Kwa nilichokiona na kukisikia leo nathibitisha rasmi kuwa Tanzania hatuna 'Critical Journalists' bali tuna 'PR and Round Table Journalists' tu

Ningeuliza hivi:
Tangu awamu ya sita imeingia madarakani chini ya uongozi wako, tumeshuhudia ukisisitiza juu ya umuhimu wa kuchukua hatua juu ya ugonjwa wa COVID, na hata hapa leo umetuambia juu ya hilo na uwepo wa wagonjwa wa COVID nchini na mipango ya serikali kuleta chanjo. Pia, umekuwa ukisisitiza Watanzania kuchukua hatua za kujilinda ikiwemo kupunguza misongamano isiyo ya lazima. Lakini, hivi karibuni tumeshuhudia ukimpigia simu mwanamuziki aliekua anatumbuiza usiku kwenye tamasha la muziki, na ukisema unatamani ungekwepo pale huku ukipongeza tamasha hilo. Je, kwa kitendo hicho huoni kuwa unachanganya wananchi kama kiongozi namba moja wa Serikali?
Au unadhani kuwa tamasha lile na matamasha ya aina ile ni moja ya misongamano muhimu isiyokwepeka?Huoni kama kwa hatua ile ume-endorse muendelezo wa mikusanyiko ya muziki katika kipindi hiki ambacho unatusisitiza tuepuke misongamano isiyo ya lazima?
Kipi ni kipi?
Hii ni awamu ya tano katika kipindi chake cha pili cha miaka Kumi !!. Awamu ya sita itaanza baada ya awamu hii ya tano kufikia ukomo wake... October 2025. Vingenevyo swali lako lingemtoa kwenye reli.
 
Ukiona anayehojiwa au Kuulizwa Maswali anayajibu kwa Furaha, hatetemeki, anatingisha Miguu yake kama yupo Sebuleni Kwake na Familia yake, hatokwi na Jasho, hapandwi na Hasira mpaka anadiriki kuomba maswali ya Nyongeza huku akiishia Kuwakaribisha Chakula ili mvimbiwe vizuri kwa Uroho wenu jua waliopo ( wanaomuhoji ) ni bure kabisa na anayehojiwa nae ameshawadharau halafu anawamudu pia hawamtishi.

Nimesikitika sana tu kwa nilichokiona.
Nafikiri bado kuna kitu hakipo sawa, wanatesti mitambo, kuna uvumi unasema msitu ni mpya komba ni wale wale.....
 
Mkuu mbona hili linajukana kabisa!! Halafu mkutano ulivyoandaliwa siyo kwa kitaalam kabisa. Mkutano kama huu unakuwa na follow up questions, na rais angejibu eg maswali matatu, matatu. Hili la kuuliza maswali yote kwa pamoja halafu rais ndiyo ajibu kuna kitu kinakwepwa. Kuhusu hili la ''waandishi'' wa Tanzania hilo wala lisikusumbue. Wenyewe walikwenda kulilia maslahi yao na kusifu ili wafikiriwe kwenye safari za nje. Kama huyo sijui Balile, huyo jamaa anachojua ni tumbo lake tu.
Huyo Balile anajulikana ni mlamba mata.ko maarufu, hakuna anachosimamia zaidi ya maslahi yake binafsi.
 
Ningeuliza hivi:
Tangu awamu ya sita imeingia madarakani chini ya uongozi wako, tumeshuhudia ukisisitiza juu ya umuhimu wa kuchukua hatua juu ya ugonjwa wa COVID, na hata hapa leo umetuambia juu ya hilo na uwepo wa wagonjwa wa COVID nchini na mipango ya serikali kuleta chanjo. Pia, umekuwa ukisisitiza Watanzania kuchukua hatua za kujilinda ikiwemo kupunguza misongamano isiyo ya lazima. Lakini, hivi karibuni tumeshuhudia ukimpigia simu mwanamuziki aliekua anatumbuiza usiku kwenye tamasha la muziki, na ukisema unatamani ungekwepo pale huku ukipongeza tamasha hilo. Je, kwa kitendo hicho huoni kuwa unachanganya wananchi kama kiongozi namba moja wa Serikali?
Au unadhani kuwa tamasha lile na matamasha ya aina ile ni moja ya misongamano muhimu isiyokwepeka?Huoni kama kwa hatua ile ume-endorse muendelezo wa mikusanyiko ya muziki katika kipindi hiki ambacho unatusisitiza tuepuke misongamano isiyo ya lazima?
Kipi ni kipi?
You are very brave & wise.
Mungu akubariki sana.
 
Mimi ningeuliza hivi:
1. Mheshimiwa, sehemu kubwa ya taarifa za vyombo vya habari ni malalamiko ya vijana kuhusu ukosefu wa ajira. Je, utaratibu ukoje wa Serikali wa kutoa ajira, ni wa moja kwa moja au ni wa kupitia mahojiano? (Interview)
Kama ni wa moja kwa moja, ufanisi wa waajiriwa katika sehemu wanazopangiwa mnautambuaje?
 
1.Awamu iliyopita tulishuhudia kila mwezi ikitoa takwimu za makusanyo kupitia TRA ambapo ni kigezo mojawapo cha uwazi ktk utendaji wa serikali.Nini kinakwamisha utolewaji wa takwimu hizo awamu hii?

2. Siku unapokea report ya CAG na TAKUKURU mwezi march uliagiza uchunguzi wa haraka ufanyike fedha zote zilizotolewa hazina kuanzia January hadi march,lakjni mpaka Leo mwezi wa tatu tangu umeagiza tunaona kimya.

3.Report ya CAG ilibainisha shirika la ndege la ATCL limekua likijiendesha kwa hasara,wakati huo huku bado waziri mkuu akitwambia bado kuna ndege kadhaa zitakuja ili kukamilisha idadi flani hauoni kama kutakua ni kuendeleza hasara?

4.Kwa miaka kadhaa serikali iliyopita wewe ukiwa makamu wake mmekua mkituaminisha kwamba tutembee kifua mbele tuko kwenye right track kiasi ambapo hata kipindi cha wimbi la kwanza la ugonjwa wa uviko tulihakikishiwa kwamba tuna dola reserve za kutosha kuendesha nchi kwa zaidi ya miezi 6 bila kuzalisha,nini kinakwamisha ajira mpya za kutosha ili kuongeza mzunguko wa fedha mtaani(multiplying effect).?

5.Siku ya kongamano UDOM ulikaririwa ukisema wewe na magufuli ni kitu kimoja,MAGUFULI alisema yeye kwake katiba mpya sio kipaumbele na wala katika kampeni zake hakuna alipoinadi,ni UPI msimamo wako juu ya takwa la katiba mpya.

6. Serikali iliyopita wewe ukiwa kama makamu tuliambiwa gas ni yetu lakini kutokana na masharti ya mkataba sisi tunapewa asilimia kidogo ambazo pia zimeshindwa kumaliza tatizo la uhaba wa umeme nchini,lakini juzi ukiwa kenya umekaririwa ukisema tuatanza kuwauzia gas Kenya,INA maana gas ya kuuza ipo lakini ya kuzalisha umeme wa kutosha na kulisha viwanda vyetu hatimae viweze kushindana kibiashara Africa ndo haitoshi.

7.Awamu iliyopita wewe ukiwa makamu tumeshuhudia uvunjwaji mkubwa wa haki za binadamu hadi kuibuka kwa msemo wa wawatu wasiojulikana,umejipangaje kuhakikisha hao waliokua hawajulikani wanajulikana na sheria inachukuliwa dhidi yao.

8.........naendelea kuload maswali mengine Bahat mbaya kadri navofikia hitimisho naona ndivo maswali konk yanazd kuload kichwani.
 
Kusema ukweli waandishi wawili au watatu tu ndio wameuliza maswali ya msingi kidogo, wengine wameuliza maswali ya kitoto sana hasa wale wanaotoka TBC na yule sijui wa redio tumaini. Yule dada wa redio ujerumani na mwingine aliyeuliza katiba mpya na mikutano ya kisiasa kuruhusiwa at least wameuliza maswali ya maana. Tanzania hatuna waandishi wa habari, kichwani weupe sana.
Angalia hata vyombo vya habari vyenyewe vilivyo dhofu mbaya! Hao walijitahidi kuuliza maswali yenye afadhali si unaona na vyombo vyao! "Vyombo vinaamua ubora wa watenda kazi.
Sionagi hata haja ya viongozi kutoa mawsali kwa wanahabari wanaowahoji.
Miongozo na sheria sahihi huzaa uchumi imara.
 
Back
Top Bottom