Kiongozi wa Upinzani Nchini Na Katibu Mkuu wa chama kikuu cha upinzani nchini-CHADEMA Dr Wilbroad Slaa amesema ameshangazwa na uamuzi wa CCM kupitisha majina ya watuhumia wakuu wa ufisadi nchini kugombea nafasi mbalimbali ndani ya chama hicho ukiwemo ujumbe wa Halmashauri kuu ya Taifa CCM-NEC.
Kiongozi huyo machachari nchini amesema hayo yote yamefanywa na CCM licha ya kelele za wananchi kote nchini kulaani ufisadi uliofanywa na watu hao na pia CCM kuizika kauli yake ya kujivua Gamba na kuwaondoa watuhumiwa wa ufisadi.
Hata hivyo Dr Slaa amesema hiyo ni furaha kubwa kwake na chama chake kwani kwa hali hiyo CCM imejizika yenyewe kwani wananchi kamwe hawawezi kukubali kuongozwa tena na chama kinachokumbatia ufisadi kwa viwango hivyo.
Source: Nipashe na Tanzania Daima.
Kiongozi huyo machachari nchini amesema hayo yote yamefanywa na CCM licha ya kelele za wananchi kote nchini kulaani ufisadi uliofanywa na watu hao na pia CCM kuizika kauli yake ya kujivua Gamba na kuwaondoa watuhumiwa wa ufisadi.
Hata hivyo Dr Slaa amesema hiyo ni furaha kubwa kwake na chama chake kwani kwa hali hiyo CCM imejizika yenyewe kwani wananchi kamwe hawawezi kukubali kuongozwa tena na chama kinachokumbatia ufisadi kwa viwango hivyo.
Source: Nipashe na Tanzania Daima.