Kwa nini Israel ilimnyima Idd Amin ndege kuipiga Tanzania?

Mwanamayu

JF-Expert Member
May 7, 2010
11,342
6,467
Jamani ni kwa nini Israel ilikataa kumpa Idd Amin ndege za kisasa (wakati ule) ili kuipiga Tanzania mwaka 1972? Na kwa nini walifunga Ubalozi Tanzania au tulivunja mahusiano ya kidiplomasia na hao jamaa?
 
Ubalozi wa Israel nchini Tz ulifungwa na Nyerere akipinga kukaliwa kwa palestina.
 
Hapana. Msipotoshe hapa. Idi Amin mwaka 1972 hakuwa na jeshi la hewa. Baada ya kumpindua Obote aliwaita wanajeshi wote wa kikosi cha anga na waliokwenda akawaua. Waliosalimika baadhi walikimbilia Tanzania. Akaanza kujenga kikosi kipya. Amin asingekuwa na uwezo wa kuishambulia Tanzania wakati huo. Hata pale aliposhambulia Mwanza kwa mabomu mwaka 1973 ndege zake zilipita kwa mbali kwa sababu ya kuogopa kutunguliwa ndio maana mabomu yake yalianguka kwenye kisiwa cha Nane Nane.
 
Hapana. Msipotoshe hapa. Idi Amin mwaka 1972 hakuwa na jeshi la hewa. Baada ya kumpindua Obote aliwaita wanajeshi wote wa kikosi cha anga na waliokwenda akawaua. Waliosalimika baadhi walikimbilia Tanzania. Akaanza kujenga kikosi kipya. Amin asingekuwa na uwezo wa kuishambulia Tanzania wakati huo. Hata pale aliposhambulia Mwanza kwa mabomu mwaka 1973 ndege zake zilipita kwa mbali kwa sababu ya kuogopa kutunguliwa ndio maana mabomu yake yalianguka kwenye kisiwa cha Nane Nane.
Mkuu jasusi heshima mbele,kwanza asante kwa kuwahi kuweka sawa mambo hapa.lakini mpaka sasa uganda inaaminika kuwa na jeshi bora kabisa la anga afrika mashariki toka enzi za KjAR kuweka headquarter ya jeshi ka anga huko,sababu za kikosi kizima(na vifaa?) kuangamizwa ni ngumu kudhibitisha,hebu tusaidie kufafanua hili mkuu,wale wana jeshi la anga,kuuwa jeshi la anga mkuu! Imenistua kidogo.natangulisha heshima mkuu.
 
Waisrael wenyewe walikuwa Taabani wakati huo. Walikuwa wanatagemea kila kitu kutoka kwa Bwana wao USA.
 
wangemsaidije idd amin wkt yeye mwenyewe aliteka ndege yao?
kuna makala inaonyeshwa NAT GEO channel kuhusiana na uvamizi
wa makomandoo wa Israel ktk uwanja wa entebe kukomboa watu wao.
kwa ufahamu wangu mdogo ndio hivo nijuavo hawakuwa na mahusiano mazuri.
 
Mkuu jasusi heshima mbele,kwanza asante kwa kuwahi kuweka sawa mambo hapa.lakini mpaka sasa uganda inaaminika kuwa na jeshi bora kabisa la anga afrika mashariki toka enzi za KjAR kuweka headquarter ya jeshi ka anga huko,sababu za kikosi kizima(na vifaa?) kuangamizwa ni ngumu kudhibitisha,hebu tusaidie kufafanua hili mkuu,wale wana jeshi la anga,kuuwa jeshi la anga mkuu! Imenistua kidogo.natangulisha heshima mkuu.
Ni kweli Uganda had the best air force in East Africa. Shule ya marubani wa ndege naturally ilikuwa Uganda. Lakini baada ya Amin kumpindua Obote hakuwaamini kabisa wanajeshi wa kikosi cha anga kwa hiyo akafanya njama kuitisha mkutano. Wote waliokwenda waliuawa. Waliobaki waliweza kutorokea Tanzania. Hebu jiulize wakati wa vita vya Kagera kwa nini Amin hakutumia ndege zake kutushambulia? Na huyu ndiye aliyekuwa anatishia kuwa atateka eneo la Tanzania hadi Tanga. Ndege zake zilikuwa hazifanyiwi matunzo tena kwa sababu most of the senior and experienced pilots had been killed. Soma kitabu cha David Martin "Idi Amin" analizungumzia kwa kirefu suala hilo.
 
Mwongozo naomba tusijadiri mada hii kwa kutumia movie(film) ya Kagera War,The last king of Scotland etc Amin hasingepata kupata msaada kutoka toka Israel kwani aliwachukia wao watu kama alivyokuwa Hitler.Hiyo ni moja,lakini ata Amin mwenyewe alijua vizuri kuendesha ndege za kivita hapo hatujui kwanini yeye hakuendesha ndege kuja kukomboa ardhi yao ya Kagera.Je unajua Uganda ni mojawapo ya nchi ambazo zilikuwa zimependekezwa kuwapokea wana Israel?
 
vita ya iddi amini ina mambo mengi ya kushangaza....

kwanza tanzania haikupata sapoti kutoka israel wala uingereza wakati nchi hizo

zilikuwa na uadui na iddi amini.....

hatukupewa 'baraka za kumpiga iddi amini ' na UN wala OAU......

kuna mtu anaitwa NOLAN...huyu jamaa aligeuka milionea kwa ajili ya vita hivi....

ndie alimuuzia nyerere silaha.....na akabaki nchini kuendelea na biashara zake...

alikuja kuoa mdada wa kinigeria aliyefungua duka la nguo lilikuwalinaitwa CONIE OF DAR pale Sheraton...now sijui inaitwa movenpick...sijui...
 
Waisrael wenyewe walikuwa Taabani wakati huo. Walikuwa wanatagemea kila kitu kutoka kwa Bwana wao USA.
hawakuwa taabani-mwishoni wa mwaka 1972 walikuwa wanapigana vita
then swala la wao kusaidiwa na USA kipindi hicho naweza sema lilikuwa kwa percent ndogo sana
 
Ni kweli Uganda had the best air force in East Africa. Shule ya marubani wa ndege naturally ilikuwa Uganda. Lakini baada ya Amin kumpindua Obote hakuwaamini kabisa wanajeshi wa kikosi cha anga kwa hiyo akafanya njama kuitisha mkutano. Wote waliokwenda waliuawa. Waliobaki waliweza kutorokea Tanzania. Hebu jiulize wakati wa vita vya Kagera kwa nini Amin hakutumia ndege zake kutushambulia? Na huyu ndiye aliyekuwa anatishia kuwa atateka eneo la Tanzania hadi Tanga. Ndege zake zilikuwa hazifanyiwi matunzo tena kwa sababu most of the senior and experienced pilots had been killed. Soma kitabu cha David Martin "Idi Amin" analizungumzia kwa kirefu suala hilo.
Nchi yenye jeshi bora la anga kwa dunia ya sasa ndio tishio zaidi.tumeshuhudia wamarekani wameshinda vita vingi kwa kutumia sana jeshi la anga hivyo kuwaachia kazi ndogo sana askari wa miguu.Waganda wanasifika sana kwa ubora wa jeshi la anga na kama kweli wanacho mpaka chuo lazima tukubali wanaweza kuwa superpower kijeshi Afrika Mashariki na kati,nafikiri ule ushindi wetu mwaka 79 usitudanganye,Museveni amejenga jeshi bora sana na bajeti yake ya jeshi ni kubwa kupitiliza hadi mataifa ya nje kupiga kelele.sisi ndio hao tunanunua helcopta feki zinadondoka hovyo! Sijui kama kuna operation gani kubwa na ngumu ukitoa vita vya kagera tunayoweza kutumia kupima uwezo wetu kijeshi nyakati hizi.tafadhali tusitaje ya commoro,kule hata mgambo wa jiji wangeshinda tu!
 
Back
Top Bottom