wanajitokeza tena kwa maneno mazito sana.

- Tumjadili rais kwa mengine, lakini la umeme ni letu wenyewe wananchi, rais amewahi mpaka kuwabadili watendaji wa sekta ya umeme, lakini wapi mpaka leo kitendawili tu na maneno mengi na kugombea hela za hiyo sekta ya umeme, aibu sana!

FMES!
 
Ahadi nyingi Mkuu alitowa na kipindi chake cha miaka mitano hakijaisha. Tutakuja kupima aliyotekeleza na aliyoshindwa na bila shaka sababu atatowa. Kwani JMK au CCM ni Mungu kila walichahidi lazima watekeleze? Mangapi tunashindwa kutekeleza ya majumbani mwetu kila siku? Tuwe wastarabu kupima na sio kung'ang'ania siasa kwa malengo ya kukosoa tu.

wewe wa kupigwa mawe wewe!!!!! Ona raha kuandika humu, kasimame karikaoo waeleze watu uliyoandika hapa!!!!

kiongozi yeyote lazima awe strategic, foreseer, JK anaexprience ya miaka zaidi ya 10 katika serikali yake, lazima alitakiwa ajue kipi ataweza na kipi asichoweza,

hivi hali mpya, nguvu mpya sijui na nini...vile vimeishia wapi??

watanzania walifanya makosa kumchagua huyu, kwani hakuwa na rekodi yeyote ya kuvutia kumchagua huyu!!! kwanza alipitia wizara ya nishati see what is going on now??????????????????????????
 
Kamwambiye aliyekutuma kwamba agenda yake imepwaya haijapokelewa JF.

Nungunungu,
Aliyenituma ni mzalendo anayeishi kwa mlo moja kwa siku huku watoto wake wakinyimwa elimu kwa kukosa karo. Aliyenituma ni mama mjamzito anayejifungulia nyumbani kwa kuwa gharama ya kumfikisha hospitalini hana. Aliyenituma ni makulima anayeshinda juani siku nzima akitumia jembe la mkono na kuhangaika kulisha watoto wake wanaolia njaa usiku kucha. Aliyenituma ni mgonjwa anayeugulia nyumbani bila matumaini ya kupona kwa sababu gharama ya matibabu na dawa haiwezi. Aliyenituma ni mwanakijiji anayehamishwa alikozaliwa na alikowazika babu zake kwa sababu mwekezaji amenunua eneo lote la kijiji. Aliyenituma ni mwanafunzi ambaye anashindwa kutumia muda wake kujisomea kwa kuwa umeme huwaka mara moja kwa wiki. Aliyenituma ni mwalimu ambaye anasota bila mshahara baada ya kuhakikisha vijana wetu wanapata elimu. Aliyenituma ni mwananchi ambaye baada ya hadaa ya maisha bora alipiga kura kumchagua atakayemtatulia matatizo yake.

Walionituma ni umma ulioahidiwa utawala wa haki na sheria na badala yake wezi wanatanua mitaani. Walionituma ni walalahoi wanaoona hali zao za maisha inazidi kudidimia huku mafisadi wakila na kusaza. Walionituma ni vijana wenye hasira waliochoshwa na utawala ulio na ubia na wahujumu uchumi na wako tayari kuwachoma kama vibaka. Walionituma ni wenye mioyo ya dhati ya kuijenga nchi lakini wenye meno kwa kutumia hila wanaitafuna nchi kama mchwa. Walionituma ni wazee wastaafu wa iliyokuwa jumuiya ya EAC ambao mafao yao yalitumika kununulia mahekalu ughaibuni na sasa moja baada ya mwingine wanafariki bila kufaidi halali yao.

Nungunungu, kama na wewe unaona haya ni vigumu kuelewa kinachokutuma lakini kama huoni naweza tu nikakupa pole. Msimamo wangu kuhusu wahusika wote wakuu kwenye ufisadi uko wazi na unajulikana - wewe je ? Mambo yote haya yanafanyika chini ya utawala wa JMK, je kwa nini aliomba kura na kwa nini alililia Uraisi kama alijua hana ujasiri wa kupambana na haya ? Jibu bila shaka ni rahisi sana - wazungu husema, "if you cant fight them, join them". Je yawezekana JMK baada ya kushindwa mapambano ameamua kuungana na MAFISADI au muda wote amekuwa moja wao ? Wengine kwa kuwa sasa baada ya miaka minne tumeweza kumwelewa tunasema hafai kuongezewa kipindi kingine, je wewe waliokutuma ni akina nani ?
 
Kikwete hana uwezo wa kutekeleza ahadi zake kwa kadiri ya kwamba anaowategemea kutekeleza ahadi hizo ni watu aliowateua yeye mwenyewe, kuwabeba, kuwavumilia na kuwadekeza katika madaraka yao.

Leo hii Waziri Mkuu anataka Mkuu wa Mkoa afute kesi mahakamani kwa vile ni ya mwana CCM na hutasikia Ikulu au CCM iseme lolote.
 
Back
Top Bottom