Elections 2010 Kwa nini CCM ina HOFU

Luteni

JF-Expert Member
Jan 9, 2010
2,274
301
Tofauti na chaguzi zilizopita ukiachilia ule wa kwanza 1995 CCM imeonyesha kuwa na wasiwasi wa hali ya juu kufanya hata waliokuwa hawafuatilii mambo ya uchaguzi kuanza kujiuliza kulikoni.

Maswali haya wanayojiuliza wananchi ni kutokana na CCM kuacha misingi iliyowapatia heshima na kuanza kufanya yale yaliyokuwa yanatazamiwa yafanywe na wapinzani.

Ukweli usiopingika ingawa CCM inadai wapinzani wanatumia lugha zisizo za ustaarabu lakini CCM itakuwa ya kwanza kulaumiwa kwa kukumbatia vitendo hivyo ikiongozwa na Katibu wake mkuu.

Kitendo kingine kinachoonyesha CCM kuwa na hofu ni kuanza kutumia vyombo vya habari vikiwemo vya umma kukifanyia kampeni za waziwazi, heri zingekuwa za ustaarabu lakini ni kampeni za kuchafuana.

Inasemekana kuna baadhi ya magazeti yameelekezwa na baadhi ya viongozi wa CCM yagawiwe bure kwa lengo la kuwachafua baadhi ya wapinzani wanaoonekana kuisumbua, hii yote ni kielelezo tosha cha hofu waliyonayo.

Hofu nyingine inatokana labda na udhaifu alionao mgombea wake Jakaya Kikwete ikiwemo afya yake dhidi ya mgombea machachari wa Chadema Dr. Slaa, inawezekana CCM hawakutarajia kuwa Dr. Slaa atachukua fomu ya kugombea urais mwaka huu, ni hofu.

Inawezekana pia hofu nyingine inasababishwa na CCM kutokuwa na majibu ya watuhumiwa wa ufisadi List of Shame. Huenda baada ya CCM kukosa majibu yake ndiyo maana imeamua kujiingiza kwenye vitendo vya kushambulia mtu badala ya kujibu tuhuma, ni hofu.

Mwaka huu Chadema imeweka wagombea karibu asilimia 80 ya majimbo yote na CUF karibu asilimia 60 ya majimbo yote na kufanya upinzani kuvunja rekodi ya kuwafikia watanzania wengi. Hii nayo inaweza kuongeza hofu ndani ya CCM.

Hofu nyingine inatokana na kukua kwa uelewa wa wananchi kwa dhana nzima ya upinzani kuwa si uadui tofauti na chaguzi zilizopita na hasa ujio wa kizazi kipya ambacho hakikushiriki uchaguzi wa 1995, ni hofu.

Hofu hizi zinadhihirishwa na mikutano ya ndani ya CCM inayofanyika usiku na mchana kwenye maeneo tofauti nchini hasa Dar es salaam kwa kubadilisha venue (Hotel) mara kwa mara, ni HOFU.

JE ni nini unafikiri CCM inahofia juu ya hatima ya uchaguzi huu au kwanini unafikiri isiwe na hofu.

Naomba kuwasilisha,

Luteni.
 
Mfalme wa dhambi anaogopa kuondoka madarakani maana atavuliwea nguo; lazima ajifiche na ajiimarishe ili asivuliwe nguo; CCM hawawezi kumuachia Dr Slaa nchi wanajua atakalofanya litawavua nguo maana walishajivua kwa matendo ila wanajua kuyaficha ndio njia sahihi; hofu inatokana na hilo la kuvuliwa nguo
 
Mfalme wa dhambi anaogopa kuondoka madarakani maana atavuliwea nguo; lazima ajifiche na ajiimarishe ili asivuliwe nguo; CCM hawawezi kumuachia Dr Slaa nchi wanajua atakalofanya litawavua nguo maana walishajivua kwa matendo ila wanajua kuyaficha ndio njia sahihi; hofu inatokana na hilo la kuvuliwa nguo
Kama hofu ni kuvuliwa nguo ina maana watatawala milele!
 
Luteni umesahau kusema ni kwa nini vyombo vya umma vya usalama pia vinahaha?
 
Luteni umesahau kusema ni kwa nini vyombo vya umma vya usalama pia vinahaha?
Asante MF kwa kunikumbusha ndio maana pale mwisho nikaachia wanaJF nao waziseme hofu, UWT wamejaa humu kweli hii nayo inadhihirisha hofu.
 
Kama haina hofu kwa nini kwa mara ya kwanza imeruhusu magazeti ya umma kufanya kampeni chafu tena waziwazi refer Habari Leo, tofautisha gazeti kuwa bias na kuandika kashifa za mgombea mwingine.

Mkuu, Hayo magazeti yalifanya hivyo hivyo 95, 2000, 2005? unashangaa nini leo 2010?

Nimekuuliza wameandika kashfa ipi? kuna tofauti kati ya kashfa na ukweli...mathalan, kusema Slaa ni mtaalamu wa kanuni za kanisa siyo kashfa ni ukweli! au siyo. Kusema Slaa amemuacha mke wake na yuko na mke wa mtu ni ukweli si kashfa au siyo..nk..kwakuwa wewe ni mpenzi wa Chadema unaumia sisi tunafurahi kwasababu jamaa si muadilifu na hafai kuwa rais

Wananchi wanahitaji kumfahamu mgombea wa urais ndio maana magazeti ya serikali yameandika huo ukweli!
 
ccm hofu wanayo sana tena sana kwani kwa asilimia kubwa wadanganyika wameaanza kutoka usingizini wanajua pumba na mchele so wapo kwenye wakati mgumu
 
Hizo Pesa CCM walizonazo kwa Uchaguzi kama wangeziweka kwenye Maendeleo ya Nchi nadhani wangetawala ka Karne Nzima
Mfano Masha ana Pesa lakini hajafanyia kitu chochote Nyamagana; angalia anapendekeza Uwanja wa Nyamagana Mwanza the only Stadium usio na makucha ya CCM mkoani kuuzwa kwa watu sio wazalendo; yaani wamesahau historia ya Uwanja Wa Mpira Wa Nyamagana - anyway Lau Hajui historia ya Mwanza... Hakukulia Mji wetu wa Miamba

Nina Uchungu hata kama niko nje ya Nchi...
 
Mkuu, Hayo magazeti yalifanya hivyo hivyo 95, 2000, 2005? unashangaa nini leo 2010?

Nimekuuliza wameandika kashfa ipi? kuna tofauti kati ya kashfa na ukweli...mathalan, kusema Slaa ni mtaalamu wa kanuni za kanisa siyo kashfa ni ukweli! au siyo. Kusema Slaa amemuacha mke wake na yuko na mke wa mtu ni ukweli si kashfa au siyo..nk..kwakuwa wewe ni mpenzi wa Chadema unaumia sisi tunafurahi kwasababu jamaa si muadilifu na hafai kuwa rais

Wananchi wanahitaji kumfahamu mgombea wa urais ndio maana magazeti ya serikali yameandika huo ukweli!
Nimesema kuna tofauti ya magazeti kuwa bias na kuandika kashifa, mfano gazeti kuandika mikutano ya chama kimoja hiyo si kashifa ni kuwa bias lakini gazeti tena la serikali kuandika maisha ya ndani ya mgombea wa upande mmoja hiyo ndiyo kashifa.

Asante kwa kuwa muwazi kuwa unafurahia hizi kashifa kwa vile tu wewe si Chadema.
 
Asante MF kwa kunikumbusha ndio maana pale mwisho nikaachia wanaJF nao waziseme hofu, UWT wamejaa humu kweli hii nayo inadhihirisha hofu.
Si humu tu wanatukela hata huku mitaani as if wao ndio watamchagua rais wa nchi hii peke yao au as if nchi hii ni personal property yao!
 
hofu inatokana kupata utambuzi kuwa tanzania bila ccm inawezekana; ccm bila tanzania haiwezekani; na ufisadi wao bila ccm hauwezekani.
 
Mkuu, Hayo magazeti yalifanya hivyo hivyo 95, 2000, 2005? unashangaa nini leo 2010?

Nimekuuliza wameandika kashfa ipi? kuna tofauti kati ya kashfa na ukweli...mathalan, kusema Slaa ni mtaalamu wa kanuni za kanisa siyo kashfa ni ukweli! au siyo. Kusema Slaa amemuacha mke wake na yuko na mke wa mtu ni ukweli si kashfa au siyo..nk..kwakuwa wewe ni mpenzi wa Chadema unaumia sisi tunafurahi kwasababu jamaa si muadilifu na hafai kuwa rais

Wananchi wanahitaji kumfahamu mgombea wa urais ndio maana magazeti ya serikali yameandika huo ukweli!

Vile vile wananchi wanahitaji kufahamu kwamba kina Mkapa, JK, Lowassa na Rostam walikwapua hela za EPA na Marando anasema ana ushahidi. Sasa CCM kupitia kwa Kinana wanalalama nini kuhusu Chadema? Ukweli ni ukweli. Mkuki kwa nguruwe.
 
Kwanini wasiwe na hofu wakati hawana uhakiwa wa mgombea wao kufikisha roundi 12, afya bwana ndiyo hofu kuu.
 
Mkuu, Hayo magazeti yalifanya hivyo hivyo 95, 2000, 2005? unashangaa nini leo 2010?

Nimekuuliza wameandika kashfa ipi? kuna tofauti kati ya kashfa na ukweli...mathalan, kusema Slaa ni mtaalamu wa kanuni za kanisa siyo kashfa ni ukweli! au siyo. Kusema Slaa amemuacha mke wake na yuko na mke wa mtu ni ukweli si kashfa au siyo..nk..kwakuwa wewe ni mpenzi wa Chadema unaumia sisi tunafurahi kwasababu jamaa si muadilifu na hafai kuwa rais

Wananchi wanahitaji kumfahamu mgombea wa urais ndio maana magazeti ya serikali yameandika huo ukweli!

Mtumwa wa mafisadi; na vyombo vyao; ukweli hupimwa mahakamani au kwa kuuliza wahusika wote; mbona vyombo havikumuuliza mhusika wa upande wa pili maan ayuko Singida na Mmewe; umesoma sawa na maprofesa kibao wajinga kabisa maanake elimu haijawakomboa; lazima ujue lengo la chombo cha habari; sio unaongea upupu hapa; taarifa bila balance ni udaku; ndio maana anatamba tanzania kwa kusema ana vyombo vya udaku wispering News media yaani habari zilizochakachuliwa; hata wenye akili waziishi hizo au sio utupu na machukizo machoni mwao; wewe unaweza kuwa uko upande wa pili
 
Mkuu, Hayo magazeti yalifanya hivyo hivyo 95, 2000, 2005? unashangaa nini leo 2010?

Nimekuuliza wameandika kashfa ipi? kuna tofauti kati ya kashfa na ukweli...mathalan, kusema Slaa ni mtaalamu wa kanuni za kanisa siyo kashfa ni ukweli! au siyo. Kusema Slaa amemuacha mke wake na yuko na mke wa mtu ni ukweli si kashfa au siyo..nk..kwakuwa wewe ni mpenzi wa Chadema unaumia sisi tunafurahi kwasababu jamaa si muadilifu na hafai kuwa rais

Wananchi wanahitaji kumfahamu mgombea wa urais ndio maana magazeti ya serikali yameandika huo ukweli!
JK ndiyo msafi?
 
Mkuu, Hayo magazeti yalifanya hivyo hivyo 95, 2000, 2005? unashangaa nini leo 2010?

Nimekuuliza wameandika kashfa ipi? kuna tofauti kati ya kashfa na ukweli...mathalan, kusema Slaa ni mtaalamu wa kanuni za kanisa siyo kashfa ni ukweli! au siyo. Kusema Slaa amemuacha mke wake na yuko na mke wa mtu ni ukweli si kashfa au siyo..nk..kwakuwa wewe ni mpenzi wa Chadema unaumia sisi tunafurahi kwasababu jamaa si muadilifu na hafai kuwa rais

Wananchi wanahitaji kumfahamu mgombea wa urais ndio maana magazeti ya serikali yameandika huo ukweli![/QUOTE]

Mimi ni mwananchi si zaidi yako labda. Umeamua kuhamisha mjadala wa sera za kutuletea maendeleo na kutupeleka kuzungumzia events na watu (people) hadi kuwasemea "Wananchi" ambao unawa"exploit" kwa kuwasababishia umasikini na ujinga. Nina uhakika dhamira yako sio safi kama sio kwa bahati mbaya hujaishi na hao wananchi wanaokugharimia kuwasaliti. Pole sidanganyiki kuzungumzia maisha ya mtu. Nashawishika kuzungumzia kazi nzuri njema zenye tija na ushahidi za Dr. Slaa kwa nchi yetu badala ya CCM ambao mgombea wao wa uraisi Jakaya Mrisho Kikwete hajui kwa nini Watanzania ni masikini. Nadhani hata wewe si ajabu hujui kwa nini Watanzania ni Masikini kama raisi wako ndio maana unatetea upuuzi.
 
Ina mgombea dhaifu kikwete ambay serikali yake ilitegemea kwa kiasi kikubwa dr.slaa atasema nini...kwa maana nyingine kwa wale waelewa wanajua jinsi slaa alivyomsaidia kikwete kuongoza nchi indirectly kutokana na ujasili wake uliotukuka......hii ndiyo hofu kubwa kuwa wananchi wanajua mchango mkubwa wa slaa kwa hiyo kuna kila dalili kuwa kikwete kura haziwezi kamwe kumtosha labda waendee kuchakachua kama walivyofanya mbeya..........
 
Hi mimi baba; jakaya uadilifu wake uko wapi? Mademu kila kona tanzania na nchi za nje?
 
Back
Top Bottom