Mara nyingi huwa naona kama kuna traffic jam magari ya askari polisi, magereza na JWTZ (na hata yanye namba zinazoanza na a ST, SU) wakitanua lakini magari ya raia yakitanua yanakamatwa. Jana jioni kama saa 2 usiku hivi karibu tugongane na gari la JWTZ kati ya Matumbi na Tabata maana baada ya kuona foleni upande wao (kutoea Buguruni kuelekea Ubungo) haiendi wakaamua kupita sehemu yetu (sisi tulikuwa tukielekea Buguruni kutokea maeneo ya Tabata) na kama kawaida yao huwa hawampishi mtu. Leo asubuhi pia niliona kitu cha aina ileile? Hivi mara zote huwa kuna emergency ya kuwafanya wafanye hivyo au huwa ni kwa vile wanajiona wako juu ya sheria? Nchi nyingine hata hapa Afrika askari wako mstari wa mbele kufuata sheria lakini hapa kwetu naona wako nyuma sana. Je, ndivyo wanavyofundishwa au wanatumia mwanya huu ambao "anything goes"?