Waziri Mkuu wa Uturuki amesema kuwa nchi za Magharibi zinaendesha siasa za nyuso mbili katika suala zima la silaha za nyuklia.
Recep Tayyid Erdogan amesema hayo alipohojiwa na televisheni ya CNN na kuongeza kuwa, utawala wa Kizayuni wa Israel ndio utawala pakee unaomiliki silaha za nyuklia katika eneo la Mashariki ya Kati na kuhoji akisema, vipi nchi hizo ambazo zinaizuia Iran kuwa na silaha za nyuklia haziipigi marufuku pia Israel kumiliki silaha hizo?
Uturuki imepunguza kwa kiasi kikubwa uhusiano wake na utawala wa Kizayuni wa Israel baada ya Tel Aviv kukataa kuomba radhi kutokana na makomandoo wake kuuvamia msafara wa meli za misaada uliokuwa unaelekea Ghaza tarehe 31 Mei, 2010 na kuua raia tisa wa Uturuki.
Hata hivyo mapema mwezi huu, Waziri wa Uchumi wa Uturuki alisema kuwa nchi yake itaendelea kuwa na uhusiano wa kawaida wa kibiashara na utawala dhalimu Israel.
Takwimu zinaonyesha kuwa, mabadilishano ya kibiashara kati ya Uturuki na utawala wa Kizayuni yalifikia dola bilioni 2.3 kuanzima mwezi Januari hadi Julai mwaka huu.
Kwa hisani ya Redio Tehran
Recep Tayyid Erdogan amesema hayo alipohojiwa na televisheni ya CNN na kuongeza kuwa, utawala wa Kizayuni wa Israel ndio utawala pakee unaomiliki silaha za nyuklia katika eneo la Mashariki ya Kati na kuhoji akisema, vipi nchi hizo ambazo zinaizuia Iran kuwa na silaha za nyuklia haziipigi marufuku pia Israel kumiliki silaha hizo?
Uturuki imepunguza kwa kiasi kikubwa uhusiano wake na utawala wa Kizayuni wa Israel baada ya Tel Aviv kukataa kuomba radhi kutokana na makomandoo wake kuuvamia msafara wa meli za misaada uliokuwa unaelekea Ghaza tarehe 31 Mei, 2010 na kuua raia tisa wa Uturuki.
Hata hivyo mapema mwezi huu, Waziri wa Uchumi wa Uturuki alisema kuwa nchi yake itaendelea kuwa na uhusiano wa kawaida wa kibiashara na utawala dhalimu Israel.
Takwimu zinaonyesha kuwa, mabadilishano ya kibiashara kati ya Uturuki na utawala wa Kizayuni yalifikia dola bilioni 2.3 kuanzima mwezi Januari hadi Julai mwaka huu.
Kwa hisani ya Redio Tehran