Course Coordinator
JF-Expert Member
- Jul 27, 2019
- 1,681
- 3,063
Katibu Mkuu wa CHADEMA, John Mnyika ametoa taarifa kwa vyombo vya habari kuwa chama hicho hakijapeleka orodha yoyote ya majina NEC kwa ajili ya uteuzi wa viti maalumu. Lakini NEC inahitaji majina orodha hiyo haraka iwezekanavyo ili iwatangaze, wahudhurie kikao cha kwanza cha bunge jumanne pamoja na kuapishwa.
Kwa kuwa Chadema imekataa kupeleka orodha hiyo, Mnyika amesema NEC inadaiwa kughushi. Yani NEC imeamua kutengeneza orodha "feki" ya wabunge wa viti maalumu wa Chadema, halafu leo usiku kabla ya saa sita itawatangaza ili jumanne wakaape.
SWALI: Kwanini NEC wameamua kufanya uharamia huu?
JIBU: Kila mwaka serikali hupewa $900M (zaidi ya shilingi Trilioni 2) kwa masharti kuwa "oversee committees" za bunge ziongozwe na kambi ya upinzani na kutoa theluthi moja au zaidi ya wajumbe. Kamati hizo ni ya hesabu za Serikali (PAC), kamati ya hesabu za mashirika ya umma (POAC) na kamati ya hesabu za serikali za mitaa (LAAC).
Lakini kuna dalili ya kupoteza fedha hizo kwa sababu hakuna wabunge wa upinzani wa kutosha kuongoza PAC, LAAC wala POAC. Kwahiyo ili tusipoteze fedha hizo inabidi wabunge wa upinzani wapatikane kwa "gharama yoyote"
Na huu ndio msingi wa hoja ya Mnyika kwamba NEC imeamua kughushi majina ya wabunge wa viti maalumu wa Chadema na itawatangaza ili jumanne wakaape. Kwa lugha rahisi ni kwamba serikali ya CCM ilifanya uharamia kwenye uchaguzi bila kujua uharamia huo utakuja kuwagharimu baadae (that's karma).
Sasa wanahaha kuokoa "matrilioni" hayo ya mabeberu. Wanataka kufanya uharamia mwingine wa kutangaza wabunge "feki" wa viti maalumu wa Chadema ili angalau wasipoteze pesa hizo.
Lakini kama uchaguzi ungekua huru na haki, wakapatikana wabunge wengi wa upinzani kuongoza kamati hizo, yote haya yasingetokea. CCM na NEC wasingekua wanahaha muda huu kulazimisha Chadema ipeleke majina ya viti maalumu wala wasingetuhumiwa kutengeneza orodha feki ya wabunge.
Hata hivyo Chadema imeshaweka wazi kuwa haitawatambua wabunge hao hata kama NEC itawatangaza.
Tutaelewana tu huko mbeleni.
Mambo ni fire ...Magufuli na CCM wameishiwa mbinu kisiasa.
Kwa kuwa Chadema imekataa kupeleka orodha hiyo, Mnyika amesema NEC inadaiwa kughushi. Yani NEC imeamua kutengeneza orodha "feki" ya wabunge wa viti maalumu wa Chadema, halafu leo usiku kabla ya saa sita itawatangaza ili jumanne wakaape.
SWALI: Kwanini NEC wameamua kufanya uharamia huu?
JIBU: Kila mwaka serikali hupewa $900M (zaidi ya shilingi Trilioni 2) kwa masharti kuwa "oversee committees" za bunge ziongozwe na kambi ya upinzani na kutoa theluthi moja au zaidi ya wajumbe. Kamati hizo ni ya hesabu za Serikali (PAC), kamati ya hesabu za mashirika ya umma (POAC) na kamati ya hesabu za serikali za mitaa (LAAC).
Lakini kuna dalili ya kupoteza fedha hizo kwa sababu hakuna wabunge wa upinzani wa kutosha kuongoza PAC, LAAC wala POAC. Kwahiyo ili tusipoteze fedha hizo inabidi wabunge wa upinzani wapatikane kwa "gharama yoyote"
Na huu ndio msingi wa hoja ya Mnyika kwamba NEC imeamua kughushi majina ya wabunge wa viti maalumu wa Chadema na itawatangaza ili jumanne wakaape. Kwa lugha rahisi ni kwamba serikali ya CCM ilifanya uharamia kwenye uchaguzi bila kujua uharamia huo utakuja kuwagharimu baadae (that's karma).
Sasa wanahaha kuokoa "matrilioni" hayo ya mabeberu. Wanataka kufanya uharamia mwingine wa kutangaza wabunge "feki" wa viti maalumu wa Chadema ili angalau wasipoteze pesa hizo.
Lakini kama uchaguzi ungekua huru na haki, wakapatikana wabunge wengi wa upinzani kuongoza kamati hizo, yote haya yasingetokea. CCM na NEC wasingekua wanahaha muda huu kulazimisha Chadema ipeleke majina ya viti maalumu wala wasingetuhumiwa kutengeneza orodha feki ya wabunge.
Hata hivyo Chadema imeshaweka wazi kuwa haitawatambua wabunge hao hata kama NEC itawatangaza.
Tutaelewana tu huko mbeleni.
Mambo ni fire ...Magufuli na CCM wameishiwa mbinu kisiasa.