"kwa nini CUF tumeshirikiana na CCM"- Hamad Rashid

dos santos

JF-Expert Member
Nov 22, 2010
256
128
Akijibu swali kwa nini CUF imekubali kushirikiana na CCM kuunda serikali ya umoja wa kitaifa Zanzibar,Mh. Hamad Rashid (mbunge) katika mdahalo uliofanyika katika hoteli ya movepick ulioandaliwa na vox media iliyo chini ya anserb ngurumo wa Gazeti la Tanzania Daima na kushirikiana na east Africa media,alianza kwa kuelezea chanzo cha kupatika serikali za namna hiyo
"…Serikali za umoja wa kitaifa zinatokana na mambo kadhaa,na kubwa ni utashi wa wananchi…" alisema na kutoa mfano "Waingereza conservative(chama cha siasa,uingereza) ambao ni rafiki wa chadema wameungana na liberals ambao sisi ni rafiki zetu vyama ambavyo uhusiano wao ulikuwa mbali sana. libers walikuwa karibu sana labour party kuliko onservative lakini mazingira ya wapiga kura yakawalazimisha ama conservative ama labour party waungane na lbers bahati nzuri makubaliano yakafikiwa libers na conservative wakaunda serikali ya pamoja hiyo ni sababu moja".Alisema na kuendelea, "Lakini ya pili ambayo imeibuka sasa hivi hasa afrika ni machafuko yanapotokea basi watu wanatafuta suluhu wanafika pahala wakasema maisha ya watu yamepotea hebu tuangalie mbele, watu wanaungana. Kwa mazingira ya Zanzibar ambayo chanzo chake na chimbuko lake ni migogoro ya kisiasa iliyotokea kabla ya hata kubenea hajazaliwa ilisababisha tufike pahala tuseme the way forward ni ipi? tutaendelea na mgogoro huu ili maisha ya watu yapotee? au tutafute njia muafaka ambayo tutafanya. Kwa hiyo tuliingia sisi katika makubaliano ya muafaka wa kwanza, wa pili na wa tatu." Akiendelea kufafanua alisema" kwahivyo kwamba katika kutafuta suluhu na katika kuwafanya watanzania na wazanzibar waishi pamoja basi ilikuwa ni lazima ipatikane njia ya kuwashirikisha kila upande ili tuingie serikalini hiyo ndio sababu kubwa wala hiyo haina unafiki kama vile libers na conservative hawajapoteza muelekeo wao, bado wameshirikiana katika mambo ya msingi wanaokubaliana. Kwa hiyo kwa utaratibu huo mnaunda tu programu ya pamoja ambayo kila chama itaikubali, hatimaye mnasema tunakwenda kutekeleza katiba hiyo kwa wananchi, ndicho kilichotokea hata Zanzibar hivi sasa. Kwahiyo si tatizo na hasa linapotokea kwa maamuzi ya wananchi wenyewe.Na hili ndo la msingi kubwa sana, kwamba wazanzibar wenyewe walipiga kura ya asilimia 64.8 hili ndio la kuzingatia kwamba sisi katika vyama mategemeo yetu ni maamuzi ya wananchi si maamuzi ya vyama vyenyewe,maamuzi ya wananchi ndo yanayotupelekea kufikia maamuzi na mifano kama hiyo niliyoitoa",alimalizia mh Hamad Rashid
 
Na hili ndo la msingi kubwa sana, kwamba wazanzibar wenyewe walipiga kura ya asilimia 64.8 hili ndio la kuzingatia kwamba sisi katika vyama mategemeo yetu ni maamuzi ya wananchi si maamuzi ya vyama vyenyewe,maamuzi ya wananchi ndo yanayotupelekea kufikia maamuzi na mifano kama hiyo niliyoitoa"[/I],alimalizia mh Hamad Rashid
Hizo kura zilichakachuliwa, sio maamuzi ya wananchi ni maamuzi ya viongozi kwa maslahi yao. Ukitaka kuamini hilo angalia ule uchaguzi wa marudio wa yale majimbo matatu ya pemba, hali haikuwa shwari kabisa kulikuwa na uhasama mkubwa kati ya wananchi (CCM&CUF members) na ilipelekea hata ngumi kupigwa mpaka alipokuja FFU ndio kidogo hali ikatulia, hii inaashiria kabisa kwa wananchi hasa wa pemba bado kuna tatizo na hawajarizika, kasoro hamad rashid, seif na duni haji ambao sasa wanakula bata ndio walio rizika
 
Kawaida Serikali za mseto katika mazingira ya kiafrika ni namna ya kutimiza ndoto za kuwa sehemu ya utawala bila kujali maslahi ya wananchi.
Ni mbinu ya Vyama tawala kutawala daima.
Jawabu halikuwa kuungana bali kuweka mazingira huru na haki ya uchaguzi mfano katiba huru na tume huru ya uchaguzi.
Mfano CUF imekuwa ikishinda na kupokwa ushindi kila mara (kama wanavyodai kwa ushaihidi). Kumbe tume huru na katiba mpya vingewezesha wananchi wakachagua na kupata viongozi wanaowataka.
Dawa sio kuungana na kukata tamaa.
 
Kawaida Serikali za mseto katika mazingira ya kiafrika ni namna ya kutimiza ndoto za kuwa sehemu ya utawala bila kujali maslahi ya wananchi.
Ni mbinu ya Vyama tawala kutawala daima.
Jawabu halikuwa kuungana bali kuweka mazingira huru na haki ya uchaguzi mfano katiba huru na tume huru ya uchaguzi.
Mfano CUF imekuwa ikishinda na kupokwa ushindi kila mara (kama wanavyodai kwa ushaihidi). Kumbe tume huru na katiba mpya vingewezesha wananchi wakachagua na kupata viongozi wanaowataka.
Dawa sio kuungana na kukata tamaa.
 
Hamad..............+............................kufu..............................+..........................sisiem.........................................majambazi
 
Hamad Rashid + CUF + CCM wanakosea wanaposema serikali ya kitaifa kwa sababu Zanzibar ni sehemu ya taifa linaloitwa Tanzania; Zanzibar si taifa. Vinginevyo muungano wa iliyokuwa Tanganyika(sasa Tanzania Bara) na Zanzibar utakuwa umevunjwa.

CUF wameungana na CCM kuunda serikali ya pamoja kwa sababu ya uchu wa madaraka waliokuwa nao viongozi wa CUF. Hamad anaposema eti mazingira ya uchaguzi na matokeo yaliyokaribiana ndiyo sababu ya kuundwa kwa serikali ya pamoja anadanganya. Ushindi hata ukiwa wa zaidi ya 50% ya kura zote halali ni sahihi kwa chama hicho kuunda serikali. Hao CUF walipata asilimia 49.1% walipaswa kuunda kambi ya upinzani ili dhana ya mfumo wa vyama vingi ionekane kama katiba ya Jamhuri ya muungano wa Tanzania ambayo inajumuisha zanzibar inavyotamka bayana kuwa Tanzania ni nchi ya Mfumo wa vyama vingi vya siasa. CUF walipaswa kudai tume huru ya uchaguzi na si kukimbilia madaraka yasiyo na nguvu.

Ni vema CDM wakaendelea na msimamo wa kutoishirikisha CUF ktk kambi ya upinzani kwa sababu wao(CUF) ni sehemu ya serikali
 
Walipokuwa hawajaahidiwa madaraka walisema wameibiwa au wamepokwa ushindi lakini walipoahidiwa madaraka Maalim Seif Sharif HAmad amewaita hadi viongozi wa vitongoji wa CCM B kusisitiza eti uchaguzi ulikuwa poa na matokeo yalikuwa sawa moja kwa moja unapata jibu hawa jamaa ni waroho wa madaraka Prof Lipumba asiyejua kusoma lama za Nyakati anaachwa taaratibu solemba ataendelea kusema yeye mlima kilimanjaro mkwere anasonga na wazanzibar wanamwaga

Idumu CCM B
 
HAMADI unachosema ni unafiki tu. Serikali ya mseto ni matokeo ya tamaa ya madaraka. waliopo madarakani hawapo tayari kuondoka hata kama wameshindwa kwenye uchaguzi na wapinzani nao hawako tayari kushindwa hata kama wameshindwa kweli. Matokeo yake mnaamua kugawana ulaji kwa kisingizio cha matakwa ya wananchi. WANASIASA MNA DHAMBI YA MAUTI.
 
Serikali ya kitaifa zanzibar imetokana na machafuko yaliyotokea pemba, si sawa na kuilinganisha na ya uingereza. Kule uingereza hakuna chama kilichoshinda hivyo ilibidi vyama ngalau viwili viungane iliviwe na wingi wa viti. Kwa Zanzibar siyo hivyo, kama matokeo ya uchaguzi yaliyotangazwa ndiyo sahihi basi ccm ilishinda na haikuwa lazima kushirikiana na chama kingine, lakini yale machafuko ya pemba yamekilazimisha kiwaingize serikalini CUF ili yasitokee. Hakika hii ni kuua malengo ya vyama vingi, na kwa mtido huu CUF mtaendelea kushirikishwa tu. Nakubaliana na aliyesema,dawa ingekuwa ni kuunda tume huru ya uchaguzi na ikaendesha uchaguzi huru.
Kama mlivyoona CUF wamepigwa changa la macho maana makamu wa kwanza warais zanzibar hana mamlaka badala yake makamu wa pili ndiye mwenye mamlaka.
 
Back
Top Bottom