Luteni
JF-Expert Member
- Jan 9, 2010
- 2,274
- 301
Tofauti na chaguzi zilizopita ukiachilia ule wa kwanza 1995 CCM imeonyesha kuwa na wasiwasi wa hali ya juu kufanya hata waliokuwa hawafuatilii mambo ya uchaguzi kuanza kujiuliza kulikoni.
Maswali haya wanayojiuliza wananchi ni kutokana na CCM kuacha misingi iliyowapatia heshima na kuanza kufanya yale yaliyokuwa yanatazamiwa yafanywe na wapinzani.
Ukweli usiopingika ingawa CCM inadai wapinzani wanatumia lugha zisizo za ustaarabu lakini CCM itakuwa ya kwanza kulaumiwa kwa kukumbatia vitendo hivyo ikiongozwa na Katibu wake mkuu.
Kitendo kingine kinachoonyesha CCM kuwa na hofu ni kuanza kutumia vyombo vya habari vikiwemo vya umma kukifanyia kampeni za waziwazi, heri zingekuwa za ustaarabu lakini ni kampeni za kuchafuana.
Inasemekana kuna baadhi ya magazeti yameelekezwa na baadhi ya viongozi wa CCM yagawiwe bure kwa lengo la kuwachafua baadhi ya wapinzani wanaoonekana kuisumbua, hii yote ni kielelezo tosha cha hofu waliyonayo.
Hofu nyingine inatokana labda na udhaifu alionao mgombea wake Jakaya Kikwete ikiwemo afya yake dhidi ya mgombea machachari wa Chadema Dr. Slaa, inawezekana CCM hawakutarajia kuwa Dr. Slaa atachukua fomu ya kugombea urais mwaka huu, ni hofu.
Inawezekana pia hofu nyingine inasababishwa na CCM kutokuwa na majibu ya watuhumiwa wa ufisadi List of Shame. Huenda baada ya CCM kukosa majibu yake ndiyo maana imeamua kujiingiza kwenye vitendo vya kushambulia mtu badala ya kujibu tuhuma, ni hofu.
Mwaka huu Chadema imeweka wagombea karibu asilimia 80 ya majimbo yote na CUF karibu asilimia 60 ya majimbo yote na kufanya upinzani kuvunja rekodi ya kuwafikia watanzania wengi. Hii nayo inaweza kuongeza hofu ndani ya CCM.
Hofu nyingine inatokana na kukua kwa uelewa wa wananchi kwa dhana nzima ya upinzani kuwa si uadui tofauti na chaguzi zilizopita na hasa ujio wa kizazi kipya ambacho hakikushiriki uchaguzi wa 1995, ni hofu.
Hofu hizi zinadhihirishwa na mikutano ya ndani ya CCM inayofanyika usiku na mchana kwenye maeneo tofauti nchini hasa Dar es salaam kwa kubadilisha venue (Hotel) mara kwa mara, ni HOFU.
JE ni nini unafikiri CCM inahofia juu ya hatima ya uchaguzi huu au kwanini unafikiri isiwe na hofu.
Naomba kuwasilisha,
Luteni.
Maswali haya wanayojiuliza wananchi ni kutokana na CCM kuacha misingi iliyowapatia heshima na kuanza kufanya yale yaliyokuwa yanatazamiwa yafanywe na wapinzani.
Ukweli usiopingika ingawa CCM inadai wapinzani wanatumia lugha zisizo za ustaarabu lakini CCM itakuwa ya kwanza kulaumiwa kwa kukumbatia vitendo hivyo ikiongozwa na Katibu wake mkuu.
Kitendo kingine kinachoonyesha CCM kuwa na hofu ni kuanza kutumia vyombo vya habari vikiwemo vya umma kukifanyia kampeni za waziwazi, heri zingekuwa za ustaarabu lakini ni kampeni za kuchafuana.
Inasemekana kuna baadhi ya magazeti yameelekezwa na baadhi ya viongozi wa CCM yagawiwe bure kwa lengo la kuwachafua baadhi ya wapinzani wanaoonekana kuisumbua, hii yote ni kielelezo tosha cha hofu waliyonayo.
Hofu nyingine inatokana labda na udhaifu alionao mgombea wake Jakaya Kikwete ikiwemo afya yake dhidi ya mgombea machachari wa Chadema Dr. Slaa, inawezekana CCM hawakutarajia kuwa Dr. Slaa atachukua fomu ya kugombea urais mwaka huu, ni hofu.
Inawezekana pia hofu nyingine inasababishwa na CCM kutokuwa na majibu ya watuhumiwa wa ufisadi List of Shame. Huenda baada ya CCM kukosa majibu yake ndiyo maana imeamua kujiingiza kwenye vitendo vya kushambulia mtu badala ya kujibu tuhuma, ni hofu.
Mwaka huu Chadema imeweka wagombea karibu asilimia 80 ya majimbo yote na CUF karibu asilimia 60 ya majimbo yote na kufanya upinzani kuvunja rekodi ya kuwafikia watanzania wengi. Hii nayo inaweza kuongeza hofu ndani ya CCM.
Hofu nyingine inatokana na kukua kwa uelewa wa wananchi kwa dhana nzima ya upinzani kuwa si uadui tofauti na chaguzi zilizopita na hasa ujio wa kizazi kipya ambacho hakikushiriki uchaguzi wa 1995, ni hofu.
Hofu hizi zinadhihirishwa na mikutano ya ndani ya CCM inayofanyika usiku na mchana kwenye maeneo tofauti nchini hasa Dar es salaam kwa kubadilisha venue (Hotel) mara kwa mara, ni HOFU.
JE ni nini unafikiri CCM inahofia juu ya hatima ya uchaguzi huu au kwanini unafikiri isiwe na hofu.
Naomba kuwasilisha,
Luteni.