Kwanini inakuwa ngumu kusamehe katika mahusiano?

Hahhaha tunatofautisha vipi hivi vitu ?

Maana katika mahusiano wanawake ni hodari sana wa kukumbushia makosa ya nyuma,na wanaume pia ni hodari kukumbushia makosa ya nyuma.

So kwa mfumo huo tunajuaje ?
Wanawake ni mabingwa wa kulibeba jambo kwa muda mrefu anaweza akawa amekusamehe lakini akalibeba,"utasikia sijawah muongelesha mwaka mzima"
 
Sasa unajuaje kama mwwnamke amekusamehe ?
Mawasiliano ndio ishara ya kwanza kujua kama amekusamehe, mawasiliano baina yenu yanaimarika kama yalikuwa yanasua sua, lakini amani itarejea kati yenu yaani atakuwa na amani na wewe, hali ya utii kwako itarejea, kumbuka mwanamke akiwa na uchungu roho ya kiburi ,ukaidi na jeuri inamtawala kwahiyo kama amekusamehe hiyo hali inatoka na anaanza kukutii
 
Mawasiliano ndio ishara ya kwanza kujua kama amekusamehe, mawasiliano baina yenu yanaimarika kama yalikuwa yanasua sua, lakini amani itarejea kati yenu yaani atakuwa na amani na wewe, hali ya utii kwako itarejea, kumbuka mwanamke akiwa na uchungu roho ya kiburi ,ukaidi na jeuri inamtawala kwahiyo kama amekusamehe hiyo hali inatoka na anaanza kukutii
Sasa ule mfano uliotoa wa "simsemeshi mwaka mzima" unakujaje mkuu
 
Shida ni aliyekosa haoni kama kosa lake ni issue

Ama aliyekosewa muda mwingine hasemi amekosewa vipi

Kikubwa mawasiliano make sure mwenzako anaelewa how you feel
Ajue kipi kwako kina uzito na kipi unapuuzia
Na yeye mhimize aseme vya upande wake
 
Sasa ule mfano uliotoa wa "simsemeshi mwaka mzima" unakujaje mkuu
Mkuu hiyo Hali ya kutomsemesha Mwaka mzima inatokana na kuwa na uchungu na aliyekukosea hebu fikiria Hali unayokuwa nayo ukikutana na Mtu unayemdai Kwa muda mrefu na simu zako hapokei ndio namna Mtu anaweza akaenda na hiyo Hali ya mateso Mwaka mzima
 
Shida ni aliyekosa haoni kama kosa lake ni issue

Ama aliyekosewa muda mwingine hasemi amekosewa vipi

Kikubwa mawasiliano make sure mwenzako anaelewa how you feel
Ajue kipi kwako kina uzito na kipi unapuuzia
Na yeye mhimize aseme vya upande wake
Kuna wengine hata ukimwambia kosa anakuwa mkali atataka kujitetea au kujitoa kwenye kosa, ninavyoamini makosa tunyafahamu na mara nyingine huwa tunawakosea wenzi wetu huku tukijua, kwamfano ukimnyima mumeo/mkeo unyumba ni kumkosea Kwa sababu ni haki yake kupata, na msamaha sio Mpaka aliyekukosea akuombe Kwa sababu anayeumia ni wewe uliyekosewa
 
Asante kwa bandiko na mimi naomba niomgeze yafuatayo.

1.hali ya kutosamehe inamuumiza yule ambaye hataki kutoa msamaha.

Ukiweka kinyongo juu ya mtu aliyekukosea basi wewe ndo unaumia kwa sababu unafeel lile kosa na wala yule aliyekukosea hatouhisi ule uchungu kama unaouhisi wewe.

So samehe unakuwa umejiepusha na mengi na kuweka huru nafsi.
Pia, kutokusamehe ni kujifungia baraka/ mafanikio yako.
 
Kiburi na jeuri ndo vinanisumbua
Kwa kifupi hua sisamehi kabisa
Kwa hyo nimerogwa?
Sio umerogwa bali una Pepo lililokuvaa linakuongoza, ulimwengu wa giza hakunaga msamaha ukikosea huko Kila kosa linaenda na adhabu lakin ulimwengu wa Nuru Kuna Rehema na mwanadamu ameumbiwa kuwa na Rehema kumhurumia mwingine.
 
Kuna wengine hata ukimwambia kosa anakuwa mkali atataka kujitetea au kujitoa kwenye kosa, ninavyoamini makosa tunyafahamu na mara nyingine huwa tunawakosea wenzi wetu huku tukijua, kwamfano ukimnyima mumeo/mkeo unyumba ni kumkosea Kwa sababu ni haki yake kupata, na msamaha sio Mpaka aliyekukosea akuombe Kwa sababu anayeumia ni wewe uliyekosewa
Ss unatoaje unyumba na mtu kakukera??
Yani ukosee afu udai unyumba kimabavu😅then uje kusema umekosewa wkt we ndo ulimtoa mood mwenzako?.
Rekebisha kwanzaa🏃🏾‍♀️🏃🏾‍♀️
 
Back
Top Bottom