Salary Slip
JF-Expert Member
- Apr 3, 2012
- 47,013
- 144,371
Kwa haya yanayoendelea hapa nchini na ambayo pia yanaripotiwa na vyombo vya habari vya kimataifa, sitarajii kama kuna mfanyabiashara mwenye kujielewa atavutiwa kuja kuwekeza katika hii nchi achilia mbali ile taarifa ya deni la matrilioni tunalowadai acacia deni ambalo litakuwa pia limeshitua wawekezaji wengine.
Hata hawa wafanyabiashara wa ndani tuliowaomba wajenge viwanda ni lazima na watajiulize mara mbili mbili nini kitatokea siku wakipelekana mahakamani na serikali kama wataweza kupata haki au laa.
Kama tunataka mikataba na wawekezaji iwe na vipengele vya kusuluhisha migogoro kwa kutumia mahakama za hapa nchini,basi inabidi tujitafakari upya.
Tusisahau taarifa hizi(bila kujali ni za kweli au laa) zinasambaa dunia nzima na muwekezaji mwenye nia ya kutaka kuwekeza ni lazima atakuwa interested kujua kila kitu kuanzia hali ya kisiasa,kiuchumi,uhuru wa mahakama,n.k.
Hata hawa wafanyabiashara wa ndani tuliowaomba wajenge viwanda ni lazima na watajiulize mara mbili mbili nini kitatokea siku wakipelekana mahakamani na serikali kama wataweza kupata haki au laa.
Kama tunataka mikataba na wawekezaji iwe na vipengele vya kusuluhisha migogoro kwa kutumia mahakama za hapa nchini,basi inabidi tujitafakari upya.
Tusisahau taarifa hizi(bila kujali ni za kweli au laa) zinasambaa dunia nzima na muwekezaji mwenye nia ya kutaka kuwekeza ni lazima atakuwa interested kujua kila kitu kuanzia hali ya kisiasa,kiuchumi,uhuru wa mahakama,n.k.