thereitis
JF-Expert Member
- Nov 8, 2010
- 297
- 41
Shukrani ni desturi ya binadamu baada ya kutendewa jambo jema. Mwaka 2005 tulishuhudia JK akipita sehemu mbalimbali za nchi yetu Tanganyika akiwashukuru wananchi kwa kumchagua kuwa rais wao; Pia alitoa ahadi nyingi zilizoashiria maisha bora kwa watanzania.
Baada ya kutangazwa mshindi wa kiti cha rais wa Tz kwa mara ya pili(2010-2015), JK hajapita maeneo mbalimbali ya nchi hii kuwashukuru wananchi kwa kumchagua kuwa rais wao kwa kipindi kingine cha miaka 5. Je JK kwa kutowashukuru wananchi anathibitisha tuhuma kuwa yeye na chama chake walichakachua matokeo ya kura za Urais?. Je bado JK anayo "Legitimate"(ridhaa) ya kuliongoza Taifa hili wakati hawezi kuwatembelea wananchi kwa lengo la kuwashukuru na kujua matatizo yao?
Baada ya kutangazwa mshindi wa kiti cha rais wa Tz kwa mara ya pili(2010-2015), JK hajapita maeneo mbalimbali ya nchi hii kuwashukuru wananchi kwa kumchagua kuwa rais wao kwa kipindi kingine cha miaka 5. Je JK kwa kutowashukuru wananchi anathibitisha tuhuma kuwa yeye na chama chake walichakachua matokeo ya kura za Urais?. Je bado JK anayo "Legitimate"(ridhaa) ya kuliongoza Taifa hili wakati hawezi kuwatembelea wananchi kwa lengo la kuwashukuru na kujua matatizo yao?